19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

63<br />

<strong>SALA</strong> <strong>YA</strong> KANUNI <strong>YA</strong> KUSIHI KIDOGO<br />

KWA BIKIRA MARIA MZAZI-MUNGU MBARIKIWA KAMILI.<br />

( Paraklisis Ndogo)<br />

Kwa Jina la Baba na la Mwana na a Roho Mtakatifi. Amina.<br />

Zaburi 142<br />

Sikia maombi yangu, ee Bwana, usikilize kusihi kwangu; katika uaminifu wako<br />

unijibu, katika haki yako. Usihukumu mutumishi wako; maana machoni mwako hakuna<br />

mutu aliye hai atahesabiwa haki. Maana adui amefuata nafsi yangu; amepiga uzima<br />

wangu chini hata udongo. Amenikalisha katika pahali pa giza, kama wale waliokufa<br />

zamani. Kwa hivi roho yangu imezimia ndani yangu; Moyo wangu ndani yangu ni ukiwa.<br />

Ninakumbuka siku za kale; ninafikili matendo yako yote; ninawaza kazi ya mikono yako.<br />

Ninakunyoshea mikono yangu; nafsi yangu inaona kiu kwa wewe, kama inchi<br />

inayochoka. Fanya mbio kwa kunijibu, ee Bwana; roho yangu inazimia; usinifichie uso<br />

wako; nisiwe kama wao wanaoshuka shimoni. Unifanye kusikia wema wako asubui; kwa<br />

maana ninakutumainia wewe; unijulishe njia nitakayoikwenda; kwa maana<br />

ninakunyanyulia nafsi yangu. Uniponyeshe, ee Bwana, na adui zangu, ninakukimbilia<br />

unifiche. Unifundishe kufanya mapenzi yako; kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu;<br />

Roho yako ni mwema; uniongoze katika inchi ya haki. Unipatize uzima, ee Bwana, kwa<br />

ajili ya jina lako; kwa haki yako utoe nafsi yangu katika taabu. Na kwa wema wako<br />

ukatilie mbali adui zangu, na kuwaharibu wote wanaotesa nafsi yangu; kwa maana mimi<br />

ni mutumishi wako.<br />

Kisha tunaimba mara Ine:<br />

Bwana ndiwe Mungu naye amefunuliwa kwetu, abarikiwe yeye ajaye kwa jina la<br />

Bwana.<br />

Kitwo: Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni Mwema, kwa maana huruma yake ni ya<br />

milele.<br />

Bwana ndiwe Mungu.. .<br />

Mataifa yote walinizunguka, kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.<br />

Bwana ndiwe Mungu.. .<br />

Mtendo huu mtendo wa Bwana, nao ni ajabu machoni mwetu.<br />

Bwana ndiwe Mungu.. .<br />

WIMBO<br />

Sauti ya Ine<br />

Tukimbilie sasa kwa Muzazi-Mungu, sisi wenye zambi na kupondwa na tusujudu,<br />

tukiita kwa kutubu toka roho: Bibi Malkia saidia, utuhurumie, fanya mbio tunapotea, kwa<br />

wingi wa makosa. Usifukuze watumishi wako kwa mikono mitupu. Kwani tulikupata,<br />

wewe peke yako matumaini.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!