You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
67<br />
Naogopa sana kifo! Kwa hiyo, mama yangu alinigeukia: “Tazama<br />
kitakachotokea kama hutobatizwa, na hutofanya matakwa ya Mungu? Dunia<br />
itatumeza, au moja ya mawe hayo makubwa mno litakupiga juu ya kichwa na<br />
litakuangusha, na hautoishi tena. Nami nitalazimika kutengeneza mtoto<br />
mwingine.”<br />
Sikutaka kuchukua nafasi ya kugongwa na moja ya mawe hayo ya mvua<br />
yaliyo makubwa. Kwa hiyo, nikabatizwa. Bila shaka mashahidi wa Yehova<br />
hawaamini kunyunyiza maji. Wao wanakuzamisha kabisa kabisa,<br />
wanakuacha ndani ya maji hayo kwa sekunde moja, kisha wanakutoa.<br />
Nilifanya hivyo nikiwa na miaka 13, Septemba 7, 1963 mjini Pasadena,<br />
Calfornia, katika birika la Rose Bowl. Ilikuwa ni mkutano wa kimataifa<br />
mkubwa sana. Tulikuwa watu 100,000 laki moja. tuliendesha magari kutokea<br />
Lubbock, Texas.<br />
Hatimaye nilianza kutoa maneno makubwa – dakika kumi mbele ya mkutano.<br />
Na kundi la wahudumu wa sinema walinipendekeza nitoe muhadhara wa saa<br />
moja ambao ulifanyika Jumapili walialikwa watu wengi. Wao kikawaida<br />
huwa wanayahifadhi mahubiri hayo kwa ajili ya wazee wa makutano.<br />
[Kwa sauti ya mamlaka:] “Kwa hakika ni ndogo, Lakini anaweza kukamata<br />
jambo hilo. Yeye ni kijana wa Kikristo mzuri. Hana maovu, na ni mtiifu kwa<br />
wazazi wake na anaonekana ana elimu bora na kubwa sana ya Biblia.”<br />
Kwa hiyo, nikiwa na miaka kumi na sita nilianza kutoa muhadhara wa saa<br />
moja mbele ya makutano yote. Kwanza kabisa niliandikwa katika kikundi<br />
kilichopo Sweetwater, Texas, na Kaosha, hatimaye, mjini Brownfield, Texas,<br />
nilipopata makutano yangu ya kwanza. Katika umri wa miaka ishirini,<br />
nilikuwa ni kile wakiitacho mchungaji chipukizi (mtangulizi).<br />
Mashahidi wa Yehova wana mpango wa mafunzo wa kisasa sana, wana aina<br />
mfumo wa haki. Unalazimika kutenga masaa kumi hadi kumi na mbili kwa<br />
mwezi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Ni kama muuza biashara. IBM<br />
haifai chochote kwa vijana hao.<br />
Kwa hiyo, nilipokuwa mchungaji mtangazaji, nilitenga muda wangu mwingi<br />
kufanya utumishi wa nyumba kwa nyumba. Nilikuwa nalazimika kufanya<br />
hivyo kiasi cha masaa mia moja kwa mwezi, na nililazimika kuwa na masomo