19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

78<br />

pasipo maana watapata haya. Unionyeshe njia zako, ee Bwana; unifundishe mapito<br />

yako. Uniongoze katika kweli yako, na kunifundisha; maana wewe ni Mungu wa wokovu<br />

wangu; nitakungojea wewe muchana kutwa. Kumbuka, ee Bwana, huruma zako na wema<br />

wako; maana zimekuwa tangu zamani. Usikumbuke zambi za ujana wangu, wala makosa<br />

yangu; unikumbuke kwa kadiri ya wema wako. Kwa ajili ya uzuri wako, ee Bwana.<br />

Bwana ni mwema na mwenye haki; kwa hivi atafundisha wenye zambi njia. Wapole<br />

atawaongoza katika hukumu, na wapole atawafundisha njia yake. Njia zote za Bwana ni<br />

wema na kweli, kwao wanaoshika agano lake na shuhuda zake. Kwa ajili ya jina lako, ee<br />

Bwana, usamehe uovu wangu, kwa kuwa ni mukubwa. Ni nani anayeogopa Bwana?<br />

Atamufundisha katika njia anayoichagua. Nafsi yake itakaa na salama; Na wazao wake<br />

watariti inchi. Siri ya Bwana ni pamoja nao wanaomwogopa; naye atawaonyesha agano<br />

lake. Macho yangu yanatazama kwa upande wa Bwana siku zote; naye atatoa miguu<br />

yangu katika wavu. Geuka kwangu, na kunihurumia; kwa sababu mimi ni mukiwa na<br />

nimeteswa. Taabu za moyo wangu zimeongezeka; unitoe katika huzuni yangu. Fikili<br />

mateso yangu na taabu yangu, na samehe zambi zangu zote. Fikili adui zangu maana wao<br />

ni wengi; na wananichukia na machukio makali. Ulinde nafsi yangu na kuniponyesha;<br />

usiniache kupata haya, maana nimekuwekea wewe tumaini langu. Ukamilifu na haki<br />

zinilinde, kwani ninakungojea wewe. Ukomboe Israeli, ee Mungu, katika taabu zake<br />

zote.<br />

ZABURI 30 (31)<br />

Nimekukimbilia wewe, ee Bwana, usiniache kupata haya milele: Kwa kila haki<br />

yako uniponyeshe. Uniinamia sikio lako, uniponyeshe mbio, uwe mwamba wangu wa<br />

nguvu, nyumba yenye boma kuniokoa. Kwa maana wewe ni mwamba wangu na boma<br />

langu, na kwa sababu ya jina lako utaniongoza na utanionyesha njia. Unitoe katika wavu<br />

walionitegea kwa siri, maana wewe ni boma langu la nguvu. Katika mukono wako<br />

ninaweka roho yangu; umenikomboa, ee Bwana, wewe Mungu wa kweli. Nimechukia<br />

wenye kuangalia maneno bule ya uwongo, lakini nimeamini Bwana. Nitafurahi na<br />

kushangilia kwa rehema yako. Kwa kuwa umeona mateso yangu, umujua roho yangu<br />

taabuni. Wala hukunifunga kwa mukono wa adui, umesimamisha miguu yangu kwa<br />

pahali pakubwa. Unirehemu, Bwana, kwa sababu niko katika taabu. Jicho langu<br />

linaharibika kwa huzuni, roho yangu na mwili wangu kwa maana maisha yangu<br />

yamekoma kwa huzuni, na miaka yangu kwa kuugua, nguvu yangu inapunguka kwa<br />

sababu ya uovu wangu, na mifupa yangu imekauka. Nimekuwa shutumu kwa adui zangu<br />

zote, lakini zaidi kwa jirani zangu, na woga kwa wenye kunijua, wenye kuniona inje<br />

walinikimbia. Nimesahauliwa kama mufu toka mawazo ya watu; nimekuwa kama<br />

chombo kilichovunjika. Maana nimesikia masingizio ya watu wengi-Maogopesho pande<br />

zote-wakati walipofanya shauri pamoja juu yangu, wafanye hila kuondoa uzima wangu.<br />

Lakini nimekutumiania wewe, ee Bwana, nimesema, wewe ni Mungu wangu. Siku zangu<br />

ni mikononi mwako; uniponyeshe kwa mukono wa adui zangu na wa wenye kunitesa.<br />

Utolee mutumwa wako nuru ya uso wako, uniokoe kwa huruma yako. Ee, Bwana,<br />

usiniache kupata haya, kwa kuwa nimekuita; acha waovu kupata haya wanyamaze kwa<br />

Hadeze. Midomo ya kusema uwongo iwe bubu, inayosema maneno magumu juu ya<br />

wenye haki kwa majivuno na kuzarau. Ee, mukubwa sana ni wema wako uliowekea<br />

wenye kukuogopa! Uliofanyia wenye kukutumainia, mbele ya wana wa watu.<br />

Utawafunika kwa maficho ya uso wako kwa fitina za mutu. Utawaficha kibandani kwa<br />

magomvi ya ndimi. Bwana abarikiwe, kwa sababu amenionyesha rehema yake ya ajabu

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!