08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

8<br />

Siku moja katika majira ya michipuo mwaka 1991, nilijua kuwa Waislamu<br />

wanaamini Biblia. Nilishtushwa. Hilo litakuwaje? Lakini hilo si la mwisho,<br />

wanaamini Yesu kuwa ni:<br />

• Mtume wa kweli wa Mungu.<br />

• Nabii wa Mungu.<br />

• Kazaliwa kimiujiza bila ya tendo la ndoa la wanadamu.<br />

• Alikuwa ni “Kristo” au Messiah kama alivyobashiriwa na Biblia;<br />

• Kwa sasa yupo pamoja na Mungu na la muhimu sana ni:<br />

• Atarejea tena siku za mwishoni kuwaongoza waumini dhidi ya<br />

mpinga Kristo.<br />

Baada ya “kushinda roho na kuipeleka kwa Bwana, kwa Yesu” siku baada<br />

ya siku, jambo hilo litakuwa ndiyo mafanikio yangu makubwa, kumnasa<br />

mmoja wa “Waislamu” hawa na ‘kumbadili’ awe Mkristo.”<br />

Nilimuuliza kama anataka chai na akanijibu ndiyo. Kwa mbali, tulikiendea<br />

kibanda kidogo kilichopo katika jengo kubwa la biashara, kukaa na<br />

kuzungumzia mada yangu niipendayo ya Imani. Tulipokuwa tumekaa katika<br />

kiduka hicho cha chai kwa masaa huku tukizungumza (nilikuwa ndiye<br />

muongeaji sana) nikagundua kuwa alikuwa ni mtu mzuri sana, mtulivu na ni<br />

mwenye kuona haya kidogo. Alinisikiliza kwa umakini kila neno<br />

nililolazimika kulisema na hakunikatiza hata mara moja. Niliipenda njia ya<br />

mtu huyo na nilifikiria kuwa mtu huyo ana uwezekano wa wazi wa kuwa<br />

Mkristo mzuri. – Ni kidogo nilichokijua juu ya mtiririko wa matukio<br />

yanayojifungua mbele ya macho yangu.<br />

Kwanza kabisa, niliafikiana na baba yangu kuwa tufanye biashara na mtu<br />

huyo na hata kupigia debe wazo la kusafiri naye katika misafara yangu ya<br />

kibiashara kuvuka eneo la Kaskazini mwa Texas. Siku baada siku tutaendesha<br />

na kujadili mambo mbali mbali yanayofungamana na imani za watu mbalil<br />

mbali. Tukiwa njiani, kwa hakika nilikuwa nahanikiza baadhi ya vipindi vya<br />

redio vya mambo ya kiibada nilivyokuwa navipenda sana na kuvitukuza ili<br />

vinisaidie kufikisha ujumbe kwa huyo masikini aliyepeke yake.<br />

Tulizungumza juu ya maana ya Mungu; maisha; lengo la kuumbwa; Mitume<br />

na kazi zao; na jinsi Mungu anvyofunua ufunuo wake kwa binadamu. Pia<br />

tulishiriki kujadili uzoefu na fikra za kila mtu binafsi.<br />

Siku moja nilijua kuwa rafiki yangu, Mohammed alikuwa anataka kuhama<br />

kutoka katika nyumba aliyokuwa akiishi na rafiki yake na alikuwa anataka

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!