19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

77<br />

ZABURI 4<br />

Unijibu wakati ninapoita, ee Mungu wa haki yangu; umenifanyizia nafasi wakati<br />

nilipokuwa katika taabu; unirehemu na kusikia maombi yangu. Ee ninyi wana wa watu,<br />

hata wakati gani utukufu wangu utageuzwa kuwa zarau? Hata wakati gani mutapenda<br />

ubatili na kutafuta uwongo? Lakini mujue ya kuwa Bwana amejiwekea mutawa mbali;<br />

Bwana atasikia wakati ninapomwita, Muwe na woga wala musitende zambi; semezaneni<br />

na moyo wenu wenyewe juu ya kitanda chenu na kutulia. Toeni zabihu za haki, na<br />

wekeeni Bwana tumaini lenu. Wao ni wengi wanaosema: Nani atakayetuonyesha mema?<br />

Bwana, utunyanyulie nuru ya uso wako. Umeweka furaha moyoni mwangu, kupita<br />

furaha yao wakati wanapozidishwa nafaka na mvinyo. Katika salama nitalala na kupata<br />

usingizi, maana wewe Bwana peke yako unanikalisha na salama.<br />

ZABURI 6<br />

Ee Bwana, usinihamakie kwa kasirani yako, wala usiniazibu kwa gazabu yako.<br />

Unirehemu, ee Bwana, maana nimekauka; uniponyeshe, ee Bwana, maana mifupa yangu<br />

imefazaika. Nafsi yangu imefazaika vilevile; Nawe, ee Bwana, hata wakati gani? Rudi,<br />

ee Bwana, uokoe nafsi yangu, uniokoe kwa ajili ya wema wako. Maana katika mauti<br />

hapana ukumbusho juu yako, katika Hadeze nani atakayekupa sante? Nimechoka kwa<br />

kuungua kwangu; kila usiku ninanyeshea kitanda changu maji; ninatia malalo yangu maji<br />

kwa machozi yangu. Jicho langu limeharibika kwa sababu ya huzuni yangu; na kuchakaa<br />

kwa sababu ya watesi wangu wote. Ondokeni kwangu, ninyi wote munaotenda uovu;<br />

kwa sababu Bwana amesikia sauti ya kilio changu. Bwana amesikia kusihi kwangu;<br />

Bwana atapokea maombi yangu. Adui zangu zote watapata haya na kufazaika sana;<br />

watarudi nyuma, watapata haya kwa gafula.<br />

ZABURI 12 (13)<br />

Hata wakati gani, ee Bwana, utanisahau hata milele? Hata wakati gani utanifichia<br />

uso wako? Hata wakati gani nitafanya shauri katika nafsi yangu? Nikiwa na huzuni<br />

moyoni mwangu muchana kutwa? Hata wakati gani adui yangu atatutukuzwa juu yangu?<br />

Ee Bwana Mungu wangu, uangalie na kunijibu, tia nuru macho yangu nisilale usingizi wa<br />

mauti; adui yangu asiseme: Nimemushinda; adui zangu wasifurahi wakati<br />

ninapoondoshwa. Lakini nimeamini rehema yako; Moyo wangu utafurahi ndani ya<br />

wokovu wako; nitaimbia Bwana, kwa sababu amenitendea na ukarimu.<br />

Mara ingine:<br />

Ee Bwana Mungu wangu, uangalie na kunijibu, tia nuru macho yangu nisilale<br />

usingizi wa mauti; adui yangu asiseme: Nimemushinda.<br />

Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Aliliya, aliluya, aliluya. Bwana hurumia<br />

(Mara tatu) , Utukufu kwa baba.. . Sasa na siku.. .<br />

ZABURI 24 (25)<br />

Kwako, ee Bwana, ninanyanyua nafsi yangu. Ee Mungu wangu, nilikuwekea<br />

wewe tumaini langu, usiniache kupata haya. Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.<br />

Ndiyo, wao wanaokungojea wewe hawatapata haya, hata mumoja; wenye kutenda hila

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!