19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

64<br />

Utukufu kwa Baba. .. Mara ingine<br />

Sasa na siku zote. ..<br />

Sisi tusiyostahili hatutanyamaza, kusema kamwe uwezo wako ee Muzazi-Mungu.<br />

Kama wewe hungepatamisha kwanza, nani angetuokoa toka hatari mingi? Nani<br />

angetuchunga huru, mupaka sasa? Hatutaondoka mbali nawe, ee Bibi Malkia, kwani<br />

unaokoa daima watumishi wako toka mateso.<br />

Tunasoma: Zaburi 50.<br />

Kisha hii Zaburi, tunaanza kuimba hii Kanuni:<br />

ODE 1<br />

Sauti ya Mnane<br />

Irmosi:<br />

Israeli akipita Baharini, kama inchi kavu, na akikimbia ubaya wa wamisri, aliita:<br />

tuimbie, Mukombozi na Mungu wetu.<br />

WIMBO<br />

Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />

Nikiushiikwa na majaribu mingi, ninakimbilia kwako, kutafuta wokovu, Ee Mama<br />

wa Neno na Bikira, uniokoe toka masumbuko na mateso.<br />

Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />

Mashambulio ya mateso yananitikisa, yakijaza nafsi yangu, kwa muchoko mingi.<br />

Binti bila doa utulize, na amani ya Mwana na Mungu wako.<br />

Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.<br />

Ninakusihi ee Bikira uliyezaa, Mwokozi na Mungu, kusudi unikomboe toka<br />

mateso. Kwani sasa nikikukimbilia, ninanyanyua nafsi na mawazo.<br />

Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Ninapata ugonjwa kwa mwili na roho. Ee Muzazi Mungu peke, unistahilishe<br />

nipate, kupona na shuruli yako, kwani uko Muzazi wa Mungu Mwema.<br />

ODE 3<br />

Irmosi<br />

Ee Bwana Mjengaji, wa anga ya mbinguni, na Mujengazi wa Kanisa,<br />

unisimamishe, mapendoni mwako, utimilifu wa tamaa, msaada wa waaminifu, peke yako<br />

Mupenda-wanadamu.<br />

Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />

Bikira Muzazi-Mungu, ninakuweka mulinzi na kivuli, cha uzima wangu,<br />

uniongoze kwa kivuko chako, kwani uko shina ya wema, msaada wa waaminifu, peke<br />

yako musifiwa kamili.<br />

Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />

Ninakusihi ee Bikira, usambaze mutetemeko wa roho, na kizunguzungu cha<br />

muchoko wangu. Bibi arusi ya Mungu, na peke yako bila doa, ulichukua mimba ya<br />

Kristu, mukubwa wa utulivu.<br />

Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!