Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
64<br />
Utukufu kwa Baba. .. Mara ingine<br />
Sasa na siku zote. ..<br />
Sisi tusiyostahili hatutanyamaza, kusema kamwe uwezo wako ee Muzazi-Mungu.<br />
Kama wewe hungepatamisha kwanza, nani angetuokoa toka hatari mingi? Nani<br />
angetuchunga huru, mupaka sasa? Hatutaondoka mbali nawe, ee Bibi Malkia, kwani<br />
unaokoa daima watumishi wako toka mateso.<br />
Tunasoma: Zaburi 50.<br />
Kisha hii Zaburi, tunaanza kuimba hii Kanuni:<br />
ODE 1<br />
Sauti ya Mnane<br />
Irmosi:<br />
Israeli akipita Baharini, kama inchi kavu, na akikimbia ubaya wa wamisri, aliita:<br />
tuimbie, Mukombozi na Mungu wetu.<br />
WIMBO<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Nikiushiikwa na majaribu mingi, ninakimbilia kwako, kutafuta wokovu, Ee Mama<br />
wa Neno na Bikira, uniokoe toka masumbuko na mateso.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Mashambulio ya mateso yananitikisa, yakijaza nafsi yangu, kwa muchoko mingi.<br />
Binti bila doa utulize, na amani ya Mwana na Mungu wako.<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.<br />
Ninakusihi ee Bikira uliyezaa, Mwokozi na Mungu, kusudi unikomboe toka<br />
mateso. Kwani sasa nikikukimbilia, ninanyanyua nafsi na mawazo.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Ninapata ugonjwa kwa mwili na roho. Ee Muzazi Mungu peke, unistahilishe<br />
nipate, kupona na shuruli yako, kwani uko Muzazi wa Mungu Mwema.<br />
ODE 3<br />
Irmosi<br />
Ee Bwana Mjengaji, wa anga ya mbinguni, na Mujengazi wa Kanisa,<br />
unisimamishe, mapendoni mwako, utimilifu wa tamaa, msaada wa waaminifu, peke yako<br />
Mupenda-wanadamu.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Bikira Muzazi-Mungu, ninakuweka mulinzi na kivuli, cha uzima wangu,<br />
uniongoze kwa kivuko chako, kwani uko shina ya wema, msaada wa waaminifu, peke<br />
yako musifiwa kamili.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Ninakusihi ee Bikira, usambaze mutetemeko wa roho, na kizunguzungu cha<br />
muchoko wangu. Bibi arusi ya Mungu, na peke yako bila doa, ulichukua mimba ya<br />
Kristu, mukubwa wa utulivu.<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.