08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

88<br />

11- MUHAMMAD AMAN HOBHM MWANADIPLOMASIA,<br />

MMISHIONARI NA MFANYAKAZI WA KAZI ZA JAMII<br />

(UJERUMANI).<br />

Kwa nini watu wa magharibi wanaingia <strong>Uislamu</strong>?<br />

Kuna sababu nyingi juu ya hilo. Inayoshika nafasi ya kwanza, ni kuwa ukweli<br />

daima una nguvu zake. Msingi wa imani ya Kiislamu ni ya uwiano sana, ni ya<br />

kimaumbile sana na ni ya kuvutia sana kiasi ambacho mtafuta ukweli aliye<br />

mwema hawezi kutovutiwa na hayo. Tuchukulie kwa mfano; imani ya kuwa<br />

kuna Mungu mmoja. Namna inavyoinua heshima ya mtu na namna<br />

inavyotuweka huru na ung`ang`aniaji wa mambo ya kichawi na ya hovyo<br />

hovyo! Namna inavyoongoza kimaumbile kueleke katika usawa wa<br />

kibinadamu, kwa kuwa binadamu wote wameumbwa na Mungu Mmoja na<br />

wote ni watumishi wa Mola huyo huyo! Kwa Wajerumani, kwa sifa ya<br />

kipekee, imani ya kumwamini Mungu ni chanzo cha ufunuo, chanzo cha<br />

ushujaa wa kutokuwa na woga na ni chanzo cha kuhisi usalama. Kisha dhana<br />

ya maisha baada ya kifo inapindua meza. Maisha katika dunia hii yanabakia<br />

kuwa si lengo kuu tena, na sehemu kubwa ya nguvu ya mwanadamu<br />

itolewayo kwa ubora wa ahera. Imani ya kuamini siku ya Kiama yenyewe<br />

inampa mtu heshima ya kuacha matendo mabaya, na kufanya matendo mazuri<br />

pekee ambayo yanaweza kuhakikisha uwokovu wa milele, ingawa matendo<br />

mabaya yanaweza kustawi hapa duniani kwa kipindi chenye mipaka maalumu<br />

tu. Imani ya kuamini kuwa hakuna mtu awezaye kukimbia matokeo ya<br />

hukumu ya haki, na Mungu Mjuzi afanyaye mambo mawili kabla ya mtu<br />

kufanya chochote kile kilichokibaya na kwa hakika huu ukaguzi wa milele ni<br />

wenye kutenda kazi zaidi kuliko polisi wenye kufaa sana duniani.<br />

Kitu kingine ambacho kinawavutia wageni wengi kuingia <strong>Uislamu</strong> ni<br />

msisitizo wake juu ya kuvumiliana. Kisha sala za kila siku zinamfundisha mtu<br />

awe anapanga wakati na mwezi mmoja wa kufunga unamuwezesha mtu<br />

kufanya mazoezi ya kujimiliki juu ya nafsi yake na bila ya shaka kupanga<br />

wakati na kuwa na nidhamu binafsi ni vitu viwili vya fikra muhimu sana ya<br />

mtu mwema na mtu mbora.<br />

Sawa, yanakuja mafanikio halisi ya <strong>Uislamu</strong>. <strong>Uislamu</strong> ni itikadi pekee<br />

ambayo imefanikiwa kuingiza, kidogo kidogo, kwa wafuasi wake roho ya<br />

kuona mfumo wa maadili na mipaka ya utu bila kulazimishwa na vitu vya nje.<br />

Kwani Mwislamu anajua kwamba, popote alipo, anatazamwa na Mungu.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!