You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
53<br />
Ee, Bibi-Arusi wetu Mungu alichukuwa mwili kwa damu yako<br />
Takatifu. Kwa hii vizazi vinakuimba; na watu mengi wenye kusikia maana wanakusifu<br />
sababu wameona waziwazi ya kama huyu alichukua mwili kwako ni Bwana wa vitu<br />
vyote.<br />
Kisha ya mashairi 9, rudi tena ku ukurasa 6 usome:<br />
Inastahili na haki. .. , Mungu Mtakatifu. .. Utukufu kwa Baba. .. Sasa na siku zote.<br />
.. Utatu Mtakatifu. .. Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote Bwana hurumia (mara<br />
tatu) Baba yetu uliye mbinguni.. . Na Sala zingine zinazofwata mpaka mwisho wa<br />
ukurasa 11.<br />
ASUBUI SIKU <strong>YA</strong> KOMONYO TAKATIFU<br />
Kisha Sala ya asubui sema:<br />
Mungu Mutakatifu, mweza Mutakatifu, msiye kufa Mutakatifu, utuhurumie (Mara<br />
tatu).<br />
Utukufu kwa Baba. .. Sasa na siku zote.. .<br />
Utatu Mutakatifu. .. Bwana hurumia (Mara tatu). Utukufu kwa Baba. .. Sasa na<br />
siku zote. ..<br />
Baba yetu uliye mbinguni. .. Bwana hurumie (Mara 12)<br />
Utukufu kwa Baba. .. Sasa na siku zote. ..<br />
Njooni tumwinamie na tumsujudu Mungu Mfalme wetu.<br />
Njooni tumwinamie na tumsujudu Kristu Yeye Mungu Mfalme wetu.<br />
Njooni tumwinamie na tumsujudu Yeye Kristu, aliye Mfalme na Mungu wetu.<br />
ZABURI 23<br />
Bwana ni mchungaji wangu; sitapungukiwa na kitu. Ananilalisha katika malisho<br />
ya majani mabichi; ananiongoza kando ya maji matulivu. Anarudisha nafsi yangu;<br />
ananiongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Ndiyo, hata nikipita kati ya bonde<br />
la kivuli cha mauti, sitaogopa mabaya; kwa maana wewe ni pamoja nami; Gongo lako na<br />
fimbo yako zinanifariji. Unanitengenezea meza mbele ya adui zangu; Umenipakalia<br />
mafuta kichwani; kikombe changu kinafurika. Hakika wema na rehema zitanifuata siku<br />
zote za maisha yangu; na nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.<br />
ZABURI 24<br />
Inchi na kujaa kwake ni mali ya Bwana; Dunia, nao wanaokaa ndani yake. Kwa<br />
maana ameweka misingi yake juu ya bahari, na kuisimamisha juu ya garika. Nani<br />
atakayepanda mulimani mwa Bwana? Na nani atakayesimama katika pahali pake<br />
patakatifu? Mtu aliye na mikono safi, na moyo mweupe; asiyenyanyua nafsi yake kwa<br />
uwongo, wala hakuapa kwa hila. Yeye atapokea baraka kwa Bwana, na haki kwa Mungu<br />
wa wokovu wake. Hiki ni kizazi chao wanaomutafuta, wanaotafuta uso wako, ee Mungu<br />
wa Yakobo. Sela. Nyanyueni vichwa vyetu, ee ninyi malango; na munyanyuliwe, ninyi