You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
4<br />
Mungu, Yesu, Utume, dhambi na uwokovu. Lakini unajua tena, kipindi fulani<br />
nilikuwa katika boti moja na watu wengi walio katika boti hiyo sasa hivi.<br />
Kwa hakika nilikuwemo. Acha nieleze.<br />
Nimezaliwa katika familia ya Kikristo madhubuti sana katika Midwest.<br />
Familia yetu na wazee wake sio tu wamejenga makanisa na shule katika ardhi<br />
hii ya Midwest, pia walikuwa ni miongoni mwa watu wa mwanzo kufika<br />
hapo. Nilipokuwa shule ya msingi, tulikuwa tunakaa Huston, Texas mwaka<br />
1949 (nikiwa ni mtu mzima). Kila siku tulikuwa tunaenda kanisani na<br />
nilibatizwa Pasadena, Texas nikiwa na umri wa miaka 12. Nikiwa kijana wa<br />
umri wa miaka kumi na kitu, nilipendelea kutembelea makanisa mengine ili<br />
nijifunze zaidi mafundisho na imani zao. Kanisa la Kibatisti, Methodisti,<br />
Episcopalians, Charismatic movement, Full Gospel, Agepe, Katoliki,<br />
Presbyterians, na mengine mengi. Nilikuwa nimeshapevuka vizuri na kiu ya<br />
(Injili) au kama tuiitavyo; “Habari njema.” Uchunguzi wangu juu ya dini<br />
haukuishia Ukristo, hata kidogo. Ulishirikisha, dini ya Kihindu, Kiyahudi,<br />
Kibudha, Metaphizikia, imani za wamarekani asilia. Na ilikuwa ni dini moja<br />
tu ambayo sijaitazama kwa makini, nayo ilikuwa ni “<strong>Uislamu</strong>” Kwa nini?<br />
Swali zuri.<br />
Mchungaji wa Muziki<br />
Kwa vyovyote vile, nilikuwa navutiwa sana na aina mbali mbali za muziki, na<br />
hasa hasa muziki wa Injili na Klasikia. Kwa kuwa familia yangu yote ilikuwa<br />
ni ya kidini na muziki ilioufuata ndiyo huo huo nilioufuata na nikaanza<br />
masomo yangu katika maeneo hayo mawili. Mambo yote hayo yamenifanya<br />
niwe katika nafasi mwafaka ya uchungaji wa muziki katika makanisa mengi<br />
ambayo nilikuwa mshiriki wake kwa miaka mingi. Nilianza kufundisha ala ya<br />
Kibodi mnamo mwaka 1960 na hadi kufikia 1963 nilikuwa namiliki studio<br />
yangu mwenyewe eneo la Laurel, Maryland, iitwayo ‘Estes Music Studiy.’<br />
Miradi ya Biashara mjini Texas, Oklahoma na Florida.<br />
Miaka therathini iliyofuata, mimi na baba, tulifanya kazi pamoja katika miradi<br />
mingi ya kibiashara. Tulikuwa na vipindi vya burudani, kuonyesha shoo na<br />
vivutio. Tulifungua maduka ya piano na vinanda katika maeneo yote kuanzia<br />
Texas na Oklahoma hadi Florida. Tulichuma mamilioni ya dola katika miaka<br />
hiyo, lakini hatukupata utulivu wa moyo ambao unaweza kuja kwa kupitia<br />
kuufahamu ukweli na kuupata mpango sahihi wa uwokovu tu. Nina hakika<br />
kuwa umeshajiuliza swali hili “Kwa nini Mungu ameniumba?” au “Mungu<br />
ananitaka nifanye nini?” au “Nani ndiye Mungu wa kweli, kwa vyovyote