08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

54<br />

5 IBRAHIM KHALIL AHMED (IBRAHIM KHALIL<br />

PHILOBUS) PADRI WA COPTIC NA NI MMISHIONARI<br />

(MISRI).<br />

Al-haji Ibrahimu Ahmad, zamani akiitwa Ibrahim Khalil Philobus, alikuwa ni<br />

padri wa Coptic mwenye asili ya Kimisri aliyejifunza mambo ya itikadi na<br />

kupata digrii ya juu katika chuo kikuu cha Princeton. Alijifunza <strong>Uislamu</strong> ili<br />

apate mianya ya kuushambulia; kinyume chake akaingia <strong>Uislamu</strong> akiwa<br />

pamoja na watoto wake wanne, mmoja wao kwa sasa ni profesa mwenye<br />

kung’ara katika chuo kikuu cha Sorbonne, Paris Ufaransa. Kwa njia ya<br />

kuvutia, anatumilia mitindo yake mwenyewe kwa kusema; “nimezaliwa<br />

Alexandria 13/1/1919 na niliingizwa shule ya misheni ya Kimarekani hadi<br />

nilipopata cheti cha elimu ya sekondari hapo hapo. Mnamo mwaka 1942<br />

nikapata diploma katika chuo kikuu cha Asiyut na kisha nikajikita katika<br />

masomo ya dini kama utangulizi wa kujiunga na kitengo cha itikadi. Ilikuwa<br />

si kazi nyepesi kujiunga na kitengo hicho, kwani hakukuwa na mtu atakaye<br />

kujiunga na akakubaliwa ispokuwa awe amepata kupendekezwa kwa<br />

pendekezo maalumu kutoka umoja wa kanisani na vilevile, baada ya kupasi<br />

idadi ya mitihani migumu. Nilipata pendekezo kutoka katika kanisa la Al-<br />

Attareen la Alexandria na pendekezo lingine kutoka mkusanyo wa kanisa wa<br />

Misri ya chini (maeneo ya kaskazini) baada ya kufaulu mitihani mingi ili<br />

kujua uwezo wangu wa kuja kuwa mtu wa dini kisha nikapata pendekezo la<br />

tatu kutoka mkusanyiko wa kanisa la Snodus ambalo linajumuisha makasisi<br />

wa Sudani na Misri.<br />

Kanisa la Snodus liliidhinisha niingie kitengo cha itikadi mwaka 1944 nikiwa<br />

ni mwanafunzi wa bweni. Huko nilijifunza mikononi mwa walimu wa<br />

Kimarekani na Kimisri hadi nilipohitimu mwaka 1948.<br />

Nilipendekezwa, aliendelea, niajiriwe Jerusalemu kama kusingekuwa na vita<br />

vilivyolipuka nchini Palestina mwaka huo huo, kwa hiyo. Nilipelekwa Esna<br />

Misri ya juu (maeneo ya kusini). Mwaka huo huo nilijiandikisha kwa ajili ya<br />

kusomea hoja katika chuo kikuu cha Marekani kilichopo Cairo. Jambo hilo<br />

lilikuwa linahusiana na kazi za Kimishionari kwa Waislamu. Ujuzi na uzoefu<br />

wangu juu ya <strong>Uislamu</strong> ulianzia katika kitengo cha itikadi nilpojifunza<br />

<strong>Uislamu</strong> na mifumo yote ambayo kwayo tungeweza kuyumbisha imani ya<br />

Waislamu na kuibua upotoshaji wa ufahamu wao wa dini yao wenyewe.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!