19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

67<br />

Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na Kwa Roho Mutakatifu.<br />

Katika Roho Mutakatifu, kila nafsi inakuwa hai, na kwa usafisho inanyanyuliwa,<br />

inaangazwa, katika Utatu Umoja, kwa siri Takatifu.<br />

Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Katika Roho Mutakatifu, maji ya neema inayotelemuka inatoka, ikinywesha<br />

kiumbe kiote, kusudi kiwe na uzima.<br />

PROKIMENON<br />

Nitakumbuka jina lako, katika vizazi vyote (Mara tatu).<br />

Shairi:<br />

Sikiliza, ee Binti, na angalia, na tega sikio lako, sahau vilevile watu wako<br />

mwenyewe, na nyumba ya Baba yako, hivi Mufalme atatamani uzuri wako.<br />

EVANGELIO TAKATIFU<br />

Evangelio Takatifu katika Luka. Sura I, mashairi 39-49 na 56).<br />

Maria akaondoka siku hizi, akakwenda katika inchi ya vilima, kwa haraka hata<br />

muji mumoja wa Yudea. Akaingia katika nyumba ya Zakaria, akasalimu Elisabeti.<br />

Wakati Elisabeti aliposikia salamu ya Maria, mutoto akaruka ndani ya tumbo lake;<br />

Elisabeti akajazwa Roho Mutakatifu, akapaza sauti yake kwa nguvu, akasema:<br />

Umebarikiwa wewe katika wanawake, na uzao wa tumbo lako umebarikiwa. Neno hili<br />

limetoka wapi, mama ya Bwana wangu anakuja kwangu? Kwani tazama, sauti ya<br />

salamu yako ilipoingia masikio yangu, mutoto aliruka kwa furaha ndani ya tumbo yangu.<br />

Heri yeye aliyesadiki kwani maneno haya aliyoyasema Bwana yatatimizwa. Maria<br />

akasema: Moyo wangu unasifu Bwana na roho yangu imefurahia Mungu Mwokozi<br />

wangu. Maana ametazama unyenyekevu wa mujakazi wake, kwani tazamatangu leo<br />

vizazi vyote wataniita heri. Maana Yeye Mwenye nguvu amenitendea matendo<br />

makubwa, na jina lake ni takatifu. Maria akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, akarudi kwa<br />

nyumba yake.<br />

Sauti ya mbili<br />

Utukufu kwa Baba na Mwana na Roho Mtakatifu.<br />

Baba, Neno Roho, Utatu katika Umoja, uzime wingi wa maovu wangu.<br />

Sasa na siku zote, hata milele na milele, Amina.<br />

Kwa upatanisho ya Mzazi-Mungu, ee Murehemu, uzime wingi wa maovu wangu.<br />

Shairi: Unirehemu, ee Mungu Murehemu, sawasawa na wema wako, sawasawa na<br />

wingi wa rehema zako, uzime makosa yangu.<br />

PROSOMION: Sauti ya Sita<br />

Usinitumainie nichungwe na mutu, lakini Bibi Malkia, pokea kusihi kwa<br />

mutumishi wako. Taabu inanipata, siweze kuvumilia, mishale ya shetani, sina kivuli,<br />

wala kimbilio, mimi maskini. Nagombanishwa pande zote, sina mufariji ila wewe. Bibi<br />

Malkia wa dunia, matumaini na mulinzi wa waaminifu, usizarau kusihi kwangu,<br />

unifanyie vilivyofaa.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!