Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
54<br />
milango ya milele; na mfalme wa utukufu ataingia. Nani aliye mfalme wa utukufu?<br />
Bwana mwenye nguvu na uwezo, Bwana mwenye uwezo vitani. Nyanyulisheni vichwa<br />
vyenu, ee ninyi malango, ndiyo, muvinyanyue, ninyi milango ya milele, na mfalme wa<br />
utukufu ataingia. Ni nani huyu mfalme wa utukufu? Bwana ya majeshi, yeye ni Mfalme<br />
wa utukufu. Sela.<br />
ZABURI 116, 10-19<br />
Ninaamini, kwa maana nitasema: Niliteswa sana: Nikasema katika haraka yangu:<br />
Watu wote ni wawongo. Nitamupa Bwana nini kwa ukarimu wake wote alionitendea?<br />
Nitapokea kikombe cha wokovu, na kuitia jina la Bwana. Nitalipa Bwana naziri zangu,<br />
ndiyo, mbele ya watu wake wote. Ni ya damani machoni mwa Bwana mauti ya<br />
watakatifu wake. Ee Bwana, kweli mimi ni mtumishi wako: Mimi ni mtumishi wako,<br />
mwana wa kijakazi chako; umefungua vifungo vyangu. Nitakutolea zabihu ya kushukuru,<br />
na kuita jina la Bwana. Nitalipa naziri zangu kwa Bwana, ndiyo, mbele ya watu wake<br />
wote; katika viwanja vya nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalema. Musifu<br />
Bwana.<br />
Utukufu. . . Sasa.. . Alliluya (mara tatu). Utukufu kwako, ee Mungu. Bwana<br />
hurumia (mara tatu)<br />
Kiisha anza kuimba nyimbo zifuatavyo: Sauti ya sita<br />
Zarau wovu wangu, ee Mungu wewe uliyezaliwa kwa Bikira, takasa roho yangu,<br />
ulifanye hekalu ya mwili na damu yako kuwa takatifu, kwa hasira yako usinitupe mbali<br />
ya uso wako, wewe mwenyi huruma usiyokadirikana kisilani mbele ya uso wako, wewe<br />
uliyekuwa na huruma yasiyo kipimo.<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.<br />
Nitasubutu je, mimi mwovu, kujongea mafumbo yako Takatifu? Nikijaribu<br />
kujongea pamoja na wenye kustahili nguo yangu itanitoa maana haiko ya arusi. Na<br />
nitavuta mbegu ya hukumu kwa moyoni mwangu mtenda zambi nyingi. Ee Bwana,<br />
takasa roho yangu yenyi kuchafuka na uniponye kwani wewe ni mwema na Mpenda<br />
wanadamu.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina. THEOTOKION<br />
Ee Mama wa Mungu, zambi zangu zinapita wingiu; ninakimbilia kwako Mtakatifu<br />
kwa kutafuta wokovu. Angalia moyo wangu wenye kushikwa na ugonjwa na uniombee<br />
kwa mwana wako, Mungu wetu, anisamehe mabaya yote niliofanya kwako, ewe<br />
Mbarikiwa.<br />
Paka siku kubwa ya kazi Ine Takatifu wanaongeza kusoma: Sauti ya Mnane.<br />
Mitume watukufu waliangazwa, wakati walioshwa miguu ku karamu ya mwisho,<br />
kwa ile wakati Yudasi kafiri, kwa tamaa yake mbaya, akaingia gizani na akakutoa<br />
wewe mwamuzi wa kweli, kwa mwamuzi waovu. Ee mnyanganyi, tazama ni kwa sababu<br />
ya hii amejitundika: Epuka tamaa iliyomuongoza kutendee Rabo wake maovu ya hii<br />
namna. Ee Bwana mwema wa wote, utukufu kwako.<br />
Bwana hurumia (Mara 40)