Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
52<br />
WIMBO 7<br />
Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />
Ee, Kristu, hii Komonyo ya Fumbo ya uzima wa meilele iwe sasa kwangu<br />
Chemchem ya uzuri, mwangaza na uzima na upole na idumu ndani yangu kwa<br />
kwendelea katika fazila ya kimungu kusudi nikutukuze wewe mwema.<br />
Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />
Ee, Mpenda wa binadamu, ninapokaribia sasa na oga, mapendo na ibada yako ku<br />
mafumbo yako ya uzima wa milele, uniokoe ku mateso ya adui, uhitaji na huzuni yote ili<br />
nikuimbie wewe mbarikiwa, Bwana Mungu wa baba zetu.<br />
Mutakatifu kamili, ee Mzazi Mungu, utuokoe. THEOTOKION<br />
Ewe, Mjaliwa na rehema kimungu kupita akili, umezaa Kristu Mwokozi, wewe<br />
uliye safi, mimi mtumishi wako mwovu nataka kukaribia sasa ku mafumbo Takatifu,<br />
unisafishe niwe safi kamili toka uchafu wa mwili na wa roho.<br />
WIMBO 8<br />
Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />
Ee, Kristu, unistahilishe sasa mimi niliyepoteza tumaini lako, nisharikie mafumbo<br />
yako kimungu ya woga na Takatifu na kwa karamu yako ya mwisho.<br />
Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />
Ninakimbilia ku rehema yako, wewe mwema, ninakuita na oga: Uwe ndani yangu<br />
nami ndani yako kama ulivyoahidi. Kwani, tazama, mwamini katika rehema yako,<br />
ninakula mwili wako na ninakunya damu yako.<br />
Mutakatifu kamili, ee Mzazi Mungu, utuokoe. THEOTOKION<br />
Nikipokea moto, natetemeka kwa kuungua kama mshumaa na nyasi: Ee Fumbo<br />
yenye kuogopesha: Ee Mungu wa huruma, namna gani nitaweza kupokea mwili wako na<br />
damu yako, mimi udongo na kuwa na uzima wa milele.<br />
WIMBO 9<br />
Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />
Mwema tele ni Bwana: Onja na utasikia. Zamani alikuja jwetu na alijitoa mara<br />
moja mwenyewe katika zabibu kwa Baba, haishi kujitoa sababu ya kutakasa waale<br />
wenye kukomunika.<br />
Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />
Ee Rabi wangu mjaliwa na huruma, nitakaswe kwa moyo na kwa mwili, ee<br />
Bwana, niangae, niokoke, niwe makayo yako kwa muungano wa Fumbo zako Takatifu,<br />
wakati ninapokupokea ndani yangu na Baba wa Roho.<br />
Utukufu kwako, ee Mungu wetu, utukufu kwako.<br />
Mwili wako na damu yako heshimiwa iwe kwangu moto na mwangaza wengi<br />
kuchoma ulimwengu wa maovu na kuteketeza miiba ya tamaa zangu zenyi kuwaka ndani<br />
yangu ili nipate kwabudu umungu wako.<br />
Mutakatifu kamili, ee Mzazi Mungu, utuokoe. THEOTOKION