19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

75<br />

Sala ya kusoma mbele ya kila somo<br />

ya roho.<br />

Ee Rabi Mungu wetu, utukumbuke sisi wenye zambi, sisi watumishi wako<br />

wasiostahili, wakati tunapoomba jina lako takatifu, usitudanganye sisi wenye kuongojea<br />

huruma yako; lakini utupe, ee Bwana, hii yote tunaomba kwa ajili ya wokovu wetu;<br />

utupe ili tukupende na tukuogope moyoni mwetu, na tufanye mapenzi yako.<br />

Ee Mungu Mwema, utushushie sisi neema ya Roho wako Mtakatifu, mwenye<br />

kuleta na kusabitisha nguvu za roho yetu, ili tukishika mafundisho tuzidi kwa ajili ya<br />

utukufu wako, ee Muumba wetu, kwa ajili ya furaha ya wazazi wetu, kwa ajili ya faida ya<br />

Eklezya, ya inchi, na ya watu wote. AMina.<br />

Kisha somo:<br />

Tunakushukuru, ee Muumba, pakutupa sisi neema sababu ya kusikiliza<br />

mafundisho. Bariki wakubwa wetu, wazazi wetu na waalimu wenye kutuongoza kwa<br />

kutambua mema, na utupe nguvu na imara kwa kwendelesha majifunzo yetu.<br />

<strong>SALA</strong> <strong>YA</strong> MTAKATIFU YOANE KRISOSTOMO<br />

(kadiri ya saa makumi mawili na ine ya mchana na usiku)<br />

Saa ya Mchana:<br />

1. Ee Bwana, usinikatalie mema yako ya mbinguni.<br />

2. Ee Bwana, uniopoe ku mateso ya milele.<br />

3. Ee Bwana, nilitenda zambi kwa akili, kwa mawazo, kwa maneno na kwa<br />

matendo.<br />

4. Ee Bwana, uniokoe mimi ku ujinga wote, ku kusahau, ku woga na ku ugumu wa<br />

moyo.<br />

5. Ee Bwana, uniopoe ku kishawishi yote.<br />

6. Ee Bwana, angaza roho yangu yenyi giza kwa tamaa.<br />

7. Ee Bwana, mimi kama mtu, nilitenda zambi; wewe kama Mungu mkarimu,<br />

unihurumie ukiona ugonjwa wa roho yangu.<br />

8. Ee Bwana, tuma neema yako inisaidie, ili nitukuze Jina Lako takatifu.<br />

9. Ee Bwana Yesu Kristu, uniandike mimi mtumishi wako katika kitabu cha<br />

uzima, na unipe mwisho mwema.<br />

10. Ee Bwana Mungu wangu, sikutenda mema hata moja; lakini katika wema<br />

wako nitaanza.<br />

11. Ee Bwana, roho yangu ipokee umande wa neema yako.<br />

12. Ee Bwana wa mbingu na dunia, unikumbuke katika ufalme wako, mimi<br />

mutumishi wako mwenye zambi mchafu na mwenye haya. Amina.<br />

Sala ya usiku:<br />

1. Ee Bwana, kwa toba yangu, unipokee.<br />

2. Ee Bwana, usiniache.<br />

3. Ee Bwana, usiniache kuanguka katika hatari.<br />

4. Ee Bwana, unipe mawazo mazuri.<br />

5. Ee Bwana, unipe machozi, nikumbuke mauti na sikitiko.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!