19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

45<br />

I K O S 10<br />

Walipokuwa wanadi wabebaji-Mungu, Majusi wakarudi ku Babyloni wakitimiza<br />

unabii wako na kukuhubiri mbele ya wote kama Kristu, wakamwacha Herodi sawasawa<br />

mpumbafu asiyejua kuimba:<br />

Alliluya.<br />

I K O S 11<br />

Ku Misri, ee Bwana, alipoangazwa na ukweli wako, ukafukuza giza ya uongo;<br />

maana sanamu zao zilishindwa na nuru yako, tena watu waliookolewa wakamwimbia<br />

Bikira:<br />

Salamu, ewe matumaini ya wanadamu na ukombozi wao;<br />

Salamu, ewe mregeo na anguko la mashetani;<br />

Salamu, ewe uliyekanyanga hila ya nyoka,<br />

Salamu, ewe uliyeangusha uongo ya sanamu.<br />

Salamu, ewe bahari uliyemzamisha Farao;<br />

Salamu, Mwamba unayowapa kinywaji wale wenye kiu ya uzima;<br />

Salamu, Mwongozi na nguzo ya moto yenye kuwaongoza walio gizani;<br />

Salamu, ewe boma la ulimwengu, pana zaidi kuliko mbingu.<br />

Salamu, kikombe munamolindwa manna mkate wa mbinguni;<br />

Salamu, mtumishi unayetayarisha furaha takatifu;<br />

Salamu, Paradizo ya siri ya inchi ya ahadi;<br />

Salamu, inchi yenye kubarikiwa vinayotaa asili na maziwa.<br />

Salamu, Bibi-Arusi Usiyeolewa.<br />

I K O S 12<br />

Simeoni alipokuwa karibu kuondoka katika dunia hii ya udanganyifu, ukapewa<br />

kwake kama kitoto; Lakini akatambua katika wewe kuwa Mungu kamili, na<br />

alipostaajabia hekima yako, akapaza sauti na kusema:<br />

Alliluya.<br />

FUNGU 3<br />

I K O S 13<br />

Mungu alifanya mpya kazi yake wakati alizaliwa mbele ya sisi viumbe vyake,<br />

akajifuma: Bila mbegu akachipuka tumboni takatifu, akailinda bila kuiharibu, ili sisi<br />

tukiona mwujiza huo, tuisifu tukisema kwa sauti kuu:<br />

Salamu, ua lisiloharibika milele;<br />

Salamu, taji ya utakatifu;<br />

Salamu, nuru ya mfano wa ufufuo;<br />

Salamu, peke yako mshindani wa Malaika na wa hali yao.<br />

Salamu, mumea wa matunda bora, wenye kulisha waaminifu;<br />

Salamu, mti wa kivuli na wa ubaridi, wa majani ya ulinzi;<br />

Salamu, kwani ulizaa Mwongozi wa wenye kupotea;

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!