19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

79<br />

kwa muji wenye boma. Nami, nilisema kwa haraka: Nimekatika mbele ya macho<br />

yako; hata hivi ulisikia sauti ya kilio changu wakati nilipolalamika mbele yako. Pendeni<br />

Bwana, ninyi watakatifu wake wote. Bwana anachunga waaminifu na analipa kwa malipo<br />

tele mwenye kutenda kwa majivuno. Muwe hodari, moyo wenu upate nguvu, ninyi wote<br />

monaongojea Bwana.<br />

ZABURI 90 (91)<br />

Yeye anayekaa kwa pahali pa maficho yake aliye juu atakaa chini ya kivuli cha<br />

Mwenyezi. Nitasema juu ya Bwana, yeye ni pahali pangu pa kukimbilia na boma la<br />

nguvu langu, Mungu wangu ninayemwamini. Kwa maana atakuokoa toka mutego wa<br />

muwindaji ndege, na kwa tauni ya uharibifu. Na manyoya yake atakufunika. Na chini ya<br />

mabawa yake utakimbilia, kweli yake ni ngabo na kigabo. Hutaogopa kwa woga wa<br />

usiku, wala kwa mushale unaoruka muchana; kwa tauni inayotembea katika giza, wala<br />

kwa kuharibu kunakoharibu azuhuri, elfu moja wataanguka kando yako, na elfu kumi<br />

kwa mukono wako wa kuume; lakini hakutafika karibu nawe. Na macho yako tu<br />

utatazama, na kuona zawabu ya waovu. Maana wewe, ee Bwana, ni pahali pangu pa<br />

kukimbilia! Umefanya aliye juu kao lako; Mabaya hayatakupata wewe wala tauni<br />

haitafika na hema yako. Maana ataagiza malaika yake juu yako, wakuchunge katika njia<br />

zako zote. Watakuchukua juu mikononi mwao, usivunje muguu wako kwa jiwe.<br />

Utakanyaga simba na nyoka mudogo mwenye sumu, utakanyaga mwana-simba na joka.<br />

Kwa sababu ametia mapendo yake juu yangu, kwa hivi nitamuponyesha. Nitamuweka<br />

juu kwa sababu amejua jina langu. Ataniita na nitamujibu; nitakuwa pamoja naye katika<br />

taabu; nitamuponyesha na kumuheshimu. Kwa maisha ndefu nitamushibisha, na<br />

kumwonyesha wokovu wangu.<br />

Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Aliluya, aliluya, aliluya, utukufu kwako,<br />

ee Mungu. Bwana hurumia (Mara tatu). Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. .<br />

Mungu yuko pamoja nasi; yueni, ee ninyi mataifa, na kushindwa.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />

Tegeni masikio, ninyi yote, mulio mpaka mwisho wa inchi.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />

Mulio na nguvu sana mutashindwa.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />

Mukipata nguvu tena, mutashindwa tena.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />

Mukifanya shauri pamoja, litabatilika.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />

Mukisema neno, halitasimama kwenu.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />

Wala tutaogopa hofu yenu, wala tutahangaika.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />

Lakini Bwana Mungu wetu tutakayemutakasa, na yeye atakuwa maogopesho<br />

kwetu.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.<br />

Na kama mimi namutumainia, alinitakasa.<br />

Maana Mungu yuko pamoja nasi.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!