Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
87<br />
Bwana, kama hatukukuwe na watakatifu sawa waombezi, na wema wako<br />
wenye kurehemu, tutasubutu je kukuimba, Mkombozi anayebarikiwa pasipo kupumzika<br />
na wamalaika. Wewe unajuwa mioyo, usamehe Roho zetu.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina. THEOTOKION<br />
Makosa yangu ni mengi, Mama Mzazi Mungu; nakimbilia kwako, wewe safi,<br />
naomba usalama. Angalia roho yangu yenyi ugonjwa, umuombe Mwana wako na Mungu<br />
wetu anihurumie kwa kosa nililotenda, wewe peke yako mbarikiwa.<br />
Mama Mtakatifu wa Mungu, usiniache katika maisha yangu, usinitoe ku shime ya<br />
kinadamu, lakini wewe mwenyewe unilinde na unihurumie.<br />
Naweka kitumaini kwako, Mama Mzazi wa Mungu, unilinde.<br />
Bwana, hurumia (Mara makumi Ine).<br />
Ewe Kristu Mungu unayesujudiwa, na kutukuzwa wakati wote na katika kila saa<br />
mbinguni na duniani, uliye mwadilifu, mrahimu tele, mfazili sana unayependa wenye<br />
haki, tena kuwahurumia wenye zambi; unayewaita wote kuona wokovu, ukiwaahidi vitu<br />
vema vilivyokuja; wewe, ee Bwana, hata katika saa hii uyapokee maombi yetu, na<br />
kuyashurutisha maisha yetu njiani pa amri, zako uzitakase roho zetu, uyasafishe miili<br />
zetu, uyatengeneze mafikira zetu, usinyoshe nia zetu; ukatuokoe na kila shida, ubaya, na<br />
teso, utulindie kwa Malaika wako, ili sisi tukiwa na utunzi na uongozi wao, tufike katika<br />
umoja wa imani na kuujulisha utukufu wako usiofifika. Kwa kuwa unahimidiwa milele<br />
na milele. Amina.<br />
Bwana hurumia (Mara tatu).<br />
Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Uliye watamani.. .<br />
Kisha tutapiga magoti mara tatu na tutasema hii Sala ya Mtakatifu Efrem.<br />
Bwana, ondosha mbali na mimi nia ya uvivu, ya kupoteza, ya mamlaka na ya<br />
masauti bure.<br />
(Metania Mkubwa).<br />
Umupe mtumishi wako roho ya kadiri, ya unyenyekevu, ya uvumilivu na ya<br />
mapendo<br />
(Metania Mkubwa).<br />
Ndiyo, Bwana na Mfalme, unipe nione makosa yangu, nisiamue ndugu yangu,<br />
kwani unabarikiwa milele na milele. Amina. (Metania Mkubwa).<br />
Trisagion: Mungu Mutakatifu.. . Utatu Mtakatifu.. . Baba yetu.. .<br />
Bwana hurumia, Bwana hurumia, Bwana hurumia, na utusaidie na wokovu sisi<br />
Bikira Maria.<br />
<strong>SALA</strong> KWA BIKIRA MARIA MZAZI MUNGU MTAKATIFU KAMILI.<br />
Ewe Bibi Malkia; uliye bila doa, bila waa, bila uchafu, safi kamili Bikira Bibi<br />
Mungu, uliyemwunganisha Mungu Mwana, na wanadamu kwa uzazi wako wa ajabu, na<br />
kuuchanganisha uumba wetu, uliokuwa ondoshwa, nao walio mbinguni, uliye peke yako<br />
matumaini ya wakufa moyo, na msaada wa washawishwa, uliye tayari kuwalinda wote<br />
wanakukimbilia wewe; wewe makimbilio ya wa Kristu wote, usinikiri mimi mtu mwenye<br />
zambi, mtu wa waa; niliofanya kufaa hata si kitu kwa mafikiri, na maneno, na matendo<br />
yangu ya aibu, tena kuwa mtumwa hiari wa anasa kihebu ya maisha kwa uzembe wangu.<br />
Lakini kwa kuwa wewe ni Mama wa Mungu Mpenda Wanadamu, unirehemu kwa