You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
22<br />
SIMVOLO <strong>YA</strong> IMANI<br />
Nasadiki Mungu mmoja Baba mwenyezi, mwumba wa mbingu na wa dunia, hata<br />
vyote vilivyo onekana na visivyoonekana, tena Bwana mmoja Yesu Kristu, Mwana wa<br />
pekee wa Mungu, aliyezaliwa na Baba mbele ya wakati wote. Nuru toka Nuru, Mungu<br />
kweli toka Mungu kweli, aliyezaliwa, si Muumbwa omousion na Baba, aliye kwake<br />
vyote vilifanywa, aliye kwa ajili yetu wanadamu na ya wokovu wetu alishuka mbinguni,<br />
akapata mwili kwa Roho Mtakatifu na kwa Bikira Maria, na akawa mtu. Aliye sulibiwa<br />
kwa ajili yetu wakati wa Pontio Pilato. Akateswa, akawekwa kaburini. Na aliyefufuka<br />
katika siku ya tatu, kama yanavyo Maandiko. Na akapanda mbinguni ndipo anapokaa<br />
kuume kwa Baba. Na atakuja tena kwa utukufu kuwahukumu walio na hai na waliokufa.<br />
Ufalme wake utakuwa bila mwisho. Tena Roho Mtakatifu yu Bwana yu Mwumba hai,<br />
aliyetoka na Baba, aliyesujudiwa na kutukuzwa pamoja na Baba na Mwana, aliyenena<br />
kwa midomo ya manabii, kwa Eklezya moja, Takatifu, Katholiki na Apostoliki.<br />
Naungama kwa ubatizo moja kwa maondoleo ya zambi. Natumaini ufufuo wa wafu hata<br />
uzima wa milele utakaokuja. Amin.<br />
Niwajibu kweli, kukuita, ee Mzazi Mungu, mwenye heri daima na usiye na doa<br />
tena Mama wa Mungu wetu. Uliye wa thamani kuwashinda wa Keruvi, uliye na utukufu<br />
kuwapita bila kiasi wa Serafi. Uliye ukimzaa Mungu Neno umebaki bila kukuharibu.<br />
Uliye Mzazi-Mungu kweli, tunakutukuza wewe.<br />
Mungu Mutakatifu. .. (Mara tatu). Utukufu kwa Baba. .. Sasa na siku zote. ..<br />
Utatu Mtakatifu kamili. .. Bwana hurumia (Mara tatu).<br />
Utukufu kwa Baba. .. Sasa na siku zote. ..<br />
Baba yetu uliye mbinguni. ..<br />
Kwa kuwa ufalme na uwezo, na utukufu ni wako, Baba, na wa Mwana, na wa<br />
Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Kisha tutasoma Kontakion ya wale watakatifu wa ile siku. Kama hakuna tutasoma<br />
hii:<br />
Mungu wa mababu zetu, kwa mapendo yako umetusaidia tangu zamani mpaka<br />
sasa usituondolee huruma yako lakini kwa maombi ya mababu zetu, uiongoze amani ya<br />
uzima wetu.<br />
Kanisa yako inapamba sawa nguo nyekundu nzuri kabisa, damu ya mashahidi<br />
wako wa dunia nzima, na inapaza sauti ya ile damu ya mashahidi, Kristu tuma rehema<br />
yako ku mataifa yote, amani kwa watu wote sawa kipawa na ku roho huruma yetu.<br />
Utukufu kwa Baba. ..<br />
Kristu, pumuzisha, karibu na Mtakatifu, roho za watumishi wako kule kusio<br />
kuuma, kusio sikitiko, kusio kutoa pumuzi lakini kuliye uzima wa milele.<br />
Sasa na siku zote. ..<br />
Ee Bwana, kwa maombezi, ya Mzazi Mungu, na ya Watakatifu wote, utume amani<br />
yako na utuhurumie, kwa sababu wewe ni mwenye huruma.<br />
Bwana hurumia (Mara 40).<br />
Ewe Kristu Mungu unayesujudiwa, na kutukuzwa wakati wote na katika kila saa<br />
mbinguni na duniani, uliye mwadilifu, mrahimu tele, mfazili sana unayependa wenye<br />
haki, tena kuwahurumia wenye zambi; unayewaita wote kuona wokovu, ukiwaahidi vitu