Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
9<br />
kukaa msikitini kwa muda fulani. Nilienda kwa baba na kumuomba<br />
tumwalike Mohammed aje kuishi nasi katika nyumba yetu kubwa iliyopo<br />
kijijini. Baada ya yote, anaweza kushirikiana nasi kazi na kulipia baadhi ya<br />
gharama na atakuwepo wakati tutakapokuwa tunaenda safari zetu. Baba<br />
alikubali na Mohammed akahamia.<br />
Bila ya shaka nilikuwa bado ninapata nafasi ya kuwatembelea rafiki zangu<br />
wahubiri na wachungaji waishio Texas. Mmoja wao alikuwa anaishi Texas<br />
karibu na mpaka wa Mexico na mwingine aliishi karibu na mpaka wa<br />
Oklahoma. Muhubiri mmoja alipendelea salaba la mbao kubwa sana ambalo<br />
lilikuwa kubwa kuliko gari ndogo. Alikuwa anaubeba juu ya mabega yake na<br />
kuuburuza. Kitako chake ardhini na kupita nao mtaani au barabarani huku<br />
akihanikiza miale miwili iliyoundwa kwa umbo la msalaba. Watu<br />
walisimamisha magari yao na kumwendea na kumuuliza kulikoni; naye<br />
angewapa vijitabu na vijikaratasi juu ya Ukristo.<br />
Siku moja rafiki yangu mwenye msalaba alipatwa na mshtuko wa moyo na<br />
kulazimika aende hospitali ya Veterans ambako alikaa kwa muda mrefu.<br />
Nilikuwa namtembelea hapo hospitalini kwa mara kadhaa kwa wiki na<br />
nilikuwa namchukuwa Mohammed pamoja nami, nikiwa na matarajio ya<br />
kuwa sote tutashiriki mada ya imani na dini. Rafiki yangu mwenye msalaba<br />
hakupandishwa mori, na ilikuwa ni wazi kuwa hakutaka kujua chochote<br />
kuhusu <strong>Uislamu</strong>. Kisha siku moja yule mtu ambaye alikuwa anashirikiana na<br />
rafiki yangu alikuja huku akiendesha kiti chake cha magurudumu na kuingia<br />
chumbani. Nilimwendea na kumuuliza jina lake na akasema kuwa hilo si<br />
muhimu na nilipomuuliza ametokea wapi alisema kuwa ametokea sayari ya<br />
Jupita. Nilifikiria kile alichokisema na kisha nilianza kustaajabu je, kama<br />
ningekuwa katika wodi ya mshtuko wa moyo au katika wodi ya wagonjwa wa<br />
akili ingekuwaje.<br />
Nilijua kuwa yule mtu alikuwa ni mpweke na amefadhaika na anahitaji mtu<br />
katika maisha yake. Kwa hiyo, nilianza kumthibitishia kuhusu Bwana.<br />
Nilimsomea kwa sauti kitabu cha Jonah katika Agano la Kale. Na fikra<br />
ilikuwa ni kuwa kwa hakika hatuwezi kukimbia matatizo yetu kwa kuwa siku<br />
zote tunajua tulichokifanya na cha ziada, Mungu pia daima anajua ambacho<br />
tumekifanya.<br />
Padri wa Kikatoliki