Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
79<br />
alikuwa na elimu nyingi ya Biblia. Mtu huyo anapenda sana hisabati, na hiyo<br />
ndiyo sababu kuwa anapenda mantiki. Siku moja, aliamua kusoma Quran ili<br />
kujaribu kupata Kosa lolote ambalo atafaidika nalo wakati wa kuwaita<br />
Waislamu waingie Ukristo… Alitarajia Quran itakuwa ni kitabu cha zamani<br />
kilichoandikwa karne kumi na nne zilizopita, kitabu kinachozungumzia<br />
jangwa na kadhalika… Alishangazwa na kile alichokikuta. Aligundua kuwa<br />
kitabu hiki kina vitu ambavyo, vitabu vyengine ulimwenguni havina…<br />
Alitarajia atakuta baadhi ya visa juu ya wakati mgumu aliokuwa nao Mtume<br />
Muhammad (S.A.W), kama vile kifo cha mkewe Khadija (Allah amrehemu)<br />
au kifo cha mwanawe na mabinti zake … Hata hivyo, hakukuta chochote<br />
kama hivyo … na kile kilichomfanya achanganyikiwe zaidi ni kuwa alikuta<br />
“sura” kamili katika Quran inaitwa “Mariamu/Maria” ambayo imeshamiri<br />
heshima nyingi kwa Mariamu (amani iwe juu yake) jambo ambalo halipo<br />
katika vitabu vilivyoandikwa na Wakristo na hata Biblia yao haina. Hakukuta<br />
sura yeyote iliyoitwa “Fatuma” (binti ya Mtume) wala “Aisha” (mkewe),<br />
Mungu awarehemu wote wawili. Pia alilikuta jina la Yesu (amani iwe juu<br />
yake) limetajwa ndani ya Quran mara ishirini na tano, wakati jina la<br />
Muhammad (S.A.W), limetajwa mara nne tu, kwa hiyo, akawa<br />
amechanganyikiwa zaidi. Akaanza kuisoma Quran kwa uangalifu zaidi<br />
akitarajia kugundua kosa, lakini alishtushwa pale aliposoma aya kubwa kabisa<br />
ambayo ni aya namba 82 ya surat Al-Nisaa (Wanawake) isemayo:<br />
“Hawaizingatii nini, hii Qurani? Na kama ingelitoka kwa asiyekuwa<br />
Mwenyezi Mungu bila shaka wangalikuta ndani yake khitilafu nyingi.”<br />
Dr. Miller anazungumzia aya hii: “Moja ya misingi ya kisayansi ni msingi wa<br />
kugundua kasoro au kutafuta kasoro katika nadharia hadi itakapothibitishwa<br />
kuwa ni sahihi (jaribio la kugundua uongo wake)… kile kilichomshangaza ni<br />
kuwa Quran Tukufu inawaambia Waislamu na wasiokuwa Waislamu<br />
wajaribu kugundua makosa katika kitabu hiki na kinawaambia watu hao kuwa<br />
hawatagundua kosa lolote.” Pia anasema juu ya aya hii, hakuna mwandishi<br />
yeyote ulimwenguni mwenye ushujaa wa kuandika kitabu na kusema kuwa<br />
kitabu chake hakina makosa, lakini Quran, kinyume kabisa, inakueleza kuwa<br />
haina kosa na inakutaka ujaribu kugundua hata kosa moja na kamwe<br />
hutoligundua.<br />
Aya nyingine ambayo Dr. Miller ameihakisi kwa muda mrefu ni aya namba<br />
30 ya Surat “Al-Anbiya’a” (Mitume): “Je! Hawakuona wale waliokufuru ya<br />
kwamba mbingu na ardhi vilikuwa vimeambatana, kisha Tukaviambua,<br />
(Tukavipambanua). Na Tukafanya kwa maji kila kitu kilicho hai. Basi je,<br />
hawaamini?”