Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
tatu).<br />
18<br />
Mukazi moya Mangaribi. Sauti ya ine.<br />
Bwana atasikia wakati ninapomuita (Mara tatu).<br />
Mukazi mbili Mangaribi. Sauti ya kwanza.<br />
Hakika wema na rehema zitanifuata siku zote za maisha yangu (Mara tatu).<br />
Mukazi Tatu Mangaribi. Sauti ya tano.<br />
Uniokoe, ee Mungu, kwa jina lako na unihukumu kwa uwezo wako (Mara tatu).<br />
Mukazi ine Mangaribi. Sauti ya sita.<br />
Kusaidiwa kwangu kunatoka kwa Bwana aliyefanya mbingu na dunia (Mara<br />
Mukazi tano mangaribi. sauti ya saba.<br />
Mungu ni boma langu na rehema yangu atanitangulia (Mara tatu).<br />
Mu Posho Mangaribi. Sauti ya sita.<br />
Bwana anatawala, amevikwa utukufu (Mara tatu).<br />
Kisha Prokimenon tunasoma hii sala:<br />
Ee Bwana, utujalie mangaribi hii kutulinda na zambi, umehimidiwa u, ee Mwana<br />
na Mungu wa Baba zetu, jina lako limehimidiwa na limetukuzwa milele. Amina. Ee<br />
Bwana, huruma yako iwe nasi tunavyokutumainia wewe. Ee Bwana umehimidiwa u,<br />
unifundishe zilizo haki zako. Ee Mtakatifu, umehimidiwa u, uniangaze kwa zilizo haki<br />
zako. Ee Bwana, huruma yako ni ya milele usitutoangalie sisi, viumbe vya mikono yako.<br />
Sifa zakulaiki kukuimbia ni kwako, utukuufu ni wako, wa Baba na Mwana na Roho<br />
Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Kisha tunaimba APOSTIKHA na ku mwanzo tunasoma hii kitwo:<br />
Kitwo ya kwanza:<br />
Nitanyanyua macho yangu kwako, ee mwenye kukaa mbinguni, tazama macho ya<br />
watumishi yanaangalia kwa mkono wa Bwana kama macho ya kijakazi kwa mkono wa<br />
muke wake, hivyo macho yetu yanavyoangalia kwa Bwana Mungu wetu hata<br />
akatuhurumie.<br />
Kitwo ya mbili: Utuhurumie, ee Bwana, utuhurumie, kwani tunajaa na<br />
kuzarauliwa. Nafsi yetu inajaa na kuzarau kwa wenye kukaa na salama tena na kuzarau<br />
kwa wenye kiburi.<br />
Utukufu kwa Baba, na kwa Mwana, na kwa Roho Mtakatifu, sasa na siku zote,<br />
hata milele na milele. Amina.<br />
Kisha Apostikha tunasoma hii sala ya Mtakatifu Simeoni (Luk. 2, 29)<br />
Sasa Bwana umuache mtumishi wako aende na amani, kama ulivyosema, kwa<br />
maana macho yangu yameona wokovu wako uliweka tayari mbele ya makabila yote,<br />
mwanga wa kwangazia mataifa na sifa ya kundi lako Israeli<br />
Amina.