You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
72<br />
kuficha bunduki aina ya AK – 47. Kwa hiyo, nilienda duka la vitabu vya<br />
Kiarabu.<br />
Wakaniuliza, “Tukusaidie nini?”<br />
“Nataka Quran.”<br />
“Sawa, hapa tunazo nakala za Quran.”<br />
Walikuwa na nakala nzuri sana – kwa dola therathini, dola arobaini.”<br />
“Tazama, nataka kusoma tu, sitaki kuwa mmoja wao, sawa?”<br />
“Sawa, tuna huo hapo mdogo dogo kwa dola tano wenye jarada la karatasi.”<br />
Nilirudi nyumbani, na kuanza kusoma Quran yangu kuanzia mwanzo, wa<br />
Suratul Fatihah. Na sikuweza kuyatoa macho yangu kutoka katika Quran.<br />
Oyaa, tazama hii. Inazungumzia juu ya Nuhu humu. Tunaye Nuhu katika<br />
Biblia yetu pia. Oyaa, Inazungumzia Lutwi na Ibrahimu. Siamini. Kamwe<br />
sijalijua jina la shetani kuwa ni Ibilisi. Oyaa, vipi kuhusu hayo?<br />
Unapopata picha hiyo katika T.V yako na ikiwa na maelezo kidogo nawe<br />
unabonyeza swichi ya kusafisha picha. Hilo ni jambo la hakika linalotoke na<br />
Quran.<br />
Nilipitia kila kitu. Kwa hiyo, nilisema: sawa; nimeshafanya haya, sasa kitu<br />
gani utakachofanya baadaye? Vizuri, uende katika eneo lao la kukutania.<br />
Nilitazama kitabu cha kurasa za manjano (kitabu cha kuelezea mambo mbali<br />
mbali yanapopatikana) na mwishowe nilikipata kituo cha Kiislamu cha<br />
Calfornia kusini, katika Vermont. Niliwapigia simu nao wakasema, “Njoo<br />
Ijumaa.”<br />
Sasa tayari nilianza kuchanganyikiwa, kwa sababu, sasa ninajua nitaanza<br />
kukabiliwa na Habibu na bunduki yake ya AK-47.<br />
Nataka watu wafahamu, Wakristo wa Marekani wapoje katika ujio wa<br />
<strong>Uislamu</strong>. Nafanya mambo ya kitoto kuhusiana na AK- 47, lakini sijui kama<br />
watu hao wana masime chini ya makoti yao, unajua? Kwa hiyo, nilienda hadi<br />
mbele, na nina hakika vya kutosha, kuwa kulikuwa na huyu ndugu mwenye<br />
(six-foot-three, 240-paundi) ndevu na kila kitu, na nilikuwa ni mwenye<br />
heshima.<br />
Nilitembea na kusema: “Samahani bwana.”<br />
[Lahaja ya Kiarabu] “Rudi nyuma!”