Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
7<br />
Kwa maombezi ya Wapadri wetu Watakatifu, ee Bwana Yesu Kristu Mungu<br />
wetu, utuhurumie na utuokoe. Amina.<br />
Eksapsalmos ni kipande cha kwanza cha sala yetu ya kila siku asubui.<br />
Eksapsalmos iko na zaburi nzuri sana sita toka zaburi za Nabii na Mfalme Daudi.<br />
WaKristiani wengi weko na zwezo nzuri, wakati hawawezi kuingia asubui mu Misa<br />
juu ya kusikia sala yote asubui, wanasoma nyumbani mwao Sala ya asubui na hii<br />
Eksapsalmos.<br />
EKSAPSALMOS<br />
Utukufu kwa Mungu juu pia, na nchini amani, urazi kwa wanadamu (Mara tatu).<br />
Ee Bwana, uifungue midomo yangu, na kinywa changu kitazinena sifa zako<br />
(Mara mbili).<br />
ZABURI 3<br />
Bwana, watesi wangu wamezidi kwangu! Wao ni wengi wanaosimama juu yangu.<br />
Wao ni wengi wanaoniambia nafsi yangu, hana wokovu kwa Bwana. Lakini wewe, ee<br />
Bwana, ni ngabo yangu pande zote; Utukufu wangu, na mwenye kunyanyua kichwa<br />
changu, nimelia kwa Bwana na sauti yangu, naye amenijibu toka mulima wake<br />
mutakatifu. Nililala na kupata usingizi; nikaamka; kwa kuwa Bwana amenitegemeza.<br />
Sitaogopa elfu kumi za watu waliojipanga juu yangu, pande zote. Simama, ee Bwana;<br />
uniokoe, ee Mungu wangu; Maana umepiga kituguta cha adui zangu zote; umevunja<br />
meno ya waovu. Wokovu ni wa Bwana; Baraka yako iwe juu ya watu wako.<br />
Na tena:<br />
Nililala na kupata usingizi; nikaamka; kwa kuwa Bwana amenitegemeza.<br />
ZABURI 37 (38).<br />
Ee Bwana, usinihamakie katika gazabu yako; wala usiniazibu kwa ukali wa hasira<br />
yako. Kwa sababu mishale yako imenichoma, na mkono wako umenipata. Hakuna uzima<br />
katika mwili wangu kwa sababu ya gazabu yako; wala hakuna afya mifupani mwangu<br />
kwa sababu ya zambi yangu. Kwa sababu zambi zangu zimenifunikiza kichwa changu;<br />
kama muzigo kunishinda. Vidonda vyangu vinanuka, vimeoza, kwa sababu ya upumbafu<br />
wangu. Nimepindika na kuinama sana; muchana kutwa ninakwenda nikiomboleza. Kwa<br />
sababu viuno vyangu vinajaa homa; wala hakuna uzima katika mwili wangu. Mimi ni<br />
zaifu na nimepondwa sana; nimeugua kwa sababu ya masumbuko ya moyo wangu.<br />
Bwana, hamu yangu yote ni mbele yako; na kuugua kwangu hakufichwi mbele yako.<br />
Moyo wangu unapigapiga, nguvu zangu zimeniacha; Nayo nuru ya macho yangu<br />
imeniondokea. Wanaonipenda na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu; na<br />
jamaa zangu wanasimama mbali. Wao vilevile wanaotafuta uzima wangu wananiwekea