08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

79<br />

alikuwa na elimu nyingi ya Biblia. Mtu huyo anapenda sana hisabati, na hiyo<br />

ndiyo sababu kuwa anapenda mantiki. Siku moja, aliamua kusoma Quran ili<br />

kujaribu kupata Kosa lolote ambalo atafaidika nalo wakati wa kuwaita<br />

Waislamu waingie Ukristo… Alitarajia Quran itakuwa ni kitabu cha zamani<br />

kilichoandikwa karne kumi na nne zilizopita, kitabu kinachozungumzia<br />

jangwa na kadhalika… Alishangazwa na kile alichokikuta. Aligundua kuwa<br />

kitabu hiki kina vitu ambavyo, vitabu vyengine ulimwenguni havina…<br />

Alitarajia atakuta baadhi ya visa juu ya wakati mgumu aliokuwa nao Mtume<br />

Muhammad (S.A.W), kama vile kifo cha mkewe Khadija (Allah amrehemu)<br />

au kifo cha mwanawe na mabinti zake … Hata hivyo, hakukuta chochote<br />

kama hivyo … na kile kilichomfanya achanganyikiwe zaidi ni kuwa alikuta<br />

“sura” kamili katika Quran inaitwa “Mariamu/Maria” ambayo imeshamiri<br />

heshima nyingi kwa Mariamu (amani iwe juu yake) jambo ambalo halipo<br />

katika vitabu vilivyoandikwa na Wakristo na hata Biblia yao haina. Hakukuta<br />

sura yeyote iliyoitwa “Fatuma” (binti ya Mtume) wala “Aisha” (mkewe),<br />

Mungu awarehemu wote wawili. Pia alilikuta jina la Yesu (amani iwe juu<br />

yake) limetajwa ndani ya Quran mara ishirini na tano, wakati jina la<br />

Muhammad (S.A.W), limetajwa mara nne tu, kwa hiyo, akawa<br />

amechanganyikiwa zaidi. Akaanza kuisoma Quran kwa uangalifu zaidi<br />

akitarajia kugundua kosa, lakini alishtushwa pale aliposoma aya kubwa kabisa<br />

ambayo ni aya namba 82 ya surat Al-Nisaa (Wanawake) isemayo:<br />

“Hawaizingatii nini, hii Qurani? Na kama ingelitoka kwa asiyekuwa<br />

Mwenyezi Mungu bila shaka wangalikuta ndani yake khitilafu nyingi.”<br />

Dr. Miller anazungumzia aya hii: “Moja ya misingi ya kisayansi ni msingi wa<br />

kugundua kasoro au kutafuta kasoro katika nadharia hadi itakapothibitishwa<br />

kuwa ni sahihi (jaribio la kugundua uongo wake)… kile kilichomshangaza ni<br />

kuwa Quran Tukufu inawaambia Waislamu na wasiokuwa Waislamu<br />

wajaribu kugundua makosa katika kitabu hiki na kinawaambia watu hao kuwa<br />

hawatagundua kosa lolote.” Pia anasema juu ya aya hii, hakuna mwandishi<br />

yeyote ulimwenguni mwenye ushujaa wa kuandika kitabu na kusema kuwa<br />

kitabu chake hakina makosa, lakini Quran, kinyume kabisa, inakueleza kuwa<br />

haina kosa na inakutaka ujaribu kugundua hata kosa moja na kamwe<br />

hutoligundua.<br />

Aya nyingine ambayo Dr. Miller ameihakisi kwa muda mrefu ni aya namba<br />

30 ya Surat “Al-Anbiya’a” (Mitume): “Je! Hawakuona wale waliokufuru ya<br />

kwamba mbingu na ardhi vilikuwa vimeambatana, kisha Tukaviambua,<br />

(Tukavipambanua). Na Tukafanya kwa maji kila kitu kilicho hai. Basi je,<br />

hawaamini?”

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!