19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

65<br />

Ukizaa mufazili, shina la uzuri tosha utajiri, wa wema kwa wote. Unaweza<br />

kutenda yote, kwani ulichukua mimba, ya Kristu Mwenyezi, ewe uliyeitwa heri na<br />

Mungu.<br />

Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Unisaidie Bikira, kwani ninajaribiwa, na magonjwa ya nguvu, na mateso ya<br />

ugonjwa. Maana ninakujua, ewe bila doa kamili, sawa hazina ya dawa, isiyomalizika.<br />

Ee Muzazi-Mungu okoa, watumishi wako kwa hatari, maana kisha Mungu wote<br />

tunakukimbilia, sawa Mulinzi na ukuta usiyobomolewa.<br />

Tazama kwa fazili, Muzazi-Mungu Musifiwa-kamili, katika taabu ya mwili<br />

wangu, na ponyesha maumivu ya nafsi yangu.<br />

KATHISMA Sauti ya mbili<br />

Upatanisho wa juhudi na ukuta wa ushindi, chemchem ya rehema, kimbilio ya<br />

watu, Bibi-Malkia Muzazi-Mungu, tunakuita daima: Utangulie kutukomboa toka hatari,<br />

uliyetunza upesi peke yako.<br />

ODE 4<br />

Irmosi<br />

Nikasikia, ee Bwana, siri ya ikonomia yako, nilifahamu kazi zako, na nilitukuza<br />

umungu wako.<br />

Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />

Tuliza sikitiko ya tamaa, na mawimbi ya makosa yangu, ewe Bibi-Arusi ya<br />

Mungu, uliyezaa Bwana Mwongozi.<br />

Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />

Wakati ninapokuita, unipe kilindi cha wema wako, uliyechukua mimba ya<br />

Mwokozi, wa wote wanaokuimbia.<br />

Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.<br />

Tukipata zawadi yako, ee safi tunaimba wimbo wa ushukuru, sisi tunaokujua, ya<br />

kama uko Muzazi-Mungu.<br />

Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Sisi tuliokupokea, Musifiwa-kamili kama matumaini, musaada na ukuta ya<br />

wokovu, tunakombolewa toka taabu yote.<br />

ODE 5<br />

Irmosi<br />

Utuangaze, kwa amri yako ee Bwana, na kwa mukono yako munyanguliwa, utupe<br />

amani yako, ee Mupenda-wanadamu.<br />

Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />

Jaza ee Safi, moyo wangu kwa furaha, ukileta shangwe yako bila doa, uliyezaa<br />

shina la furaha.<br />

Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />

Utukomboe, toka hatari, ee Muzazi-Mungu Safi, uliyezaa Mukombozi wa milele,<br />

na Amani inayopita akili zote.<br />

Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!