Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
28<br />
THEOTOKION<br />
Siri ya kificho tangu milele iliyokuwa isijulikane na Malaika, imeonekana duniani<br />
katika wewe, ee Mzazi-Mungu; maana Mungu alitwaa mwili kwa ushirika, bila<br />
muchanganyo, na alikubali msalaba kwa kutaka kwake kwa ajili yetu; juu ya hii akifufua<br />
Muumbwa wa kwanza, akaokoa toka lufu nafsi yetu.<br />
IPAKOI<br />
Ee Kristu, Wabebaji manukato, watangazaji wa kwanza wa ufufuo wako, wa<br />
ajabu, wakaenda mbio kwa Mitume wakasema: Kristu amefufuka kama Mungu, analeta<br />
duniani neema kubwa.<br />
APOLITIKION<br />
Sauti ya tano<br />
Neno lasipo mwanzo pamoja na Baba na Roho, huyu alizaliwa kwa Bikira kwa<br />
ajili ya wokovu wetu; basi, waaminifu, tumwimbie na tumwabudu; kwani mapenzi yake<br />
katika mwili, alipanda juu ya msalaba, akavumilia lufu, na alifufua wafu, katika ufufuo<br />
wake muheshimiwa.<br />
THEOTOKION<br />
Salamu, mulango wa Bwana usioweza kupitwa; Salamu, ukuta na kivuli cha wale<br />
waliokimbilia kwako; salamu, kivuko bila kutikisika, na musiyeolewa, uliyezaa katika<br />
mwili Muumba na Mungu wako; usiache kupatanisha kwa ajili ya wale walikuimbia, na<br />
walioabudu Mwana wako.<br />
IPAKOI<br />
Walipoogopeshwa kwa mwangaza wa malaika, walipoangazwa kwa nuru ya ufufuo, Mirofori<br />
wakaenda mbio kwa Mitume wakasema: Tangazieni mataifa yote habari njema ya Ufufuo wa<br />
Bwana wenye kutenda hapa chini maajabu ya nuru na kutupatia neema kubwa.<br />
APOLITIKION<br />
Sauti ya sita<br />
Majeshi ya Malaika pa kaburi yako, na wachungaji walikuwa kama wafu; Maria<br />
alisimama kaburini, akitafuta mwili wako usiye na doa. Ulinyanganya Hadeze bila<br />
kujaribiwa kwake. Ulikuta Bikira, ukileta uzima. Ewe Bwana uliyefufuka katika wafu,<br />
utukufu kwako.