Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
daima: Mungu atukuzwe. Lakini mimi ni<br />
21<br />
masikini na mwenye hitaji unisaidie mbio,<br />
ee Mungu; wewe ni musaidia wangu na mwokozi wangu; ee Bwana, usikawie.<br />
ZABURI 142 (143)<br />
Sikia maombi yangu, ee Bwana; usikilize kusihi kwangu; katika uaminifu wako<br />
unijibu, katika haki yako. Usihukumu mtumishi wako; maana machoni mwako hakuna<br />
mtu aliye hai atahesabiwa haki. Maana adui amefuata nafsi yangu; amepiga uzima wangu<br />
chini hata udongo: Amenikalisha katika pahali pa giza, kama wale waliokufa zamani.<br />
Kwa hivi roho yangu imezimia ndani yangu; moyo wangu ndani yangu ni ukiwa.<br />
Ninakumbuka siku za kale; Ninafikili matendo yako yote: Ninawaza kazi ya mikono<br />
yako. Ninakunyoshea mikono yangu; nafsi yangu inaona kiu kwa wewe, kama inchi<br />
inayochoka. Fanya mbio kwa kuni jibu, ee Bwana; roho yangu inazimia: Usinifichie uso<br />
wako; nisiwe kama wao wanaoshuka shimoni: Unifanye kusikia wema wako asubui; kwa<br />
maana ninakutumainia wewe: Unijulishe njia nitakayoikwenda; kwa maana<br />
ninakunyanyulia nafsi yangu. Uniponyeshe, ee Bwana, na adui zangu: Ninakukimbilia<br />
unifiche. Unifundishe kufanya mapenzi yako; kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu:<br />
Roho yako ni mwema; uniongoze katika inchi ya haki. Unipatize uzima, kwa ajili ya jina<br />
lako: Kwa haki yako utoe nafsi yangu katika taabu. Na kwa wema wako ukatilie mbali<br />
adui zangu, na kuwaharibu wote wanaotesa nafsi yangu; kwa maana mimi ni mtumishi<br />
wako.<br />
DOKSOLOGIA KIDOGO<br />
Utukufu kwa Mungu juu pia, nchini amani urazi kwa wanadamu. Tukusifu,<br />
tukuhimidi, tukusujudu, tukutukuza, tukushukuru, maana utukufu wako ni mkuu. Ee<br />
Bwana mfalme, Mungu wa juu mbinguni, Baba mwenyezi, ee Bwana Mwana wa pekee<br />
Yesu Kristu na wewe Roho Mtakatifu. Ee Bwana, Mungu we, Mwana Kondoo wa<br />
Mungu, Mwana wa Baba, unazibeba zambi za dunia utuhurumie, unazibeba zambi za<br />
dunia. Upokee ombi letu, uliyeketi kuume kwa Baba na utuhurumie. Kwa kuwa<br />
Mtakatifu wa pekee, Bwana wa pekee, Yesu Kristu katika utukufu wa Mungu Baba.<br />
Amina. Kila Mangaribi nitakuhimidi, nitalisifu jina lako la milele, hata milele na milele.<br />
Ee Bwana wewe ni kimbilio letu, kizazi baada ya kizazi. Mimi nilisema: Ee Bwana,<br />
unihurumie, uiponye roho yangu, maana nimekutendea zambi. Ee Bwana, nimekimbilia<br />
kwako, unifundishe kutenda mapenzi yako, maana ndiwe Mungu wangu. Maana kwako<br />
wewe iko chemchem ya uzima; katika mwangaza wako tutaona mwangaza. Onyesha<br />
huruma yako kwao wakujue. Ee Bwana, utujalie usiku huu, kutulinda na zambi.<br />
Umehimidiwa, ee Bwana Mungu wa Baba zetu jina lako limesifiwa, na limetukuzwa<br />
milele. Amina. Ee Bwana, huruma yako iwe nasi, tumevyokutumainia wewe. Ee Bwana,<br />
umehimidiwa, unifundishe zilizo haki zako. Ee Rabi, umehimidiwa, unifahamishe zilizo<br />
haki zako. Ee Mtakatifu, umehimidiwa, uniangaze kwa zilizo haki zako. Ee Bwana<br />
huruma yako ni ya milele; usiache kutuangalia sisi viumbe vya mikono yako. Sifa<br />
zakulaiki, kukuimbia ni kwako, utukufu ni wako, wa Baba, na wa Mwana, na wa Roho<br />
Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.