You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
79<br />
kwa muji wenye boma. Nami, nilisema kwa haraka: Nimekatika mbele ya macho<br />
yako; hata hivi ulisikia sauti ya kilio changu wakati nilipolalamika mbele yako. Pendeni<br />
Bwana, ninyi watakatifu wake wote. Bwana anachunga waaminifu na analipa kwa malipo<br />
tele mwenye kutenda kwa majivuno. Muwe hodari, moyo wenu upate nguvu, ninyi wote<br />
monaongojea Bwana.<br />
ZABURI 90 (91)<br />
Yeye anayekaa kwa pahali pa maficho yake aliye juu atakaa chini ya kivuli cha<br />
Mwenyezi. Nitasema juu ya Bwana, yeye ni pahali pangu pa kukimbilia na boma la<br />
nguvu langu, Mungu wangu ninayemwamini. Kwa maana atakuokoa toka mutego wa<br />
muwindaji ndege, na kwa tauni ya uharibifu. Na manyoya yake atakufunika. Na chini ya<br />
mabawa yake utakimbilia, kweli yake ni ngabo na kigabo. Hutaogopa kwa woga wa<br />
usiku, wala kwa mushale unaoruka muchana; kwa tauni inayotembea katika giza, wala<br />
kwa kuharibu kunakoharibu azuhuri, elfu moja wataanguka kando yako, na elfu kumi<br />
kwa mukono wako wa kuume; lakini hakutafika karibu nawe. Na macho yako tu<br />
utatazama, na kuona zawabu ya waovu. Maana wewe, ee Bwana, ni pahali pangu pa<br />
kukimbilia! Umefanya aliye juu kao lako; Mabaya hayatakupata wewe wala tauni<br />
haitafika na hema yako. Maana ataagiza malaika yake juu yako, wakuchunge katika njia<br />
zako zote. Watakuchukua juu mikononi mwao, usivunje muguu wako kwa jiwe.<br />
Utakanyaga simba na nyoka mudogo mwenye sumu, utakanyaga mwana-simba na joka.<br />
Kwa sababu ametia mapendo yake juu yangu, kwa hivi nitamuponyesha. Nitamuweka<br />
juu kwa sababu amejua jina langu. Ataniita na nitamujibu; nitakuwa pamoja naye katika<br />
taabu; nitamuponyesha na kumuheshimu. Kwa maisha ndefu nitamushibisha, na<br />
kumwonyesha wokovu wangu.<br />
Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Aliluya, aliluya, aliluya, utukufu kwako,<br />
ee Mungu. Bwana hurumia (Mara tatu). Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. .<br />
Mungu yuko pamoja nasi; yueni, ee ninyi mataifa, na kushindwa.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />
Tegeni masikio, ninyi yote, mulio mpaka mwisho wa inchi.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />
Mulio na nguvu sana mutashindwa.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />
Mukipata nguvu tena, mutashindwa tena.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />
Mukifanya shauri pamoja, litabatilika.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />
Mukisema neno, halitasimama kwenu.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />
Wala tutaogopa hofu yenu, wala tutahangaika.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />
Lakini Bwana Mungu wetu tutakayemutakasa, na yeye atakuwa maogopesho<br />
kwetu.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />
Na kama mimi namutumainia, alinitakasa.<br />
Maana Mungu yuko pamoja nasi.