You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
48<br />
I K O S 21<br />
Kama taa yenye kwangaa katika giza, Bikira Mtakatifu anawakisha nuru ya kiroho<br />
sababu ya kutuongoza wote ku maarifa ya mbinguni; tutukuze mwangaza wake wenye<br />
kustahili zaidi nyimbo zetu:<br />
Salamu, mwangaza wa Jua la wakristu;<br />
Salamu, mwana wa Nuru ya milele;<br />
Salamu, umeme wenye kuangaza mioyo yetu;<br />
Salamu, mungurumo wenye kumuogopesha Adui.<br />
Salamu, Mtume-mbebaji taa takatifu;<br />
Salamu, pwani kunakoingia mto wa maji mengi;<br />
Salamu, mfano takatifu na wa hai wa kisima cha maji ya ubatizo;<br />
Salamu, kwani unaondoa alama ya zambi mioyoni mwetu.<br />
Salamu, Bikira munamosafishwa zamiri yenyewe;<br />
Salamu, kikombe chenye kutapanya furaha na uzima; ;<br />
Salamu, manukato ya harufu nzuri ya kiroho; ;<br />
Salamu, nuru ya hai ya Karamu ya mbinguni.<br />
Salamu, Bibi-Arusi Usiyeolewa.<br />
I K O S 22<br />
Alipotaka kuwasamehe wenye deni wake wa zamani, huyu mwenye kuhurumia<br />
deni za wanadamu alikuja kwa kutaka kwake kuwaletea neema wale waliojitenga mbali;<br />
alipopasua hati ya deni zetu, akasikia watu wote wakimuimbia:<br />
Alliluya.<br />
I K O S 23<br />
Tunaposifu uzazi wako, tunakutukuza ewe Mtakatifu Mzazi-Mungu, hekalu la hai<br />
alimokaa Bwana wa milele, na alipokutakasa na kukutukuza, akatufundisha wote tuimbe:<br />
Salamu, hema takatifu ya Mungu-Neno;<br />
Salamu, pahali takatifu kuu zaidi kuliko Patakatifu;<br />
Salamu, sanduku iliopambwa kwa zahabu na Roho Mtakatifu;<br />
Salamu, hazina ya uzima isiyomalizika.<br />
Salamu, ewe taji heshimiwa ya Wafalme Wakristu;<br />
Salamu, sifa ya kiroho ya Mapadri Watakatifu;<br />
Salamu, ewe njia pana ya Eklezia isiyotikisika;<br />
Salamu, ewe boma la Wakristu lisiloweza kuharibika.<br />
Salamu, utukufu wa ushindi wetu;<br />
Salamu, kwani katika wewe adui ameshindwa;<br />
Salamu, ewe maponyesho ya mwili wangu;<br />
Salamu, ewe wokovu wa roho yangu.<br />
Salamu, Bibi-Arusi usiyeolewa.