19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

6<br />

SIMVOLO <strong>YA</strong> IMANI<br />

Nasadiki Mungu mmoja Baba mwenyezi, mwumba wa mbingu na wa dunia, hata<br />

vyote vilivyoonekana na visivyoonekana, tena Bwana mmoja Yesu Kristu, Mwana wa<br />

pekee wa Mungu, aliyezaliwa na Baba mbele ya wakati wote. Nuru toka Nuru, Mungu<br />

kweli toka Mungu kweli, aliyazaliwa, si muumbwa omousion na Baba, aliye kwake vyote<br />

vilifanywa, aliye kwa ajili yetu wanadamu na ya wokovu wetu alishuka mbinguni,<br />

akapata mwili kwa Roho Mtakatifu na kwa Bikira Maria, na akawa mtu. Aliye sulibiwa<br />

kwa ajili yetu wakati wa Pontio Pilato. Akateswa, akawekwa kaburini. Na aliyefufuka<br />

katika siku ya tatu, kama yanavyo Maandiko. Na akapanda mbinguni ndipo anapokaa<br />

kuume kwa Baba. Na atakuja tena kwa utukufu kuwahukumu walio na hai na waliokufa.<br />

Ufalme wake utakuwa bila mwisho. Tena Roho Mtakatifu yu Bwana yu Mwumba hai,<br />

aliyetoka na Baba, aliyesujudiwa na kutukuzwa pamoja na Baba na Mwana, aliyenena<br />

kwa midomo ya manabii, kwa Ekklezya moja, Takatifu, Katholiki na Apostoliki.<br />

Naungama kwa ubatizo moja kwa maondoleo ya zambi. Natumaini ufufuo wa wafu hata<br />

uzima wa milele utakapokuja. Amin.<br />

DOKSOLOGIA KIDOGO<br />

Utukufu kwa Mungu juu pia, nchini amani urazi kwa wanadamu. Tukusifu,<br />

tukuhimidi, tukusujudu, tukutukuza, tukushukuru, maana utukufu wako ni mkuu. Ee<br />

Bwana mfalme, Mungu wa juu mbinguni, Baba mwenyezi, ee Bwana Mwana wa pekee<br />

Yesu Kristu na wewe Roho Mtakatifu. Ee Bwana, Mungu we, Mwana Kondoo wa<br />

Mungu, Mwana wa Baba, unazibeba zambi za dunia utuhurumie, unazibeba zambi za<br />

dunia. Upokee ombi letu, uliyeketi kuume kwa Baba na utuhurumie. Kwa kuwa<br />

Mtakatifu wa pekee, Bwana wa pekee, Yesu Kristu katika utukufu wa Mungu Baba.<br />

Amina. Kila Mangaribi nitakuhimidi, nitalisifu jina lako la milele, hata milele na milele.<br />

Ee Bwana wewe ni kimbilio letu, kizazi baada ya kizazi. Mimi nilisema: Ee Bwana,<br />

unihurumie, uiponye roho yangu, maana nimekutendea zambi. Ee Bwana, nimekimbilia<br />

kwako, unifundishe kutenda mapenzi yako, maana ndiwe Mungu wangu. Maana kwako<br />

wewe iko chemchem ya uzima; katika mwangaza wako tutaona mwangaza. Onyesha<br />

huruma yako kwao wakujue. Ee Bwana, utujalie usiku huu, kutulinda na zambi.<br />

Umehimidiwa, ee Bwana Mungu wa Baba zetu jina lako limesifiwa, na limetukuzwa<br />

milele. Amina. Ee Bwana, huruma yako iwe nasi, kama tumevyokutumainia wewe. Ee<br />

Bwana, umehimidiwa, unifundishe zilizo haki zako. Ee Rabi, umehimidiwa,<br />

unifahamishe zilizo haki zako. Ee Mtakatifu, umehimidiwa, uniangaze kwa zilizo haki<br />

zako. Ee Bwana huruma yako ni ya milele; usiache kutuangalia sisi viumbe vya mikono<br />

yako. Sifa zakulaiki, kukuimbia ni kwako, utukufu ni wako, wa Baba, na wa Mwana, na<br />

wa Roho Mtaklatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Maombi ya Saa ya kwanza:<br />

Ee Kristu, Nuru ya kweli, uliyeangaza na kutakasa kila mutu, uliyekuja duniani, na<br />

imeonekana kwetu nuru ya uso wako, ulituonyesha nuru ya uso wako isiyozimika na<br />

ongoza mwendo wetu katika kazi ya amri yako. Kwa maombezi ya Mama wako<br />

Mtakatifu na ya Watakatifu wote. Amina

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!