19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

22<br />

SIMVOLO <strong>YA</strong> IMANI<br />

Nasadiki Mungu mmoja Baba mwenyezi, mwumba wa mbingu na wa dunia, hata<br />

vyote vilivyo onekana na visivyoonekana, tena Bwana mmoja Yesu Kristu, Mwana wa<br />

pekee wa Mungu, aliyezaliwa na Baba mbele ya wakati wote. Nuru toka Nuru, Mungu<br />

kweli toka Mungu kweli, aliyezaliwa, si Muumbwa omousion na Baba, aliye kwake<br />

vyote vilifanywa, aliye kwa ajili yetu wanadamu na ya wokovu wetu alishuka mbinguni,<br />

akapata mwili kwa Roho Mtakatifu na kwa Bikira Maria, na akawa mtu. Aliye sulibiwa<br />

kwa ajili yetu wakati wa Pontio Pilato. Akateswa, akawekwa kaburini. Na aliyefufuka<br />

katika siku ya tatu, kama yanavyo Maandiko. Na akapanda mbinguni ndipo anapokaa<br />

kuume kwa Baba. Na atakuja tena kwa utukufu kuwahukumu walio na hai na waliokufa.<br />

Ufalme wake utakuwa bila mwisho. Tena Roho Mtakatifu yu Bwana yu Mwumba hai,<br />

aliyetoka na Baba, aliyesujudiwa na kutukuzwa pamoja na Baba na Mwana, aliyenena<br />

kwa midomo ya manabii, kwa Eklezya moja, Takatifu, Katholiki na Apostoliki.<br />

Naungama kwa ubatizo moja kwa maondoleo ya zambi. Natumaini ufufuo wa wafu hata<br />

uzima wa milele utakaokuja. Amin.<br />

Niwajibu kweli, kukuita, ee Mzazi Mungu, mwenye heri daima na usiye na doa<br />

tena Mama wa Mungu wetu. Uliye wa thamani kuwashinda wa Keruvi, uliye na utukufu<br />

kuwapita bila kiasi wa Serafi. Uliye ukimzaa Mungu Neno umebaki bila kukuharibu.<br />

Uliye Mzazi-Mungu kweli, tunakutukuza wewe.<br />

Mungu Mutakatifu. .. (Mara tatu). Utukufu kwa Baba. .. Sasa na siku zote. ..<br />

Utatu Mtakatifu kamili. .. Bwana hurumia (Mara tatu).<br />

Utukufu kwa Baba. .. Sasa na siku zote. ..<br />

Baba yetu uliye mbinguni. ..<br />

Kwa kuwa ufalme na uwezo, na utukufu ni wako, Baba, na wa Mwana, na wa<br />

Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Kisha tutasoma Kontakion ya wale watakatifu wa ile siku. Kama hakuna tutasoma<br />

hii:<br />

Mungu wa mababu zetu, kwa mapendo yako umetusaidia tangu zamani mpaka<br />

sasa usituondolee huruma yako lakini kwa maombi ya mababu zetu, uiongoze amani ya<br />

uzima wetu.<br />

Kanisa yako inapamba sawa nguo nyekundu nzuri kabisa, damu ya mashahidi<br />

wako wa dunia nzima, na inapaza sauti ya ile damu ya mashahidi, Kristu tuma rehema<br />

yako ku mataifa yote, amani kwa watu wote sawa kipawa na ku roho huruma yetu.<br />

Utukufu kwa Baba. ..<br />

Kristu, pumuzisha, karibu na Mtakatifu, roho za watumishi wako kule kusio<br />

kuuma, kusio sikitiko, kusio kutoa pumuzi lakini kuliye uzima wa milele.<br />

Sasa na siku zote. ..<br />

Ee Bwana, kwa maombezi, ya Mzazi Mungu, na ya Watakatifu wote, utume amani<br />

yako na utuhurumie, kwa sababu wewe ni mwenye huruma.<br />

Bwana hurumia (Mara 40).<br />

Ewe Kristu Mungu unayesujudiwa, na kutukuzwa wakati wote na katika kila saa<br />

mbinguni na duniani, uliye mwadilifu, mrahimu tele, mfazili sana unayependa wenye<br />

haki, tena kuwahurumia wenye zambi; unayewaita wote kuona wokovu, ukiwaahidi vitu

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!