You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
77<br />
ZABURI 4<br />
Unijibu wakati ninapoita, ee Mungu wa haki yangu; umenifanyizia nafasi wakati<br />
nilipokuwa katika taabu; unirehemu na kusikia maombi yangu. Ee ninyi wana wa watu,<br />
hata wakati gani utukufu wangu utageuzwa kuwa zarau? Hata wakati gani mutapenda<br />
ubatili na kutafuta uwongo? Lakini mujue ya kuwa Bwana amejiwekea mutawa mbali;<br />
Bwana atasikia wakati ninapomwita, Muwe na woga wala musitende zambi; semezaneni<br />
na moyo wenu wenyewe juu ya kitanda chenu na kutulia. Toeni zabihu za haki, na<br />
wekeeni Bwana tumaini lenu. Wao ni wengi wanaosema: Nani atakayetuonyesha mema?<br />
Bwana, utunyanyulie nuru ya uso wako. Umeweka furaha moyoni mwangu, kupita<br />
furaha yao wakati wanapozidishwa nafaka na mvinyo. Katika salama nitalala na kupata<br />
usingizi, maana wewe Bwana peke yako unanikalisha na salama.<br />
ZABURI 6<br />
Ee Bwana, usinihamakie kwa kasirani yako, wala usiniazibu kwa gazabu yako.<br />
Unirehemu, ee Bwana, maana nimekauka; uniponyeshe, ee Bwana, maana mifupa yangu<br />
imefazaika. Nafsi yangu imefazaika vilevile; Nawe, ee Bwana, hata wakati gani? Rudi,<br />
ee Bwana, uokoe nafsi yangu, uniokoe kwa ajili ya wema wako. Maana katika mauti<br />
hapana ukumbusho juu yako, katika Hadeze nani atakayekupa sante? Nimechoka kwa<br />
kuungua kwangu; kila usiku ninanyeshea kitanda changu maji; ninatia malalo yangu maji<br />
kwa machozi yangu. Jicho langu limeharibika kwa sababu ya huzuni yangu; na kuchakaa<br />
kwa sababu ya watesi wangu wote. Ondokeni kwangu, ninyi wote munaotenda uovu;<br />
kwa sababu Bwana amesikia sauti ya kilio changu. Bwana amesikia kusihi kwangu;<br />
Bwana atapokea maombi yangu. Adui zangu zote watapata haya na kufazaika sana;<br />
watarudi nyuma, watapata haya kwa gafula.<br />
ZABURI 12 (13)<br />
Hata wakati gani, ee Bwana, utanisahau hata milele? Hata wakati gani utanifichia<br />
uso wako? Hata wakati gani nitafanya shauri katika nafsi yangu? Nikiwa na huzuni<br />
moyoni mwangu muchana kutwa? Hata wakati gani adui yangu atatutukuzwa juu yangu?<br />
Ee Bwana Mungu wangu, uangalie na kunijibu, tia nuru macho yangu nisilale usingizi wa<br />
mauti; adui yangu asiseme: Nimemushinda; adui zangu wasifurahi wakati<br />
ninapoondoshwa. Lakini nimeamini rehema yako; Moyo wangu utafurahi ndani ya<br />
wokovu wako; nitaimbia Bwana, kwa sababu amenitendea na ukarimu.<br />
Mara ingine:<br />
Ee Bwana Mungu wangu, uangalie na kunijibu, tia nuru macho yangu nisilale<br />
usingizi wa mauti; adui yangu asiseme: Nimemushinda.<br />
Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Aliliya, aliluya, aliluya. Bwana hurumia<br />
(Mara tatu) , Utukufu kwa baba.. . Sasa na siku.. .<br />
ZABURI 24 (25)<br />
Kwako, ee Bwana, ninanyanyua nafsi yangu. Ee Mungu wangu, nilikuwekea<br />
wewe tumaini langu, usiniache kupata haya. Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.<br />
Ndiyo, wao wanaokungojea wewe hawatapata haya, hata mumoja; wenye kutenda hila