You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
29<br />
Mwanzo Mpya<br />
Haikuchukua muda mrefu baada ya kuwasili Saudi Arabia nikaona<br />
mabadiliko ya haraka katika mfumo wa maisha ya Waislamu. Walikuwa<br />
wanatofautiana na wafuasi wa Elijah Muhammad na mchungaji Louios<br />
Farrakhan kwa upande wa kuwa wote walikuwa ni wazalendo, rangi moja na<br />
lugha moja. Nami, kwa haraka haraka nilieleza shauku yangu ya kusoma zaidi<br />
kuhusu dini hii ya kipekee yenye kushangaza. Nilishangazwa na maisha ya<br />
Mtume Muhammad na nilitaka kuyafahamu zaidi. Niliazima vitabu kutoka<br />
kwa mmoja wa jamaa aliyekuwa mchangamfu katika kuwalingania watu<br />
waingie <strong>Uislamu</strong>. Nilipewa vitabu vyote nilivyokuwa navitaka. Nilikisoma<br />
kila kitabu. Kisha nikapewa Quran Tukufu na nikaisoma yote yote kwa mara<br />
kadhaa katika kipindi cha miezi minne. Kilichonivutia zaidi ni kuwa, wale<br />
jamaa hawakuwa ni wenye kunigandamiza kwa elimu zao. Kama ndugu<br />
yeyote hakujua jibu la swali aliloulizwa, aliniambia kwa wepesi kabisa, kuwa<br />
hawezi kulijibu na ataliangalia kwa mtu anayeliweza. Na siku inayofuata<br />
daima ataniletea jibu. Nikaona jinsi ya unyenyekevu ulivyofanya kazi kubwa<br />
katika maisha ya watu hao wa ajabu wa mashariki ya kati.<br />
Nilishangazwa kuwaona wanawake wakijifunika kuanzia nyuso zao hadi<br />
miguuni. Sijaona dini yeyote ya makasisi ikiwa hivyo. Hakuna mtu<br />
aliyeshindana kwa ajili ya kupata cheo cha kidini. Yote hayo yalikuwa ni<br />
mazuri ajabu, lakini vipi nitaziendesha fikra za kuacha mafundisho ambayo<br />
nimeshayafuata tangu nikiwa mdogo? Je, kuna nini kuhusiana na Biblia?<br />
Nilijuwa kuwa kuna baadhi ya ukweli ndani yake hata hivyo,<br />
imeshabadilishwa na kurejewa kwa mara nyingi. Kisha nilipewa mkanda wa<br />
video wa mahojiano kati ya sheikh Ahmadi Deedat na Reverend Jimmy<br />
Swaggart. Baada ya kutazama mjadala huo kwa haraka haraka nikawa<br />
Mwislamu.<br />
Unaweza kusikiliza majadiliano hayo katika website<br />
sitehtt:// www.islam.org/audiyo/ra622_4.ram