You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
41<br />
mbili za Kingereza zilizotofauti tofauti za maana ya Quran. Kamwe<br />
sikuongea na rafiki zangu wa Kiislamu kuhusu huo uchunguzi wangu binafsi<br />
wa kugundua mwenyewe. Kamwe sikutaja ni aina gani ya vitabu nilivyokuwa<br />
navisoma, wala kuzungumzia kwa nini nilikuwa navisoma vitabu hivyo. Hata<br />
hivyo, mara kwa mara nilikuwa nawapelekea maswali yenye mipaka<br />
maalumu.<br />
Huku nikiwa siwaambii rafiki zungu wa Kiislamu kuhusu vitabu hivyo,<br />
lakini mimi na mke wangu tulikuwa na mijadala mbali mbali juu ya kile<br />
nilichokuwa nakisoma. Kufikia wiki ya mwisho ya Desemba 1992,<br />
nililazimika kukiri, kuwa sijapata upenyo wowote wa kukataa kimsingi kati<br />
ya imani yangu ya kidini na mafundisho ya Kiislamu. Nilipokuwa tayari<br />
kufahamu kuwa Muhammad, amani iwe juu yake, alikuwa ni Mtume<br />
(mmojawapo aliyeongea kwa, au chini ya msukumo) wa Mungu, na<br />
nilipokuwa sina uzito wowote wa kuthibisha kuwa hakuna Mungu kinyume<br />
na Allah, Mtukufu aliyetukuka, nilikuwa bado ninasitasita kuchukua uamuzi<br />
wowote. Tayari nilikuwa nimekiri katika nafsi yangu kuwa nilikuwa pamoja<br />
sana na imani ya Kiislamu kama baadaye nilivyoifahamu, kuliko nilivyofanya<br />
na mila ya Kikristo ya kuweka umoja wa kanisa. Nilijua vizuri sana kuwa<br />
kiwepesi kabisa ningeweza kuthibitisha kutokana na mafunzo na elimu yangu<br />
ya seminari, mambo mengi ambayo Quran ililazimika kuusema Ukristo,<br />
Biblia, na Yesu, amani iwe juu yake. Hata hivyo, nilisita. Zaidi, nilitazama<br />
kimantiki usitaji wangu kwa kujiendesha mimi mwenyewe kuwa kweli sikijui<br />
kiini na suala la msingi na maelezo kamili juu ya <strong>Uislamu</strong>, na kwa hiyo,<br />
maeneo yangu ya kuafiki yaliwekewa mipaka kwa dhana nzima. Kwa hiyo,<br />
niliendelea kusoma, na kurudia kusoma.<br />
Wazo moja la kujitambulisha, mimi ni nani, ni uthibitisho wenye nguvu zaidi<br />
juu ya nafasi ya mtu binafsi ulimwenguni. Katika kazi zangu nizifanyazo,<br />
mara kwa mara niliitwa kutibia tabia mbaya, zinazojipanga kuanzia, kuvuta<br />
sigara, hadi ulevi, utumiaji wa madawa ya kulevya. Nikiwa ni tabibu, nilijua<br />
kuwa msingi wa tabia mbaya za kiwili wili lazima utibiwe ili kuunda kinga ya<br />
awali. Na hilo lilikuwa ni sehemu rahisi sana ya matibabu. Mark Twain<br />
alisema: “Kuacha sigara ni kwepesi; nimeshaacha mara mia kadhaa.” Hata<br />
hivyo, pia nilijua kuwa funguo ya kudumisha uzuiaji wa wigo wa muda<br />
ilikuwa ni kumtibu mgonjwa tabia mbaya za kisaikolojia, ambazo kwa kiasi<br />
kikubwa zilizunguka mzizi wa fikra za mgonjwa za kujitambulisha, yaani,<br />
mgonjwa anajitambulisha kuwa yeye alikuwa ni “mvuta sigara,” au “mlevi”<br />
na kuendelea. Tabia mbaya imeshakuwa ni sehemu na ni mfuko wa fikra hii