You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
88<br />
11- MUHAMMAD AMAN HOBHM MWANADIPLOMASIA,<br />
MMISHIONARI NA MFANYAKAZI WA KAZI ZA JAMII<br />
(UJERUMANI).<br />
Kwa nini watu wa magharibi wanaingia <strong>Uislamu</strong>?<br />
Kuna sababu nyingi juu ya hilo. Inayoshika nafasi ya kwanza, ni kuwa ukweli<br />
daima una nguvu zake. Msingi wa imani ya Kiislamu ni ya uwiano sana, ni ya<br />
kimaumbile sana na ni ya kuvutia sana kiasi ambacho mtafuta ukweli aliye<br />
mwema hawezi kutovutiwa na hayo. Tuchukulie kwa mfano; imani ya kuwa<br />
kuna Mungu mmoja. Namna inavyoinua heshima ya mtu na namna<br />
inavyotuweka huru na ung`ang`aniaji wa mambo ya kichawi na ya hovyo<br />
hovyo! Namna inavyoongoza kimaumbile kueleke katika usawa wa<br />
kibinadamu, kwa kuwa binadamu wote wameumbwa na Mungu Mmoja na<br />
wote ni watumishi wa Mola huyo huyo! Kwa Wajerumani, kwa sifa ya<br />
kipekee, imani ya kumwamini Mungu ni chanzo cha ufunuo, chanzo cha<br />
ushujaa wa kutokuwa na woga na ni chanzo cha kuhisi usalama. Kisha dhana<br />
ya maisha baada ya kifo inapindua meza. Maisha katika dunia hii yanabakia<br />
kuwa si lengo kuu tena, na sehemu kubwa ya nguvu ya mwanadamu<br />
itolewayo kwa ubora wa ahera. Imani ya kuamini siku ya Kiama yenyewe<br />
inampa mtu heshima ya kuacha matendo mabaya, na kufanya matendo mazuri<br />
pekee ambayo yanaweza kuhakikisha uwokovu wa milele, ingawa matendo<br />
mabaya yanaweza kustawi hapa duniani kwa kipindi chenye mipaka maalumu<br />
tu. Imani ya kuamini kuwa hakuna mtu awezaye kukimbia matokeo ya<br />
hukumu ya haki, na Mungu Mjuzi afanyaye mambo mawili kabla ya mtu<br />
kufanya chochote kile kilichokibaya na kwa hakika huu ukaguzi wa milele ni<br />
wenye kutenda kazi zaidi kuliko polisi wenye kufaa sana duniani.<br />
Kitu kingine ambacho kinawavutia wageni wengi kuingia <strong>Uislamu</strong> ni<br />
msisitizo wake juu ya kuvumiliana. Kisha sala za kila siku zinamfundisha mtu<br />
awe anapanga wakati na mwezi mmoja wa kufunga unamuwezesha mtu<br />
kufanya mazoezi ya kujimiliki juu ya nafsi yake na bila ya shaka kupanga<br />
wakati na kuwa na nidhamu binafsi ni vitu viwili vya fikra muhimu sana ya<br />
mtu mwema na mtu mbora.<br />
Sawa, yanakuja mafanikio halisi ya <strong>Uislamu</strong>. <strong>Uislamu</strong> ni itikadi pekee<br />
ambayo imefanikiwa kuingiza, kidogo kidogo, kwa wafuasi wake roho ya<br />
kuona mfumo wa maadili na mipaka ya utu bila kulazimishwa na vitu vya nje.<br />
Kwani Mwislamu anajua kwamba, popote alipo, anatazamwa na Mungu.