08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

41<br />

mbili za Kingereza zilizotofauti tofauti za maana ya Quran. Kamwe<br />

sikuongea na rafiki zangu wa Kiislamu kuhusu huo uchunguzi wangu binafsi<br />

wa kugundua mwenyewe. Kamwe sikutaja ni aina gani ya vitabu nilivyokuwa<br />

navisoma, wala kuzungumzia kwa nini nilikuwa navisoma vitabu hivyo. Hata<br />

hivyo, mara kwa mara nilikuwa nawapelekea maswali yenye mipaka<br />

maalumu.<br />

Huku nikiwa siwaambii rafiki zungu wa Kiislamu kuhusu vitabu hivyo,<br />

lakini mimi na mke wangu tulikuwa na mijadala mbali mbali juu ya kile<br />

nilichokuwa nakisoma. Kufikia wiki ya mwisho ya Desemba 1992,<br />

nililazimika kukiri, kuwa sijapata upenyo wowote wa kukataa kimsingi kati<br />

ya imani yangu ya kidini na mafundisho ya Kiislamu. Nilipokuwa tayari<br />

kufahamu kuwa Muhammad, amani iwe juu yake, alikuwa ni Mtume<br />

(mmojawapo aliyeongea kwa, au chini ya msukumo) wa Mungu, na<br />

nilipokuwa sina uzito wowote wa kuthibisha kuwa hakuna Mungu kinyume<br />

na Allah, Mtukufu aliyetukuka, nilikuwa bado ninasitasita kuchukua uamuzi<br />

wowote. Tayari nilikuwa nimekiri katika nafsi yangu kuwa nilikuwa pamoja<br />

sana na imani ya Kiislamu kama baadaye nilivyoifahamu, kuliko nilivyofanya<br />

na mila ya Kikristo ya kuweka umoja wa kanisa. Nilijua vizuri sana kuwa<br />

kiwepesi kabisa ningeweza kuthibitisha kutokana na mafunzo na elimu yangu<br />

ya seminari, mambo mengi ambayo Quran ililazimika kuusema Ukristo,<br />

Biblia, na Yesu, amani iwe juu yake. Hata hivyo, nilisita. Zaidi, nilitazama<br />

kimantiki usitaji wangu kwa kujiendesha mimi mwenyewe kuwa kweli sikijui<br />

kiini na suala la msingi na maelezo kamili juu ya <strong>Uislamu</strong>, na kwa hiyo,<br />

maeneo yangu ya kuafiki yaliwekewa mipaka kwa dhana nzima. Kwa hiyo,<br />

niliendelea kusoma, na kurudia kusoma.<br />

Wazo moja la kujitambulisha, mimi ni nani, ni uthibitisho wenye nguvu zaidi<br />

juu ya nafasi ya mtu binafsi ulimwenguni. Katika kazi zangu nizifanyazo,<br />

mara kwa mara niliitwa kutibia tabia mbaya, zinazojipanga kuanzia, kuvuta<br />

sigara, hadi ulevi, utumiaji wa madawa ya kulevya. Nikiwa ni tabibu, nilijua<br />

kuwa msingi wa tabia mbaya za kiwili wili lazima utibiwe ili kuunda kinga ya<br />

awali. Na hilo lilikuwa ni sehemu rahisi sana ya matibabu. Mark Twain<br />

alisema: “Kuacha sigara ni kwepesi; nimeshaacha mara mia kadhaa.” Hata<br />

hivyo, pia nilijua kuwa funguo ya kudumisha uzuiaji wa wigo wa muda<br />

ilikuwa ni kumtibu mgonjwa tabia mbaya za kisaikolojia, ambazo kwa kiasi<br />

kikubwa zilizunguka mzizi wa fikra za mgonjwa za kujitambulisha, yaani,<br />

mgonjwa anajitambulisha kuwa yeye alikuwa ni “mvuta sigara,” au “mlevi”<br />

na kuendelea. Tabia mbaya imeshakuwa ni sehemu na ni mfuko wa fikra hii

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!