19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

52<br />

WIMBO 7<br />

Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />

Ee, Kristu, hii Komonyo ya Fumbo ya uzima wa meilele iwe sasa kwangu<br />

Chemchem ya uzuri, mwangaza na uzima na upole na idumu ndani yangu kwa<br />

kwendelea katika fazila ya kimungu kusudi nikutukuze wewe mwema.<br />

Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />

Ee, Mpenda wa binadamu, ninapokaribia sasa na oga, mapendo na ibada yako ku<br />

mafumbo yako ya uzima wa milele, uniokoe ku mateso ya adui, uhitaji na huzuni yote ili<br />

nikuimbie wewe mbarikiwa, Bwana Mungu wa baba zetu.<br />

Mutakatifu kamili, ee Mzazi Mungu, utuokoe. THEOTOKION<br />

Ewe, Mjaliwa na rehema kimungu kupita akili, umezaa Kristu Mwokozi, wewe<br />

uliye safi, mimi mtumishi wako mwovu nataka kukaribia sasa ku mafumbo Takatifu,<br />

unisafishe niwe safi kamili toka uchafu wa mwili na wa roho.<br />

WIMBO 8<br />

Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />

Ee, Kristu, unistahilishe sasa mimi niliyepoteza tumaini lako, nisharikie mafumbo<br />

yako kimungu ya woga na Takatifu na kwa karamu yako ya mwisho.<br />

Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />

Ninakimbilia ku rehema yako, wewe mwema, ninakuita na oga: Uwe ndani yangu<br />

nami ndani yako kama ulivyoahidi. Kwani, tazama, mwamini katika rehema yako,<br />

ninakula mwili wako na ninakunya damu yako.<br />

Mutakatifu kamili, ee Mzazi Mungu, utuokoe. THEOTOKION<br />

Nikipokea moto, natetemeka kwa kuungua kama mshumaa na nyasi: Ee Fumbo<br />

yenye kuogopesha: Ee Mungu wa huruma, namna gani nitaweza kupokea mwili wako na<br />

damu yako, mimi udongo na kuwa na uzima wa milele.<br />

WIMBO 9<br />

Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />

Mwema tele ni Bwana: Onja na utasikia. Zamani alikuja jwetu na alijitoa mara<br />

moja mwenyewe katika zabibu kwa Baba, haishi kujitoa sababu ya kutakasa waale<br />

wenye kukomunika.<br />

Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />

Ee Rabi wangu mjaliwa na huruma, nitakaswe kwa moyo na kwa mwili, ee<br />

Bwana, niangae, niokoke, niwe makayo yako kwa muungano wa Fumbo zako Takatifu,<br />

wakati ninapokupokea ndani yangu na Baba wa Roho.<br />

Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />

Mwili wako na damu yako heshimiwa iwe kwangu moto na mwangaza wengi<br />

kuchoma ulimwengu wa maovu na kuteketeza miiba ya tamaa zangu zenyi kuwaka ndani<br />

yangu ili nipate kwabudu umungu wako.<br />

Mutakatifu kamili, ee Mzazi Mungu, utuokoe. THEOTOKION

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!