19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

74<br />

mbele yako, tukikataa kuja kwako, basi wapi utajificha Wewe ambaye popote<br />

haupate fasi ya Wewe kupumzikia! Kwa nini utajificha Wewe usiyeacha hata mumoja wa<br />

wanadamu usiyefukuza hata mumoja? Kuja basi, ee Rabi, leo jenga hema lako ndani<br />

yangu, fanya daima nyumba yako na makao yako mpaka mwisho ndani yangu bila<br />

kutengana, mimi mtumishi wako, ewe mwema kamili, na mimi pia nikiondoka mu dunia<br />

na kisha kuondoka kwangu, nipatikane ndani yako, ee mwema kamili, na nitawale<br />

pamoja nawe, Wewe Mungu uliye juu ya yote. Kaa, ee Rabi, usiniache peke yangu,<br />

kusudi maadui zangu wakija, wao wenye kutafuta daima kurarua roho yangu, wakukute<br />

umekaa ndani yangu na wakimbie, wasambazwe bila nguvu juu yangu, wakikuona Wewe<br />

mwenye nguvu kabisa kuliko yote, wakikuona Wewe mwenye, umekaa ndani, ndani ya<br />

nyumba ya roho yangu maskini. Ndiyo, ee Rabi, kama ulivyonikumbuka mimi wakati<br />

nilikua duniani na kwa ujinga wangu ni Wewe uliyenichagua na kunitenga ku hii dunia<br />

na uliyeniweka mbele ya utukufu wako, vivyo hivyo, sasa unilinde ndani mwenyi<br />

kusimama daima, imara, katika makao yako ndani yangu; nikikuona milele mimi<br />

mwenye kufa, niishi; nikiwa na Wewe, mimi maskini, niwe daima mtajiri, mtajiri juu ya<br />

wafalme wote; wakati ninapokukukula na kukukunywa, nikikuvaa kila mara, niwe na<br />

furaha katika mema isiyokadirika: Kwa maana ni Wewe uliye mema yote, utukufu yote<br />

na furaha yote, kwa kuwa utukufu na Utatu Mtakatifu wa asili moja na wenye kuleta<br />

uzima, ni Kwako, Wewe ambaye waaminifu wote wanaheshimu, wanaungama,<br />

wanaabudu na kutumikia katika Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu daima sasa na siku<br />

zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Sala ya Mtakatifu Dimitrios, Askofu wa Rostovia-Rusia kwa Bikira Maria<br />

Mzazi-Mungu Mtakatifu kamili.<br />

Ee Bikira Mtakatifu Mzazi-Mungu, unifunike, chunga mtumishi wako kwa kila<br />

kitu mbaya yenye kutoka katika roho na mwili wangu na kwa kila adui, ya kuonekana na<br />

isiyoonekana. Salamu Maria Mjaliwa neema, Bwana ni pamoja nawe. Mbarikiwa Wewe<br />

katika wanawake wote na mbarikiwa ni tunda la tumbo lako, kwani ulizaa Mwokozi wa<br />

roho zetu. Salamu na shangilia, ee Bikira Mzazi-Mungu ombea watumishi wako. Ee<br />

Mama wa Malaika na wa waaminifu, unisaidie mimi mtumishi wako. Ee Maria uliye safi,<br />

salamu Bibi Arusi usiyeolewa. Salamu, furaha ya wenye kusikitika, utulivu ya wenye<br />

kuomboleza. Salamu, Chakula cha wenye njaa, kikavu cha wenye kuteswa baharini.<br />

Salamu, Mtakatifu kamili wa Watakatifu wote na uliye wa thamani kupita viumbe vyote.<br />

Salamu, nyumba takatifu ya Baba, hema ya Mwana, na kivuli cha Roho Mtakatifu.<br />

Salamu, nyumba kifalme ya furaha ya Mufalme Kristu Mungu wetu. Salamu, mama ya<br />

mayatima tena bakora ya vipofu. Salamu, utukufu wa waaminifu tena msaada wa wenye<br />

kukuomba. Ee Bikira wangu Mtakatifu kamili, unilinde chini ya kivuli chako; kwa maana<br />

naweka roho yangu mikononi mwako. Saidia na funika roho yangu kwa ile siku ya<br />

hukumu, ombea moyo wangu usiostahili kwa kuingia safi katika Paradizo. Usiniache<br />

mimi mtumishi wako, lakini unisaidie na unipe faida ya maombi yangu. Uniokoe kwa<br />

kila hatari, ugonjwa na mateso, na unipe kutubu mbele ya mwisho. Hivi kwa msaada<br />

wako nitaokolewa kwa kila jambo ya hii uzima katika mapenzi ya Mwana wako aliye<br />

Mungu wetu, na ku gehena ya ajabu ya milele. Amina.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!