19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

24<br />

kusali tuwe wahodari mu amri zako, na kuyakamata makumbusho ya hukumu<br />

yako. Tena utujalie usiku kucha tuwe na sifa yako, ili tulisifu, tulihimidi, tulitukuze jina<br />

lako linaloheshimiwa kamili, na kulipaza sana, jina la Baba, na la Mwana, na la Roho<br />

Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Ee Mzazi Mungu, Mbarikiwa, Bikira daima, Mtukufu kushinda, uipishe sala yetu<br />

kwa Mwana wako tena Mungu wetu, na kutuombea aziokoe roho zetu kwa mateteo yako.<br />

Baba ni Matumaini yangu, Mwana ni makimbilio yangu, Roho Mtakatifu ni<br />

himaya yangu. Utatu Mtakatifu, utukufu kwako.<br />

yako.<br />

Matumaini yangu yote ni kwako, ee Mama wa Mungu, unilinde chini ya himaya<br />

Ewe, Mjaliwa na neema kabisa, dunia yote inafurahi, mifano yote ya wamalaika na<br />

makabila yote ya wanadamu, na nyumba ya Mungu Takatifu, na paradizo ya akili, Bikira<br />

mrahimu, kwa hii, Mungu alichukua mwili na akajifanya mtoto, na tangu milele,<br />

alikuwako Mungu wetu. Kwa sababu utumbu wako umefanya kiti cha ufalme na utumbo<br />

wako tena umefanya mkuu kupita mbingu. Ewe, mjaliwa na neema kabisa, duniani yote<br />

inafurahi.<br />

<strong>SALA</strong> KWA MALAIKA MLINZI<br />

Malaika Mtakatifu, musimamizi wa kuchunga moyo wangu maskini na uzima<br />

wangu wa tamaa, usiniache mimi mukosefu na usinitenge kwa sababu ya ulaji wangu.<br />

Usiniachilie na shetani mwovu kwa kunikamata na kwazibisha mwili wa mauti. Sabitisha<br />

mukono wangu mwembamba na mregevu, uniongoze katika njia ya wokovu. Ndiyo, ee<br />

Malaika Mtakatifu wa Mungu, mulinzi wa moyo wangu na wa mwili maskini, unisamehe<br />

zambi zangu zote kwani nilikutukana siku zote za uzima wangu na zambi zangu za hizi<br />

siku, unifunike usiku ya leo na unichunge ku vishawishi vya shetani ili nisivute tena<br />

hasira ya Mungu na kutenda zambi ingine. Uniombee kwa Bwana ili asinisabitishe katika<br />

oga wake na anifanye mtumishi mstahilivu wa rehema yake. Amina.<br />

Kwako, jemadari kunilinda nina deni kukushukuru kwa wokovu na kushinda<br />

kwangu; Mimi mji wako, ee Mzazi Mungu. Tena kwa mamlaka yako si kushindwa, na<br />

hatari kila namna niepuke kukuimba. Kwa kelele kuu: Salamu, Bibi-arusi, usiyeolewa.<br />

Salamu Mujaliwa Mzazi-Mungu Bikira Maria, Bwana ni pamoja nawe.<br />

Unahimidiwa Wewe katika wanawake na muhimidiwa ni tunda la tumbo lako, kwani<br />

ulizaa Mwokozi wa roho zetu. (Mara tatu).<br />

Kwa maombezi ya Wapadri wetu Watakatifu, ee Bwana Yesu Kristu Mungu wetu,<br />

utuhurumie na utuokoe.<br />

Sala mbele ya kulala.<br />

Bwana hurumia wale wanatuchukia na walitutukana; fanya mema kwa wafazili<br />

(wenyi mema). Upokee maombi ya ndugu na jirani zetu kwa ajili ya wokovu na uzima<br />

wa milele. Angalia wagonjwa, uwape tunzo; ongoza wale weko juu ya bahari, sindikiza

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!