You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
45<br />
I K O S 10<br />
Walipokuwa wanadi wabebaji-Mungu, Majusi wakarudi ku Babyloni wakitimiza<br />
unabii wako na kukuhubiri mbele ya wote kama Kristu, wakamwacha Herodi sawasawa<br />
mpumbafu asiyejua kuimba:<br />
Alliluya.<br />
I K O S 11<br />
Ku Misri, ee Bwana, alipoangazwa na ukweli wako, ukafukuza giza ya uongo;<br />
maana sanamu zao zilishindwa na nuru yako, tena watu waliookolewa wakamwimbia<br />
Bikira:<br />
Salamu, ewe matumaini ya wanadamu na ukombozi wao;<br />
Salamu, ewe mregeo na anguko la mashetani;<br />
Salamu, ewe uliyekanyanga hila ya nyoka,<br />
Salamu, ewe uliyeangusha uongo ya sanamu.<br />
Salamu, ewe bahari uliyemzamisha Farao;<br />
Salamu, Mwamba unayowapa kinywaji wale wenye kiu ya uzima;<br />
Salamu, Mwongozi na nguzo ya moto yenye kuwaongoza walio gizani;<br />
Salamu, ewe boma la ulimwengu, pana zaidi kuliko mbingu.<br />
Salamu, kikombe munamolindwa manna mkate wa mbinguni;<br />
Salamu, mtumishi unayetayarisha furaha takatifu;<br />
Salamu, Paradizo ya siri ya inchi ya ahadi;<br />
Salamu, inchi yenye kubarikiwa vinayotaa asili na maziwa.<br />
Salamu, Bibi-Arusi Usiyeolewa.<br />
I K O S 12<br />
Simeoni alipokuwa karibu kuondoka katika dunia hii ya udanganyifu, ukapewa<br />
kwake kama kitoto; Lakini akatambua katika wewe kuwa Mungu kamili, na<br />
alipostaajabia hekima yako, akapaza sauti na kusema:<br />
Alliluya.<br />
FUNGU 3<br />
I K O S 13<br />
Mungu alifanya mpya kazi yake wakati alizaliwa mbele ya sisi viumbe vyake,<br />
akajifuma: Bila mbegu akachipuka tumboni takatifu, akailinda bila kuiharibu, ili sisi<br />
tukiona mwujiza huo, tuisifu tukisema kwa sauti kuu:<br />
Salamu, ua lisiloharibika milele;<br />
Salamu, taji ya utakatifu;<br />
Salamu, nuru ya mfano wa ufufuo;<br />
Salamu, peke yako mshindani wa Malaika na wa hali yao.<br />
Salamu, mumea wa matunda bora, wenye kulisha waaminifu;<br />
Salamu, mti wa kivuli na wa ubaridi, wa majani ya ulinzi;<br />
Salamu, kwani ulizaa Mwongozi wa wenye kupotea;