19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

daima: Mungu atukuzwe. Lakini mimi ni<br />

21<br />

masikini na mwenye hitaji unisaidie mbio,<br />

ee Mungu; wewe ni musaidia wangu na mwokozi wangu; ee Bwana, usikawie.<br />

ZABURI 142 (143)<br />

Sikia maombi yangu, ee Bwana; usikilize kusihi kwangu; katika uaminifu wako<br />

unijibu, katika haki yako. Usihukumu mtumishi wako; maana machoni mwako hakuna<br />

mtu aliye hai atahesabiwa haki. Maana adui amefuata nafsi yangu; amepiga uzima wangu<br />

chini hata udongo: Amenikalisha katika pahali pa giza, kama wale waliokufa zamani.<br />

Kwa hivi roho yangu imezimia ndani yangu; moyo wangu ndani yangu ni ukiwa.<br />

Ninakumbuka siku za kale; Ninafikili matendo yako yote: Ninawaza kazi ya mikono<br />

yako. Ninakunyoshea mikono yangu; nafsi yangu inaona kiu kwa wewe, kama inchi<br />

inayochoka. Fanya mbio kwa kuni jibu, ee Bwana; roho yangu inazimia: Usinifichie uso<br />

wako; nisiwe kama wao wanaoshuka shimoni: Unifanye kusikia wema wako asubui; kwa<br />

maana ninakutumainia wewe: Unijulishe njia nitakayoikwenda; kwa maana<br />

ninakunyanyulia nafsi yangu. Uniponyeshe, ee Bwana, na adui zangu: Ninakukimbilia<br />

unifiche. Unifundishe kufanya mapenzi yako; kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu:<br />

Roho yako ni mwema; uniongoze katika inchi ya haki. Unipatize uzima, kwa ajili ya jina<br />

lako: Kwa haki yako utoe nafsi yangu katika taabu. Na kwa wema wako ukatilie mbali<br />

adui zangu, na kuwaharibu wote wanaotesa nafsi yangu; kwa maana mimi ni mtumishi<br />

wako.<br />

DOKSOLOGIA KIDOGO<br />

Utukufu kwa Mungu juu pia, nchini amani urazi kwa wanadamu. Tukusifu,<br />

tukuhimidi, tukusujudu, tukutukuza, tukushukuru, maana utukufu wako ni mkuu. Ee<br />

Bwana mfalme, Mungu wa juu mbinguni, Baba mwenyezi, ee Bwana Mwana wa pekee<br />

Yesu Kristu na wewe Roho Mtakatifu. Ee Bwana, Mungu we, Mwana Kondoo wa<br />

Mungu, Mwana wa Baba, unazibeba zambi za dunia utuhurumie, unazibeba zambi za<br />

dunia. Upokee ombi letu, uliyeketi kuume kwa Baba na utuhurumie. Kwa kuwa<br />

Mtakatifu wa pekee, Bwana wa pekee, Yesu Kristu katika utukufu wa Mungu Baba.<br />

Amina. Kila Mangaribi nitakuhimidi, nitalisifu jina lako la milele, hata milele na milele.<br />

Ee Bwana wewe ni kimbilio letu, kizazi baada ya kizazi. Mimi nilisema: Ee Bwana,<br />

unihurumie, uiponye roho yangu, maana nimekutendea zambi. Ee Bwana, nimekimbilia<br />

kwako, unifundishe kutenda mapenzi yako, maana ndiwe Mungu wangu. Maana kwako<br />

wewe iko chemchem ya uzima; katika mwangaza wako tutaona mwangaza. Onyesha<br />

huruma yako kwao wakujue. Ee Bwana, utujalie usiku huu, kutulinda na zambi.<br />

Umehimidiwa, ee Bwana Mungu wa Baba zetu jina lako limesifiwa, na limetukuzwa<br />

milele. Amina. Ee Bwana, huruma yako iwe nasi, tumevyokutumainia wewe. Ee Bwana,<br />

umehimidiwa, unifundishe zilizo haki zako. Ee Rabi, umehimidiwa, unifahamishe zilizo<br />

haki zako. Ee Mtakatifu, umehimidiwa, uniangaze kwa zilizo haki zako. Ee Bwana<br />

huruma yako ni ya milele; usiache kutuangalia sisi viumbe vya mikono yako. Sifa<br />

zakulaiki, kukuimbia ni kwako, utukufu ni wako, wa Baba, na wa Mwana, na wa Roho<br />

Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!