Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
82<br />
Dr. Miller anaendelea: Je, waweza kuona namna aya ambazo zinazungumzia<br />
juu ya uadui kati ya Waislamu na Wayahudi zinaanzisha changamoto kwa<br />
akili ya mwanadamu? “Hakika utawakuta walio maadui zaidi kuliko watu<br />
(wengine) kwa Waislamu ni Mayahudi na wale mushirikina (wasiokuwa na<br />
Kitabu), na utawaona walio karibu kwa urafiki na Waislamu ni wale<br />
wanaosema: “Sisi ni Wakristo.” (Hayo) ni kwa sababu wako miongoni mwao<br />
wanavyuoni na wamchao Mungu, na kwa sababu wao (Wakristo)<br />
hawatakabari; (wakijua haki huifuata). Na wanaposikia yaliyoteremshwa<br />
kwa Mtume (na yakawatulilikia kuwa ni kweli), utaona macho yao<br />
yanamiminika machozi kwa sababu ya haki waliyoitambua; wanasema:<br />
“Mola wetu! Tumeamini, basi tuandike pamoja na wanaoshuhudia (ukweli<br />
huu).” (Na wakilaumiwa kwa kusilimu kwao husema): “Na kwa nini<br />
tusimwamini Mwenyezi Mungu na haki iliyotufikia, na hali tunatumai Mola<br />
wetu atuingize (Peponi) pamoja na watu wema?” (Qurani 5:82-84).<br />
Aya hizi zilitumiwa na: Dr. Miller pia alipokuwa Mkristo lakini alipoujua<br />
ukweli, aliamini na kuingia <strong>Uislamu</strong> na akawa ni muhubiri wa Kiislamu.<br />
Mungu alitie nguvu.<br />
Dr. Miller anasema juu ya mtindo wa kipekee wa Quran kuwa yeye anauona<br />
ni wa kupendeza sana: hakuna shaka kuwa kuna kitu cha pekee na cha<br />
kushangaza katika Qurani ambacho hakijatajwa sehemu yeyote ile, kwani<br />
Quran inakupa maelezo maalumu na inakuambia kuwa ulikuwa huyajui hapo<br />
kabla. Kwa mfano: Hizi ni habari za ghaibu Tunazokufunulia; nawe hukuwa<br />
nao walipokuwa wakitupa kalamu zao ndani ya maji (kwa kura, wajue) nani<br />
wao atamlea Maryamu, na hakuwa nao walipokuwa wakishindana. (Quran<br />
3:44)<br />
Hizi ni katika khabari za siri Tunazokufunulia. Hukuwa ukizijua wewe, wala<br />
watu wako, kabla ya hii (Qurani kuteremshwa). Basi subiri; hakika mwisho<br />
(mwema) utawathubutikia wanaomcha Mungu.” (Quran 11:49).<br />
Hizi ni katika khabari za siri Tulizokufunulia. na hukuwa pamoja nao<br />
walipoazimia shauri lao, hali wakifanya vitimbi vibaya. (Quran 12:102).<br />
Dr. Miller anaendelea: “Vitabu vitakatifu vingine havitumii mtindo huu,<br />
vitabu vingine vyote vina maelezo ambayo yanakwambia maelezo hayo<br />
yametokea wapi. Kwa mfano, wakati Biblia Takatifu iliyopotoshwa<br />
inazungumzia juu ya kisa cha mataifa ya kale, inakusimulia kuwa mfalme