08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

30<br />

Unaweza kuvishusha vitabu vya<br />

Shaykh Ahmadi Deedat<br />

Kupitia website hizi:<br />

www.ahmed-deedat.co.za<br />

au www.aljame3.com<br />

Nami kirasmi nilitangaza kuukubali <strong>Uislamu</strong>. Na ilikuwa hapo ndipo<br />

nilipopewa ushauri wa mdomo juu ya namna ya kujiandaa kwa safari ndefu<br />

huko mbele. Ilikuwa ni mazazi ya kweli kutoka kizani na kuingia katika nuru.<br />

Nilistaajabu, kivipi, wenzangu wa kutoka kanisani wangenifikiria<br />

watakaposikia kuwa nimeingia <strong>Uislamu</strong>. Haikuchukuwa muda mrefu kabla<br />

sijagundua. Nilirudi USA kwa ajili ya likizo na nilikosolewa vikali mno kwa<br />

“ukosefu wangu wa imani.” Nilibandikwa majina mengi – kuanzia muhaini<br />

hadi mpotovu. Watu waliambiwa na viongozi wa kanisa hata wasinikumbuke<br />

wakati wa sala. Hiyo ilikuwa ni kama ugeni, inavyoonekana kwani mwishoni<br />

sikuudhika. Nilikuwa na furaha sana kwa kuwa Mungu Muweza, Allah,<br />

amenichagua na kuniongoza katika haki ambayo hakuna kitu kingine cha<br />

kukijali.<br />

Kitu pekee, ninachohitaji kwa sasa ni kuwa Mwislamu niliyejitolea kwa dhati<br />

kama nilivyokuwa Mkristo. Hili, bila ya shaka, linamaanisha kusoma.<br />

Nilitambua kuwa mtu anaweza kukua kielimu kama atakavyo ndani ya<br />

<strong>Uislamu</strong>. Hakuna ukiritimba wa elimu – na elimu ni bure kwa kila atakaye<br />

kujinufaisha kwa nafasi ya kusoma. Nilipewa seti ya Saheeh Muslim kama<br />

zawadi kutoka kwa mwalimu wangu wa Quran. Na ilikuwa ni hapo ndipo<br />

nilipogundua kuwa kuna haja ya kujifunza kuhusu maisha, maneno na<br />

matendo ya Mtume Muhammad. Nilisoma na kijifunza hadithi nyingi<br />

zilizokuwepo katika Kingereza kwa kadiri ilivyowezekana. Nilitambua kuwa<br />

elimu yangu ya Biblia ilikuwa ni rasilimali ambayo inafaa zaidi kwa sasa<br />

katika kushughulika na wale wenye historia ya kuwa Wakristo. Kwangu<br />

maisha yalikuwa na maana mpya kabisa. Moja ya mabadiliko ya kimtazamo<br />

ya maana sana ni matokeo ya kujua kuwa maisha haya kwa hakika yatumiwe<br />

kwa kujiandaa na Ahera. Pia, ilikuwa ni uzoefu mpya kujua kuwa tunalipwa<br />

hata kwa nia zetu. Kama umenuia kutenda jema, utalipwa. Hiyo ilikuwa ni<br />

tofauti kabisa na kanisani. Mtazamo ulikuwa ni “njia ya Motoni imepambiwa<br />

nia nzuri nzuri.” Kulikuwa hakuna njia ya kushinda. Kama umefanya dhambi,<br />

ulitakiwa uungame kwa mchungaji, na hasa hasa kama dhambi yenyewe ni<br />

kubwa, kama vile uzinzi. Ulihukumiwa moja kwa moja kwa matendo yako.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!