Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
66<br />
Bibi-Arusi ya Mungu, sambaza kungu ya makosa yangu, kwa mwangaza<br />
wa nuru yako, uliyezaa Nuru kimungu, kilichokuwa tangu milele.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Safi ponyesha, ugonjwa wa tamaa yangu, ukinistahilisha kupata tunzo lako, na<br />
unipe afya, kwa upatanisho wako.<br />
ODE 6<br />
Irmosi<br />
Ninamwanga, mashitaki yangu mbele ya Bwana, ninamwonyesha taabu yangu,<br />
maana nafsi yangu ilijazwa na ubaya, na uzima wangu unakaribia Hadeze, na ninakusihi<br />
kama Yuna: Mungu wangu, unitoshe toka uharibifu.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu utuokoe.<br />
Bikira, sihi Bwana na Mwana wako, aliyeokoa hali yangu iliyokamatwa, kwa<br />
mauti na uharibifu, akijitoa kwa mauti, kusudi aniponyeshe, toka uovu wa adui.<br />
Mutakatifu kamili, ee Muzazi-Mungu, utuokoe.<br />
Ninakujua, sawa mulinzi wa uzima, na muchunga wa imara ee Bikira, ukisambaza<br />
wingi wa majaribu, na ukifukuza nguvu ya shetani. Na kusihi daima uniponyeshe toka<br />
uharibifu wa tamaa yangu.<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu.<br />
Tulikupata, kama ukuta wa kimbilio, na wokovu timilifu wa nafsi yetu, na tulizo<br />
kwa taabu ee Binti, na tunashangilia kwa nuru yako daima. Bibi Malkia sasa utuokoe,<br />
toka mateso na hatari.<br />
Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Ninalala, sawa mugonjwa kitandani, na hakuna tunzo mwilini mwangu. Lakini<br />
ewe ulichukua mimba ya Mungu, na Mwokozi wa dunia na muponya magonjwa.<br />
Ninakusihi ewe Mwema, unitoshe toka magonjwa.<br />
Muzazi Mungu okoa, watumishi wako kwa hatari, maana kisha Mungu wote<br />
tunakukimbilia, sawa mulinzi na ukuta usiyobomolewa.<br />
Bikira bila uchafu, uliyezaa Neno kwa namna isiyosemwa, katika siku ya mwisho,<br />
umusihi, kwani wewe uko na uhodari ya umama.<br />
KONTAKION Sauti ya Mbili.<br />
Ee Mulinzi usiyepatisha wakristu haya, na mupatanishi wa Muumba usiyeweza<br />
kubadilika, usizarau sauti ya kusihi ya wenye-zambi. Lakini fika kama mwema, kwa<br />
kutusaidia sisi, tunaokuita na imani: Ujiharikishe kwa upatanisho, na ukimbie kwa<br />
kutuomba, ewe Muzazi-Mungu unayelinda, wanaokuheshimu daima.<br />
Kisha tunaimba Antifonon ya kwanza ya Daraja (Anavathmi)<br />
Sauti ya Ine<br />
Toka ujana wangu, tamaa mbaya mingi inanigombanisha. Lakini ewe Mwokozi<br />
wangu, unilinde na uniokoe (Mara mbili)<br />
Enyi muliochukia Sayuni, mupate haya toka Bwana. Kwani kama majani mbele ya<br />
moto, mutakuwa wakikauka (Mara mbili).