Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
59<br />
ulishukuru mitume wako kwa chombo cha heshima, unifanye niwe makao mastahilivu<br />
ya kuja kwako. Wewe utakaokuja tena kuhukumu ulimwengu na uhaki wote, uniruhusu<br />
nami kuja mbele yako mwamzi na mwumba wangu. Kwa Baba yako na kwa Roho<br />
Mtakatifu, Mwema na Mpaji wa roho na uzima, sasa na siku zote, hata milele na milele.<br />
Amina.<br />
<strong>SALA</strong> 9<br />
<strong>YA</strong> YOANNE DAMASCENI<br />
Ninasimama mbele ya milango ya hekalu yako na mawazo mabaya yanaokataa<br />
kunitoka. Lakini wewe Kristu Mungu ulihakikisha mtoza ushuru aliyemhurumia<br />
mkanana moja aliyemfungulia mwivi milango ya mbinguni, unifungulie basi nami<br />
matunbo ya mapendo ya binadamu na unipokee nami ninakukaribia na kukugusa sawa<br />
yule mwanamke kahaba na mbawasiri, mmoja alipogusa kanzu yako: Na alipata sasa hivi<br />
kupona, na mwengine aliposhika miguu yako takatifu, aliondolewa zambi zake zote. Na<br />
vilevile nami mkosefu, wakati ninaposubutu kupokeya mwili wako kamili nisiteketezwe.<br />
Lakini unipokee sawa wale wawili na angazia makosa ya moyo wangu unaonguza<br />
uinamizi wa zambi kwa maombezi ya yule bila doa alikuzaa kwa nguvu ya mbinguni,<br />
kwa sababu uko mbarikiwa milele na milele.<br />
<strong>SALA</strong> 10 <strong>YA</strong> MTAKATIFU YOANNE KRISOSTOMO<br />
Nasadiki, ee Bwana, na naungama ya kama wewe kweli Kristu, Mwana wa Mungu<br />
mzima, ulikuja duniani kwa ajili ya kuokoa wenye zambi, ambao mimi ni wa kwanza.<br />
Nasadiki tena ya kama huu ni Mwili wako safi na hiyi ni Damu yako ya samani.<br />
Minakuomba: Unihurumie na unisamehe makosa yangu yakupenda na yasiyokupenda<br />
niliotenda kwa maneno, kwa matendo, kwa kujua ao bila kujua, tena niwe mstahilivu<br />
wakusharikia, bila hukumu, kubeba Mwili na Damu zako safi, juu ya maondoleo ya<br />
zambi zangu na sababu ya uzima wa milele. Amina.<br />
Wakati wa kukomunika ukipofika, wanasoma sala zifuatayo za Simeoni Mfasiri<br />
<strong>SALA</strong> 11 <strong>YA</strong> SIMEONI MFASIRI<br />
Angalia sasa najongea karibu ya Komonyo yako Takatifu, ee Mwumba wangu,<br />
usiniunguze ku ushariki huo. Sababu Wewe ni moto unaounguza wasiyostahili. Lakini<br />
unitakase ku aibu hiyi.<br />
Ee Mwana wa Mungu, unipokee mimi leo ku Karamu yako ya mwisho: Kwani<br />
sitafumbua siri zako kwa adui zako; sitakubusu sawa Yudasi, lakini sawa Munyanganyi,<br />
nakuungamia: Ee Bwana, unikumbuke katika ufalme wako.<br />
Akionapo Damu Kimungu, atetemeke, ee Mwanadamu, kwa sababu ni makala ya<br />
moto ilunguzayo wasiostahilivu. Mwili Kimungu unageuzwa kimungu na unalisha,<br />
unatakasa na unalisha mawazo namna isiosikilizwa<br />
Ee Kristu, kwa mapendo yako ulinipeleka ku furaha na kwa ulinzi wako ulinigeuza<br />
kuwa mtu mwengine: Choma zambi zangu kwa moto usiyo vyombo na kubali kunijaza<br />
na furaha zako, sababu nikiwa tele na furaha, nitasifu majio zako mawili, ee Wewe<br />
mjaliwa na wema.<br />
Nitaingia je, mimi msiye stahili, katika ukuu wa watakatifu wako? Nikisubutu<br />
kwingia katika nyumba ya arusi, nguo langu litanitoa, maana hayuko ya arusi na<br />
nikifwatane, malaika watanifukuza. Bwana, safisha basi mataka ya moyo wangu na<br />
uniokoe, wewe mpenda wanadamu.