You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
30<br />
Unaweza kuvishusha vitabu vya<br />
Shaykh Ahmadi Deedat<br />
Kupitia website hizi:<br />
www.ahmed-deedat.co.za<br />
au www.aljame3.com<br />
Nami kirasmi nilitangaza kuukubali <strong>Uislamu</strong>. Na ilikuwa hapo ndipo<br />
nilipopewa ushauri wa mdomo juu ya namna ya kujiandaa kwa safari ndefu<br />
huko mbele. Ilikuwa ni mazazi ya kweli kutoka kizani na kuingia katika nuru.<br />
Nilistaajabu, kivipi, wenzangu wa kutoka kanisani wangenifikiria<br />
watakaposikia kuwa nimeingia <strong>Uislamu</strong>. Haikuchukuwa muda mrefu kabla<br />
sijagundua. Nilirudi USA kwa ajili ya likizo na nilikosolewa vikali mno kwa<br />
“ukosefu wangu wa imani.” Nilibandikwa majina mengi – kuanzia muhaini<br />
hadi mpotovu. Watu waliambiwa na viongozi wa kanisa hata wasinikumbuke<br />
wakati wa sala. Hiyo ilikuwa ni kama ugeni, inavyoonekana kwani mwishoni<br />
sikuudhika. Nilikuwa na furaha sana kwa kuwa Mungu Muweza, Allah,<br />
amenichagua na kuniongoza katika haki ambayo hakuna kitu kingine cha<br />
kukijali.<br />
Kitu pekee, ninachohitaji kwa sasa ni kuwa Mwislamu niliyejitolea kwa dhati<br />
kama nilivyokuwa Mkristo. Hili, bila ya shaka, linamaanisha kusoma.<br />
Nilitambua kuwa mtu anaweza kukua kielimu kama atakavyo ndani ya<br />
<strong>Uislamu</strong>. Hakuna ukiritimba wa elimu – na elimu ni bure kwa kila atakaye<br />
kujinufaisha kwa nafasi ya kusoma. Nilipewa seti ya Saheeh Muslim kama<br />
zawadi kutoka kwa mwalimu wangu wa Quran. Na ilikuwa ni hapo ndipo<br />
nilipogundua kuwa kuna haja ya kujifunza kuhusu maisha, maneno na<br />
matendo ya Mtume Muhammad. Nilisoma na kijifunza hadithi nyingi<br />
zilizokuwepo katika Kingereza kwa kadiri ilivyowezekana. Nilitambua kuwa<br />
elimu yangu ya Biblia ilikuwa ni rasilimali ambayo inafaa zaidi kwa sasa<br />
katika kushughulika na wale wenye historia ya kuwa Wakristo. Kwangu<br />
maisha yalikuwa na maana mpya kabisa. Moja ya mabadiliko ya kimtazamo<br />
ya maana sana ni matokeo ya kujua kuwa maisha haya kwa hakika yatumiwe<br />
kwa kujiandaa na Ahera. Pia, ilikuwa ni uzoefu mpya kujua kuwa tunalipwa<br />
hata kwa nia zetu. Kama umenuia kutenda jema, utalipwa. Hiyo ilikuwa ni<br />
tofauti kabisa na kanisani. Mtazamo ulikuwa ni “njia ya Motoni imepambiwa<br />
nia nzuri nzuri.” Kulikuwa hakuna njia ya kushinda. Kama umefanya dhambi,<br />
ulitakiwa uungame kwa mchungaji, na hasa hasa kama dhambi yenyewe ni<br />
kubwa, kama vile uzinzi. Ulihukumiwa moja kwa moja kwa matendo yako.