You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
63<br />
<strong>SALA</strong> <strong>YA</strong> KANUNI <strong>YA</strong> KUSIHI KIDOGO<br />
KWA BIKIRA MARIA MZAZI-MUNGU MBARIKIWA KAMILI.<br />
( Paraklisis Ndogo)<br />
Kwa Jina la Baba na la Mwana na a Roho Mtakatifi. Amina.<br />
Zaburi 142<br />
Sikia maombi yangu, ee Bwana, usikilize kusihi kwangu; katika uaminifu wako<br />
unijibu, katika haki yako. Usihukumu mutumishi wako; maana machoni mwako hakuna<br />
mutu aliye hai atahesabiwa haki. Maana adui amefuata nafsi yangu; amepiga uzima<br />
wangu chini hata udongo. Amenikalisha katika pahali pa giza, kama wale waliokufa<br />
zamani. Kwa hivi roho yangu imezimia ndani yangu; Moyo wangu ndani yangu ni ukiwa.<br />
Ninakumbuka siku za kale; ninafikili matendo yako yote; ninawaza kazi ya mikono yako.<br />
Ninakunyoshea mikono yangu; nafsi yangu inaona kiu kwa wewe, kama inchi<br />
inayochoka. Fanya mbio kwa kunijibu, ee Bwana; roho yangu inazimia; usinifichie uso<br />
wako; nisiwe kama wao wanaoshuka shimoni. Unifanye kusikia wema wako asubui; kwa<br />
maana ninakutumainia wewe; unijulishe njia nitakayoikwenda; kwa maana<br />
ninakunyanyulia nafsi yangu. Uniponyeshe, ee Bwana, na adui zangu, ninakukimbilia<br />
unifiche. Unifundishe kufanya mapenzi yako; kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu;<br />
Roho yako ni mwema; uniongoze katika inchi ya haki. Unipatize uzima, ee Bwana, kwa<br />
ajili ya jina lako; kwa haki yako utoe nafsi yangu katika taabu. Na kwa wema wako<br />
ukatilie mbali adui zangu, na kuwaharibu wote wanaotesa nafsi yangu; kwa maana mimi<br />
ni mutumishi wako.<br />
Kisha tunaimba mara Ine:<br />
Bwana ndiwe Mungu naye amefunuliwa kwetu, abarikiwe yeye ajaye kwa jina la<br />
Bwana.<br />
Kitwo: Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni Mwema, kwa maana huruma yake ni ya<br />
milele.<br />
Bwana ndiwe Mungu.. .<br />
Mataifa yote walinizunguka, kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.<br />
Bwana ndiwe Mungu.. .<br />
Mtendo huu mtendo wa Bwana, nao ni ajabu machoni mwetu.<br />
Bwana ndiwe Mungu.. .<br />
WIMBO<br />
Sauti ya Ine<br />
Tukimbilie sasa kwa Muzazi-Mungu, sisi wenye zambi na kupondwa na tusujudu,<br />
tukiita kwa kutubu toka roho: Bibi Malkia saidia, utuhurumie, fanya mbio tunapotea, kwa<br />
wingi wa makosa. Usifukuze watumishi wako kwa mikono mitupu. Kwani tulikupata,<br />
wewe peke yako matumaini.