19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

48<br />

I K O S 21<br />

Kama taa yenye kwangaa katika giza, Bikira Mtakatifu anawakisha nuru ya kiroho<br />

sababu ya kutuongoza wote ku maarifa ya mbinguni; tutukuze mwangaza wake wenye<br />

kustahili zaidi nyimbo zetu:<br />

Salamu, mwangaza wa Jua la wakristu;<br />

Salamu, mwana wa Nuru ya milele;<br />

Salamu, umeme wenye kuangaza mioyo yetu;<br />

Salamu, mungurumo wenye kumuogopesha Adui.<br />

Salamu, Mtume-mbebaji taa takatifu;<br />

Salamu, pwani kunakoingia mto wa maji mengi;<br />

Salamu, mfano takatifu na wa hai wa kisima cha maji ya ubatizo;<br />

Salamu, kwani unaondoa alama ya zambi mioyoni mwetu.<br />

Salamu, Bikira munamosafishwa zamiri yenyewe;<br />

Salamu, kikombe chenye kutapanya furaha na uzima; ;<br />

Salamu, manukato ya harufu nzuri ya kiroho; ;<br />

Salamu, nuru ya hai ya Karamu ya mbinguni.<br />

Salamu, Bibi-Arusi Usiyeolewa.<br />

I K O S 22<br />

Alipotaka kuwasamehe wenye deni wake wa zamani, huyu mwenye kuhurumia<br />

deni za wanadamu alikuja kwa kutaka kwake kuwaletea neema wale waliojitenga mbali;<br />

alipopasua hati ya deni zetu, akasikia watu wote wakimuimbia:<br />

Alliluya.<br />

I K O S 23<br />

Tunaposifu uzazi wako, tunakutukuza ewe Mtakatifu Mzazi-Mungu, hekalu la hai<br />

alimokaa Bwana wa milele, na alipokutakasa na kukutukuza, akatufundisha wote tuimbe:<br />

Salamu, hema takatifu ya Mungu-Neno;<br />

Salamu, pahali takatifu kuu zaidi kuliko Patakatifu;<br />

Salamu, sanduku iliopambwa kwa zahabu na Roho Mtakatifu;<br />

Salamu, hazina ya uzima isiyomalizika.<br />

Salamu, ewe taji heshimiwa ya Wafalme Wakristu;<br />

Salamu, sifa ya kiroho ya Mapadri Watakatifu;<br />

Salamu, ewe njia pana ya Eklezia isiyotikisika;<br />

Salamu, ewe boma la Wakristu lisiloweza kuharibika.<br />

Salamu, utukufu wa ushindi wetu;<br />

Salamu, kwani katika wewe adui ameshindwa;<br />

Salamu, ewe maponyesho ya mwili wangu;<br />

Salamu, ewe wokovu wa roho yangu.<br />

Salamu, Bibi-Arusi usiyeolewa.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!