You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
6<br />
SIMVOLO <strong>YA</strong> IMANI<br />
Nasadiki Mungu mmoja Baba mwenyezi, mwumba wa mbingu na wa dunia, hata<br />
vyote vilivyoonekana na visivyoonekana, tena Bwana mmoja Yesu Kristu, Mwana wa<br />
pekee wa Mungu, aliyezaliwa na Baba mbele ya wakati wote. Nuru toka Nuru, Mungu<br />
kweli toka Mungu kweli, aliyazaliwa, si muumbwa omousion na Baba, aliye kwake vyote<br />
vilifanywa, aliye kwa ajili yetu wanadamu na ya wokovu wetu alishuka mbinguni,<br />
akapata mwili kwa Roho Mtakatifu na kwa Bikira Maria, na akawa mtu. Aliye sulibiwa<br />
kwa ajili yetu wakati wa Pontio Pilato. Akateswa, akawekwa kaburini. Na aliyefufuka<br />
katika siku ya tatu, kama yanavyo Maandiko. Na akapanda mbinguni ndipo anapokaa<br />
kuume kwa Baba. Na atakuja tena kwa utukufu kuwahukumu walio na hai na waliokufa.<br />
Ufalme wake utakuwa bila mwisho. Tena Roho Mtakatifu yu Bwana yu Mwumba hai,<br />
aliyetoka na Baba, aliyesujudiwa na kutukuzwa pamoja na Baba na Mwana, aliyenena<br />
kwa midomo ya manabii, kwa Ekklezya moja, Takatifu, Katholiki na Apostoliki.<br />
Naungama kwa ubatizo moja kwa maondoleo ya zambi. Natumaini ufufuo wa wafu hata<br />
uzima wa milele utakapokuja. Amin.<br />
DOKSOLOGIA KIDOGO<br />
Utukufu kwa Mungu juu pia, nchini amani urazi kwa wanadamu. Tukusifu,<br />
tukuhimidi, tukusujudu, tukutukuza, tukushukuru, maana utukufu wako ni mkuu. Ee<br />
Bwana mfalme, Mungu wa juu mbinguni, Baba mwenyezi, ee Bwana Mwana wa pekee<br />
Yesu Kristu na wewe Roho Mtakatifu. Ee Bwana, Mungu we, Mwana Kondoo wa<br />
Mungu, Mwana wa Baba, unazibeba zambi za dunia utuhurumie, unazibeba zambi za<br />
dunia. Upokee ombi letu, uliyeketi kuume kwa Baba na utuhurumie. Kwa kuwa<br />
Mtakatifu wa pekee, Bwana wa pekee, Yesu Kristu katika utukufu wa Mungu Baba.<br />
Amina. Kila Mangaribi nitakuhimidi, nitalisifu jina lako la milele, hata milele na milele.<br />
Ee Bwana wewe ni kimbilio letu, kizazi baada ya kizazi. Mimi nilisema: Ee Bwana,<br />
unihurumie, uiponye roho yangu, maana nimekutendea zambi. Ee Bwana, nimekimbilia<br />
kwako, unifundishe kutenda mapenzi yako, maana ndiwe Mungu wangu. Maana kwako<br />
wewe iko chemchem ya uzima; katika mwangaza wako tutaona mwangaza. Onyesha<br />
huruma yako kwao wakujue. Ee Bwana, utujalie usiku huu, kutulinda na zambi.<br />
Umehimidiwa, ee Bwana Mungu wa Baba zetu jina lako limesifiwa, na limetukuzwa<br />
milele. Amina. Ee Bwana, huruma yako iwe nasi, kama tumevyokutumainia wewe. Ee<br />
Bwana, umehimidiwa, unifundishe zilizo haki zako. Ee Rabi, umehimidiwa,<br />
unifahamishe zilizo haki zako. Ee Mtakatifu, umehimidiwa, uniangaze kwa zilizo haki<br />
zako. Ee Bwana huruma yako ni ya milele; usiache kutuangalia sisi viumbe vya mikono<br />
yako. Sifa zakulaiki, kukuimbia ni kwako, utukufu ni wako, wa Baba, na wa Mwana, na<br />
wa Roho Mtaklatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Maombi ya Saa ya kwanza:<br />
Ee Kristu, Nuru ya kweli, uliyeangaza na kutakasa kila mutu, uliyekuja duniani, na<br />
imeonekana kwetu nuru ya uso wako, ulituonyesha nuru ya uso wako isiyozimika na<br />
ongoza mwendo wetu katika kazi ya amri yako. Kwa maombezi ya Mama wako<br />
Mtakatifu na ya Watakatifu wote. Amina