Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
16<br />
4. – Tafakari juu ya maana yake na uzingatie ukarimu wa Mola wako.<br />
5. – Tafuta – kusamehewa dhambi kwa Mungu na jifunze<br />
kuwasamehe watu wengine.<br />
6. – Omba – kimoyo moyo uongozwe kutoka juu.<br />
7. – Funga – moyo wako na akili zako.<br />
8. – Endelea – kufanya haya kwa miezi michache. Na jizoeshe kufanya<br />
hayo kila siku.<br />
9. – Jiepushe – na sumu ya shetani wakati moyo wako utakapofunguliwa<br />
ili “kuzaliwa upya kwa moyo wako”.<br />
Kumbuka – kujisafisha; kutoa shukrani; kusoma; kutafakari, kisha tafuta,<br />
“na nyinyi hakika mtapata. Omba, na utapewa. Bisha hodi utafunguliwa.”<br />
Kisha endelea na Jiepushe:<br />
Lililobaki ni kati yako na Mungu Muweza wa Ulimwengu. Kama kweli<br />
unampenda Mungu, Yeye tayari anajua hilo na atatushughulikia kila mmoja<br />
wetu kulingana na mioyo yetu.<br />
Majibu ya Maswali:<br />
Kwa sasa kama nilivyowaahidi kuna majibu ya maswali mengi niliyoulizwa<br />
yanayofungamana na chaguo langu la <strong>Uislamu</strong>:<br />
1. Vipi umebadilika kutoka katika mpango mkamilifu wa uwokovu<br />
wa Yesu Kristo msalabani kuokoa dhambi zako?<br />
Jibu: Swali lako linaashiria bado hujazingatia mlingano uliopo kati ya<br />
mafundisho ya Biblia na Quran.<br />
“<strong>Uislamu</strong>” maana yake ni kujisalimisha, kunyenyekea na kumtii Mola wako<br />
kwa uaminifu na amani.” Yeyote anayejaribu kufanya hayo, ni Mwislamu.<br />
“Kama mtu anaamini Mungu Muweza kuwa ni Mungu Mmoja na ni Mola<br />
Mmoja anayetaka kuyafanya maisha yao ili kumtumikia Yeye na kutii amri<br />
zake, mtu huyo atakuwa katika njia sahihi na watu hao watakuwa<br />
“wameokolewa.” Kulingana na Rehema za Mungu. Hakuna wa kuchukua<br />
dhambi za wengine na waovu lazima wasimame na kushitakiwa kwa vile<br />
walilivyovitenda. Itakuwa ni juu ya Mola Muweza kuwasamehe au<br />
kuwaadhibu kwa mujibu wa Hukumu yake katika siku hiyo.