19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

83<br />

mangaribi, tuwe wastahilivu wenyi kupumzika usiku pasipo ugombezi, kwa<br />

boma la uovu wowote. Utuokoe koka mashaka na woga shetani alituwekea. Leta rohoni<br />

mwetu toba ya zambi, kwa mawazo yetu, kukumbuka hukumu yako ya kweli na ya<br />

kyogopesha. Utoboe mwili wetu kwa woga wako, regeza watu wa dunia: Kwa hivi katika<br />

mapumziko ya usingizi, tutaangazwa na matezamo ya hukumu zako. Ondosha kwetu<br />

wazo lote mbaya, na tamaa yenyi kuzuru. Utuamushe wakati wa sala, tuwe wenyi<br />

kujikaza kwa imani, na kutembee katika njia za kawaida, kwa wema na haki ya Mwana<br />

wako, ambaye unahimidiwa, pamoja naye, na Roho Mtakatifu mwenyi haki na mwenyi<br />

kuleta uhai, sasa na siku zote hata milele na milele. Amina.<br />

Njooni tumwinamie na tumusujudu Mungu Mfalme wetu.<br />

Njooni tumwinamie Kristu aliye Mfalme wetu.<br />

Njooni tumwinamie yeye Kristu aliye Mfalme na Mungu wetu.<br />

ZABURI 50 (51).. .<br />

Unirehemu, ee Mungu, sawasawa na wema wako; sawasawa na wingi wa rehema<br />

zako uzime makosa yangu. Unioshe kabisa na uovu wangu, na kunisafisha na zambi<br />

yangu. Maana ninajua makosa yangu, na zambi yangu ni mbele yangu daima.<br />

Nimekukosea wewe peke yako, na kufanya yaliyo mabaya machoni mwako; ili ujulikane<br />

kuwa mwenye haki wakati unaposema, na kuwa safi wakati unapotoa hukumu. Tazama,<br />

niliumbwa katika hali ya uovu; na katika makosa mama yangu alinichukua mimba.<br />

Tazama, wewe unataka kweli moyoni, na kwa siri utanijulisha hekima. Unisafishe kwa<br />

hisopo na nitakuwa safi; unioshe, na nitakuwa mweupe kupita theluji. Unifanye kusikia<br />

furaha na shangwe; ili mifupa uliyovunja ifurahi. Ufiche uso wako usitazame zambi<br />

zangu; na uzime maovu yangu yote. Umba moyo safi ndani yangu, ee Mungu, na ufanye<br />

upya roho nzuri ndani yangu. Usinitenge na uso wako, wala usiondolee Roho yako<br />

mutakatifu. Unirudishie furaha ya wokovu wako; unitegemeze kwa roho ya tayari. Halafu<br />

nitafundisha wenye makosa njia zako; na wenye zambi watarudi kwako. Uniponyeshe na<br />

damu ya watu, ee Mungu, wewe Mungu wa wokovu wangu; ulimi wangu utaimba na<br />

sauti haki yako. Ee Bwana, ufungue midomo yangu, na kinywa changu kitaonyesha sifa<br />

zako. Maana hupendezwi na zabihu, ao ningeitoa, hufurahi kwa sadaka ya kuteketezwa.<br />

Zabihu za Mungu ni roho ya kuvunjika, moyo uliovunjika na wa toba hutauzarau, ee<br />

Mungu. Utendee Sayuni mema kwa mapenzi yako, ujenge kuta za Yerusalema. Halafu<br />

utafurahi kwa zabihu za haki, kwa sadaka ya kuteketezwa, na sadaka nzima ya<br />

kuteketezwa; halafu watatoa ngombe ndume juu ya masabahu yako.<br />

ZABURI 101 (102)<br />

Sikia maombi yangu, ee Bwana, na kilio changu kikufikie. Usinifichie uso wako<br />

kwa siku ya taabu yangu: Unitegee sikio lako; kwa siku ninapoita unijibu mbio. Maana<br />

siku zangu zinaharibika kama moshi, na mifupa yangu imeteketea kama ukuni unaowaka.<br />

Moyo wangu umepigwa kama majani, na umekauka, maana nilisahabu kula chakula<br />

changu. Kwa sababu ya sauti ya kuugua kwangu mifupa yangu inafungana na nyama<br />

yangu. Mimi ni kama mwari ya jangwa; nimekuwa kama bundi ya pahali pa ukiwa.<br />

Ninakesha, na nimekuwa kama zawaradi aliye peke yake juu ya dari ya nyumba. Adui<br />

zangu wananilaumu muchana kutwa; wao wanaonikasirikia kama wazimu wanatukana<br />

kwa kunitaja mimi. Maana nimekula majivu kama chakula, na kuchanganya kinyweo<br />

changu na machozi. Kwa sababu ya gazabu yako na hasira yako: Maana umeninyanyua

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!