Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
54<br />
5 IBRAHIM KHALIL AHMED (IBRAHIM KHALIL<br />
PHILOBUS) PADRI WA COPTIC NA NI MMISHIONARI<br />
(MISRI).<br />
Al-haji Ibrahimu Ahmad, zamani akiitwa Ibrahim Khalil Philobus, alikuwa ni<br />
padri wa Coptic mwenye asili ya Kimisri aliyejifunza mambo ya itikadi na<br />
kupata digrii ya juu katika chuo kikuu cha Princeton. Alijifunza <strong>Uislamu</strong> ili<br />
apate mianya ya kuushambulia; kinyume chake akaingia <strong>Uislamu</strong> akiwa<br />
pamoja na watoto wake wanne, mmoja wao kwa sasa ni profesa mwenye<br />
kung’ara katika chuo kikuu cha Sorbonne, Paris Ufaransa. Kwa njia ya<br />
kuvutia, anatumilia mitindo yake mwenyewe kwa kusema; “nimezaliwa<br />
Alexandria 13/1/1919 na niliingizwa shule ya misheni ya Kimarekani hadi<br />
nilipopata cheti cha elimu ya sekondari hapo hapo. Mnamo mwaka 1942<br />
nikapata diploma katika chuo kikuu cha Asiyut na kisha nikajikita katika<br />
masomo ya dini kama utangulizi wa kujiunga na kitengo cha itikadi. Ilikuwa<br />
si kazi nyepesi kujiunga na kitengo hicho, kwani hakukuwa na mtu atakaye<br />
kujiunga na akakubaliwa ispokuwa awe amepata kupendekezwa kwa<br />
pendekezo maalumu kutoka umoja wa kanisani na vilevile, baada ya kupasi<br />
idadi ya mitihani migumu. Nilipata pendekezo kutoka katika kanisa la Al-<br />
Attareen la Alexandria na pendekezo lingine kutoka mkusanyo wa kanisa wa<br />
Misri ya chini (maeneo ya kaskazini) baada ya kufaulu mitihani mingi ili<br />
kujua uwezo wangu wa kuja kuwa mtu wa dini kisha nikapata pendekezo la<br />
tatu kutoka mkusanyiko wa kanisa la Snodus ambalo linajumuisha makasisi<br />
wa Sudani na Misri.<br />
Kanisa la Snodus liliidhinisha niingie kitengo cha itikadi mwaka 1944 nikiwa<br />
ni mwanafunzi wa bweni. Huko nilijifunza mikononi mwa walimu wa<br />
Kimarekani na Kimisri hadi nilipohitimu mwaka 1948.<br />
Nilipendekezwa, aliendelea, niajiriwe Jerusalemu kama kusingekuwa na vita<br />
vilivyolipuka nchini Palestina mwaka huo huo, kwa hiyo. Nilipelekwa Esna<br />
Misri ya juu (maeneo ya kusini). Mwaka huo huo nilijiandikisha kwa ajili ya<br />
kusomea hoja katika chuo kikuu cha Marekani kilichopo Cairo. Jambo hilo<br />
lilikuwa linahusiana na kazi za Kimishionari kwa Waislamu. Ujuzi na uzoefu<br />
wangu juu ya <strong>Uislamu</strong> ulianzia katika kitengo cha itikadi nilpojifunza<br />
<strong>Uislamu</strong> na mifumo yote ambayo kwayo tungeweza kuyumbisha imani ya<br />
Waislamu na kuibua upotoshaji wa ufahamu wao wa dini yao wenyewe.