Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
78<br />
pasipo maana watapata haya. Unionyeshe njia zako, ee Bwana; unifundishe mapito<br />
yako. Uniongoze katika kweli yako, na kunifundisha; maana wewe ni Mungu wa wokovu<br />
wangu; nitakungojea wewe muchana kutwa. Kumbuka, ee Bwana, huruma zako na wema<br />
wako; maana zimekuwa tangu zamani. Usikumbuke zambi za ujana wangu, wala makosa<br />
yangu; unikumbuke kwa kadiri ya wema wako. Kwa ajili ya uzuri wako, ee Bwana.<br />
Bwana ni mwema na mwenye haki; kwa hivi atafundisha wenye zambi njia. Wapole<br />
atawaongoza katika hukumu, na wapole atawafundisha njia yake. Njia zote za Bwana ni<br />
wema na kweli, kwao wanaoshika agano lake na shuhuda zake. Kwa ajili ya jina lako, ee<br />
Bwana, usamehe uovu wangu, kwa kuwa ni mukubwa. Ni nani anayeogopa Bwana?<br />
Atamufundisha katika njia anayoichagua. Nafsi yake itakaa na salama; Na wazao wake<br />
watariti inchi. Siri ya Bwana ni pamoja nao wanaomwogopa; naye atawaonyesha agano<br />
lake. Macho yangu yanatazama kwa upande wa Bwana siku zote; naye atatoa miguu<br />
yangu katika wavu. Geuka kwangu, na kunihurumia; kwa sababu mimi ni mukiwa na<br />
nimeteswa. Taabu za moyo wangu zimeongezeka; unitoe katika huzuni yangu. Fikili<br />
mateso yangu na taabu yangu, na samehe zambi zangu zote. Fikili adui zangu maana wao<br />
ni wengi; na wananichukia na machukio makali. Ulinde nafsi yangu na kuniponyesha;<br />
usiniache kupata haya, maana nimekuwekea wewe tumaini langu. Ukamilifu na haki<br />
zinilinde, kwani ninakungojea wewe. Ukomboe Israeli, ee Mungu, katika taabu zake<br />
zote.<br />
ZABURI 30 (31)<br />
Nimekukimbilia wewe, ee Bwana, usiniache kupata haya milele: Kwa kila haki<br />
yako uniponyeshe. Uniinamia sikio lako, uniponyeshe mbio, uwe mwamba wangu wa<br />
nguvu, nyumba yenye boma kuniokoa. Kwa maana wewe ni mwamba wangu na boma<br />
langu, na kwa sababu ya jina lako utaniongoza na utanionyesha njia. Unitoe katika wavu<br />
walionitegea kwa siri, maana wewe ni boma langu la nguvu. Katika mukono wako<br />
ninaweka roho yangu; umenikomboa, ee Bwana, wewe Mungu wa kweli. Nimechukia<br />
wenye kuangalia maneno bule ya uwongo, lakini nimeamini Bwana. Nitafurahi na<br />
kushangilia kwa rehema yako. Kwa kuwa umeona mateso yangu, umujua roho yangu<br />
taabuni. Wala hukunifunga kwa mukono wa adui, umesimamisha miguu yangu kwa<br />
pahali pakubwa. Unirehemu, Bwana, kwa sababu niko katika taabu. Jicho langu<br />
linaharibika kwa huzuni, roho yangu na mwili wangu kwa maana maisha yangu<br />
yamekoma kwa huzuni, na miaka yangu kwa kuugua, nguvu yangu inapunguka kwa<br />
sababu ya uovu wangu, na mifupa yangu imekauka. Nimekuwa shutumu kwa adui zangu<br />
zote, lakini zaidi kwa jirani zangu, na woga kwa wenye kunijua, wenye kuniona inje<br />
walinikimbia. Nimesahauliwa kama mufu toka mawazo ya watu; nimekuwa kama<br />
chombo kilichovunjika. Maana nimesikia masingizio ya watu wengi-Maogopesho pande<br />
zote-wakati walipofanya shauri pamoja juu yangu, wafanye hila kuondoa uzima wangu.<br />
Lakini nimekutumiania wewe, ee Bwana, nimesema, wewe ni Mungu wangu. Siku zangu<br />
ni mikononi mwako; uniponyeshe kwa mukono wa adui zangu na wa wenye kunitesa.<br />
Utolee mutumwa wako nuru ya uso wako, uniokoe kwa huruma yako. Ee, Bwana,<br />
usiniache kupata haya, kwa kuwa nimekuita; acha waovu kupata haya wanyamaze kwa<br />
Hadeze. Midomo ya kusema uwongo iwe bubu, inayosema maneno magumu juu ya<br />
wenye haki kwa majivuno na kuzarau. Ee, mukubwa sana ni wema wako uliowekea<br />
wenye kukuogopa! Uliofanyia wenye kukutumainia, mbele ya wana wa watu.<br />
Utawafunika kwa maficho ya uso wako kwa fitina za mutu. Utawaficha kibandani kwa<br />
magomvi ya ndimi. Bwana abarikiwe, kwa sababu amenionyesha rehema yake ya ajabu