You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
67<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na Kwa Roho Mutakatifu.<br />
Katika Roho Mutakatifu, kila nafsi inakuwa hai, na kwa usafisho inanyanyuliwa,<br />
inaangazwa, katika Utatu Umoja, kwa siri Takatifu.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Katika Roho Mutakatifu, maji ya neema inayotelemuka inatoka, ikinywesha<br />
kiumbe kiote, kusudi kiwe na uzima.<br />
PROKIMENON<br />
Nitakumbuka jina lako, katika vizazi vyote (Mara tatu).<br />
Shairi:<br />
Sikiliza, ee Binti, na angalia, na tega sikio lako, sahau vilevile watu wako<br />
mwenyewe, na nyumba ya Baba yako, hivi Mufalme atatamani uzuri wako.<br />
EVANGELIO TAKATIFU<br />
Evangelio Takatifu katika Luka. Sura I, mashairi 39-49 na 56).<br />
Maria akaondoka siku hizi, akakwenda katika inchi ya vilima, kwa haraka hata<br />
muji mumoja wa Yudea. Akaingia katika nyumba ya Zakaria, akasalimu Elisabeti.<br />
Wakati Elisabeti aliposikia salamu ya Maria, mutoto akaruka ndani ya tumbo lake;<br />
Elisabeti akajazwa Roho Mutakatifu, akapaza sauti yake kwa nguvu, akasema:<br />
Umebarikiwa wewe katika wanawake, na uzao wa tumbo lako umebarikiwa. Neno hili<br />
limetoka wapi, mama ya Bwana wangu anakuja kwangu? Kwani tazama, sauti ya<br />
salamu yako ilipoingia masikio yangu, mutoto aliruka kwa furaha ndani ya tumbo yangu.<br />
Heri yeye aliyesadiki kwani maneno haya aliyoyasema Bwana yatatimizwa. Maria<br />
akasema: Moyo wangu unasifu Bwana na roho yangu imefurahia Mungu Mwokozi<br />
wangu. Maana ametazama unyenyekevu wa mujakazi wake, kwani tazamatangu leo<br />
vizazi vyote wataniita heri. Maana Yeye Mwenye nguvu amenitendea matendo<br />
makubwa, na jina lake ni takatifu. Maria akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, akarudi kwa<br />
nyumba yake.<br />
Sauti ya mbili<br />
Utukufu kwa Baba na Mwana na Roho Mtakatifu.<br />
Baba, Neno Roho, Utatu katika Umoja, uzime wingi wa maovu wangu.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele, Amina.<br />
Kwa upatanisho ya Mzazi-Mungu, ee Murehemu, uzime wingi wa maovu wangu.<br />
Shairi: Unirehemu, ee Mungu Murehemu, sawasawa na wema wako, sawasawa na<br />
wingi wa rehema zako, uzime makosa yangu.<br />
PROSOMION: Sauti ya Sita<br />
Usinitumainie nichungwe na mutu, lakini Bibi Malkia, pokea kusihi kwa<br />
mutumishi wako. Taabu inanipata, siweze kuvumilia, mishale ya shetani, sina kivuli,<br />
wala kimbilio, mimi maskini. Nagombanishwa pande zote, sina mufariji ila wewe. Bibi<br />
Malkia wa dunia, matumaini na mulinzi wa waaminifu, usizarau kusihi kwangu,<br />
unifanyie vilivyofaa.