Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
75<br />
Sala ya kusoma mbele ya kila somo<br />
ya roho.<br />
Ee Rabi Mungu wetu, utukumbuke sisi wenye zambi, sisi watumishi wako<br />
wasiostahili, wakati tunapoomba jina lako takatifu, usitudanganye sisi wenye kuongojea<br />
huruma yako; lakini utupe, ee Bwana, hii yote tunaomba kwa ajili ya wokovu wetu;<br />
utupe ili tukupende na tukuogope moyoni mwetu, na tufanye mapenzi yako.<br />
Ee Mungu Mwema, utushushie sisi neema ya Roho wako Mtakatifu, mwenye<br />
kuleta na kusabitisha nguvu za roho yetu, ili tukishika mafundisho tuzidi kwa ajili ya<br />
utukufu wako, ee Muumba wetu, kwa ajili ya furaha ya wazazi wetu, kwa ajili ya faida ya<br />
Eklezya, ya inchi, na ya watu wote. AMina.<br />
Kisha somo:<br />
Tunakushukuru, ee Muumba, pakutupa sisi neema sababu ya kusikiliza<br />
mafundisho. Bariki wakubwa wetu, wazazi wetu na waalimu wenye kutuongoza kwa<br />
kutambua mema, na utupe nguvu na imara kwa kwendelesha majifunzo yetu.<br />
<strong>SALA</strong> <strong>YA</strong> MTAKATIFU YOANE KRISOSTOMO<br />
(kadiri ya saa makumi mawili na ine ya mchana na usiku)<br />
Saa ya Mchana:<br />
1. Ee Bwana, usinikatalie mema yako ya mbinguni.<br />
2. Ee Bwana, uniopoe ku mateso ya milele.<br />
3. Ee Bwana, nilitenda zambi kwa akili, kwa mawazo, kwa maneno na kwa<br />
matendo.<br />
4. Ee Bwana, uniokoe mimi ku ujinga wote, ku kusahau, ku woga na ku ugumu wa<br />
moyo.<br />
5. Ee Bwana, uniopoe ku kishawishi yote.<br />
6. Ee Bwana, angaza roho yangu yenyi giza kwa tamaa.<br />
7. Ee Bwana, mimi kama mtu, nilitenda zambi; wewe kama Mungu mkarimu,<br />
unihurumie ukiona ugonjwa wa roho yangu.<br />
8. Ee Bwana, tuma neema yako inisaidie, ili nitukuze Jina Lako takatifu.<br />
9. Ee Bwana Yesu Kristu, uniandike mimi mtumishi wako katika kitabu cha<br />
uzima, na unipe mwisho mwema.<br />
10. Ee Bwana Mungu wangu, sikutenda mema hata moja; lakini katika wema<br />
wako nitaanza.<br />
11. Ee Bwana, roho yangu ipokee umande wa neema yako.<br />
12. Ee Bwana wa mbingu na dunia, unikumbuke katika ufalme wako, mimi<br />
mutumishi wako mwenye zambi mchafu na mwenye haya. Amina.<br />
Sala ya usiku:<br />
1. Ee Bwana, kwa toba yangu, unipokee.<br />
2. Ee Bwana, usiniache.<br />
3. Ee Bwana, usiniache kuanguka katika hatari.<br />
4. Ee Bwana, unipe mawazo mazuri.<br />
5. Ee Bwana, unipe machozi, nikumbuke mauti na sikitiko.