You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
83<br />
mangaribi, tuwe wastahilivu wenyi kupumzika usiku pasipo ugombezi, kwa<br />
boma la uovu wowote. Utuokoe koka mashaka na woga shetani alituwekea. Leta rohoni<br />
mwetu toba ya zambi, kwa mawazo yetu, kukumbuka hukumu yako ya kweli na ya<br />
kyogopesha. Utoboe mwili wetu kwa woga wako, regeza watu wa dunia: Kwa hivi katika<br />
mapumziko ya usingizi, tutaangazwa na matezamo ya hukumu zako. Ondosha kwetu<br />
wazo lote mbaya, na tamaa yenyi kuzuru. Utuamushe wakati wa sala, tuwe wenyi<br />
kujikaza kwa imani, na kutembee katika njia za kawaida, kwa wema na haki ya Mwana<br />
wako, ambaye unahimidiwa, pamoja naye, na Roho Mtakatifu mwenyi haki na mwenyi<br />
kuleta uhai, sasa na siku zote hata milele na milele. Amina.<br />
Njooni tumwinamie na tumusujudu Mungu Mfalme wetu.<br />
Njooni tumwinamie Kristu aliye Mfalme wetu.<br />
Njooni tumwinamie yeye Kristu aliye Mfalme na Mungu wetu.<br />
ZABURI 50 (51).. .<br />
Unirehemu, ee Mungu, sawasawa na wema wako; sawasawa na wingi wa rehema<br />
zako uzime makosa yangu. Unioshe kabisa na uovu wangu, na kunisafisha na zambi<br />
yangu. Maana ninajua makosa yangu, na zambi yangu ni mbele yangu daima.<br />
Nimekukosea wewe peke yako, na kufanya yaliyo mabaya machoni mwako; ili ujulikane<br />
kuwa mwenye haki wakati unaposema, na kuwa safi wakati unapotoa hukumu. Tazama,<br />
niliumbwa katika hali ya uovu; na katika makosa mama yangu alinichukua mimba.<br />
Tazama, wewe unataka kweli moyoni, na kwa siri utanijulisha hekima. Unisafishe kwa<br />
hisopo na nitakuwa safi; unioshe, na nitakuwa mweupe kupita theluji. Unifanye kusikia<br />
furaha na shangwe; ili mifupa uliyovunja ifurahi. Ufiche uso wako usitazame zambi<br />
zangu; na uzime maovu yangu yote. Umba moyo safi ndani yangu, ee Mungu, na ufanye<br />
upya roho nzuri ndani yangu. Usinitenge na uso wako, wala usiondolee Roho yako<br />
mutakatifu. Unirudishie furaha ya wokovu wako; unitegemeze kwa roho ya tayari. Halafu<br />
nitafundisha wenye makosa njia zako; na wenye zambi watarudi kwako. Uniponyeshe na<br />
damu ya watu, ee Mungu, wewe Mungu wa wokovu wangu; ulimi wangu utaimba na<br />
sauti haki yako. Ee Bwana, ufungue midomo yangu, na kinywa changu kitaonyesha sifa<br />
zako. Maana hupendezwi na zabihu, ao ningeitoa, hufurahi kwa sadaka ya kuteketezwa.<br />
Zabihu za Mungu ni roho ya kuvunjika, moyo uliovunjika na wa toba hutauzarau, ee<br />
Mungu. Utendee Sayuni mema kwa mapenzi yako, ujenge kuta za Yerusalema. Halafu<br />
utafurahi kwa zabihu za haki, kwa sadaka ya kuteketezwa, na sadaka nzima ya<br />
kuteketezwa; halafu watatoa ngombe ndume juu ya masabahu yako.<br />
ZABURI 101 (102)<br />
Sikia maombi yangu, ee Bwana, na kilio changu kikufikie. Usinifichie uso wako<br />
kwa siku ya taabu yangu: Unitegee sikio lako; kwa siku ninapoita unijibu mbio. Maana<br />
siku zangu zinaharibika kama moshi, na mifupa yangu imeteketea kama ukuni unaowaka.<br />
Moyo wangu umepigwa kama majani, na umekauka, maana nilisahabu kula chakula<br />
changu. Kwa sababu ya sauti ya kuugua kwangu mifupa yangu inafungana na nyama<br />
yangu. Mimi ni kama mwari ya jangwa; nimekuwa kama bundi ya pahali pa ukiwa.<br />
Ninakesha, na nimekuwa kama zawaradi aliye peke yake juu ya dari ya nyumba. Adui<br />
zangu wananilaumu muchana kutwa; wao wanaonikasirikia kama wazimu wanatukana<br />
kwa kunitaja mimi. Maana nimekula majivu kama chakula, na kuchanganya kinyweo<br />
changu na machozi. Kwa sababu ya gazabu yako na hasira yako: Maana umeninyanyua