Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
2<br />
3)Maombi ya kweli ni kuchunga akili yetu na kuinyanyua juu. Wakati<br />
tunaomba, tunaondoa mu akili yetu kila wazo la hii dunia na kazi na jamaa yetu. Na,<br />
kama tutaepuka kila kitu chenye kutuuzi, tunaweza basi kunyanyua akili na roho yetu<br />
katika sala.<br />
Somo na vitabu vya roho vinatusaidia sana kwa kuomba muzuri. Kuwa watu<br />
mengi wenyi kutayarisha roho yao mbele ya kusoma fundisho ya roho ao ukurasa mbili<br />
ya Biblia Takatifu ao kitabu ingine.<br />
Pasopo mingi kwa wale watu weingine wenye kumuzarau Mungu. Mara mingi ile<br />
mawazo inakuja wakati wa maombi yetu. Sisi, kama wanavyotushauria Watakatifu wetu,<br />
tuzarau hii mawazo mbaya, kwani ni yetu, inatoka kwa shetani.<br />
4). Wakati tunaomba, tunajikaza kusikia nini tunafanya na nini tunasema.<br />
Haifai kurudisia maombi na wimbo bila kuisikia na akili na roho yetu.<br />
Haifai kusoma ao kuimba tu na ulimi wetu, lakini akili iko mbali na inazunguka<br />
fasi ingine.<br />
5) Kabisa, wakati tunaomba inafai kufanya mzuri alama ya Msalaba na heshima,<br />
woka na mapendo ya Mungu.<br />
Msalaba ni alama Takatifu kupita alama zingine zote za Kanisa zetu.<br />
Ni kitu cha wokovu wetu. Ni bunduki mbele ya Shetani.<br />
Kila mara na alama ya Msalaba tunaanza na tunamaliza maombi yetu. Tena<br />
tunafanya alama ya musalaba kila wakati tunataka kutukuza Nyuso tatu za Utatu<br />
Mutakatifu; wakati tunakumbuka jina la Mzazi-Mungu; wakati tunakumbuka jina la<br />
Mtakatifu mumoja.<br />
6)Maombi si kitu tunakumbuka paka saa fulani ya hatari ao wakati tuko na lazima<br />
ao tunateswa. Tunamuomba Mungu hapana juu ya ma siku fulani, lakini juu ya<br />
kumutukuza na kumutolea uzima yetu ya mapendo na utii. Tena tunaomba juu ya<br />
kumushukuru sana kwani Yeye alituumba; kwani alituokoa kwa Shetani na kwa kila<br />
zambi katika sadaka ya Mwana Wake wa pekee; kwani kila siku kwa baraka yake<br />
anatupatia vitu nyingi.<br />
Bila shaka, katika kila sala yetu kuwa maombi. Kwa kila sala yetu tunamutolea<br />
Mungu maombi na mahitaji yetu. YOte tunaitoa mikononi mwake. Hapana, kwa sababu<br />
Mungu hajui mambo yetu, lakini katika hii tunaonyesha kweli mapendo na imani yetu,<br />
tunakumbuka zambi zetu na tunajinyenyekeza kwa Baba yetu Mwenyezi na Mutukufu.<br />
Pasopo kwa maombi yetu: Haifai kuomba vitu vya bure na vya upumbafu; vitu<br />
haipatane na mafundisho ya Mungu; Tuombeni vitu vyenye kutupatia sisi utukufu.<br />
Kila cha kwanza kumuomba Mungu rehema na uwangaza wake. Tena inafaa<br />
kumuomba mapenzi yake yafanyika hapana yetu sisi.<br />
7)Unyenyekevu na kulilia zambi zetu ni msingi wa sala ya kweli; Basi tunaomba<br />
inamupendeza Mungu na anaipokea. Tukijua daima zambi zetu kama alivyofanya Mtoza-<br />
Kodi katika mfano wa Evangelio ya Kristu.<br />
Wakati wa sala yetu tusiweke akili yetu fasi ingine. Haifai kujivuna, wala<br />
kusimanga watu weingine, kama alivyofanya Mufarisayo.<br />
Inafaa kusali na mapendo na furaha katika roho yetu. Hakuna kitu nzuri kupata ile<br />
sala safi tunatoa kwa Mungu.<br />
Haifai kufanya sala na uzaifu na uvivu. Sala haiko kazi sawa kazi ingine, ile<br />
tunaweza kufanya na uvivu na kisha tutalala.<br />
Wakati tunamuomba tusiangalie saa yetu. Kama tunataka kuisha mbio sala yetu, ao<br />
tunasikia ndani yetu furaha sababu sala yetu inaisha, basi, inapaswa kusikia ya kama sala<br />
yetu ilifanyikwa muzuri na ilisaidia roho yetu.