Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
65<br />
Ukizaa mufazili, shina la uzuri tosha utajiri, wa wema kwa wote. Unaweza<br />
kutenda yote, kwani ulichukua mimba, ya Kristu Mwenyezi, ewe uliyeitwa heri na<br />
Mungu.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Unisaidie Bikira, kwani ninajaribiwa, na magonjwa ya nguvu, na mateso ya<br />
ugonjwa. Maana ninakujua, ewe bila doa kamili, sawa hazina ya dawa, isiyomalizika.<br />
Ee Muzazi-Mungu okoa, watumishi wako kwa hatari, maana kisha Mungu wote<br />
tunakukimbilia, sawa Mulinzi na ukuta usiyobomolewa.<br />
Tazama kwa fazili, Muzazi-Mungu Musifiwa-kamili, katika taabu ya mwili<br />
wangu, na ponyesha maumivu ya nafsi yangu.<br />
KATHISMA Sauti ya mbili<br />
Upatanisho wa juhudi na ukuta wa ushindi, chemchem ya rehema, kimbilio ya<br />
watu, Bibi-Malkia Muzazi-Mungu, tunakuita daima: Utangulie kutukomboa toka hatari,<br />
uliyetunza upesi peke yako.<br />
ODE 4<br />
Irmosi<br />
Nikasikia, ee Bwana, siri ya ikonomia yako, nilifahamu kazi zako, na nilitukuza<br />
umungu wako.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Tuliza sikitiko ya tamaa, na mawimbi ya makosa yangu, ewe Bibi-Arusi ya<br />
Mungu, uliyezaa Bwana Mwongozi.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Wakati ninapokuita, unipe kilindi cha wema wako, uliyechukua mimba ya<br />
Mwokozi, wa wote wanaokuimbia.<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.<br />
Tukipata zawadi yako, ee safi tunaimba wimbo wa ushukuru, sisi tunaokujua, ya<br />
kama uko Muzazi-Mungu.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Sisi tuliokupokea, Musifiwa-kamili kama matumaini, musaada na ukuta ya<br />
wokovu, tunakombolewa toka taabu yote.<br />
ODE 5<br />
Irmosi<br />
Utuangaze, kwa amri yako ee Bwana, na kwa mukono yako munyanguliwa, utupe<br />
amani yako, ee Mupenda-wanadamu.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Jaza ee Safi, moyo wangu kwa furaha, ukileta shangwe yako bila doa, uliyezaa<br />
shina la furaha.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Utukomboe, toka hatari, ee Muzazi-Mungu Safi, uliyezaa Mukombozi wa milele,<br />
na Amani inayopita akili zote.<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.