08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

46<br />

Na ilikuwa ni mwishoni mwa safari yetu ya Mashariki ya kati. Pale rafiki<br />

mmoja mzee aliyekuwa hajui Kingereza, na nikiwa natembea katika njia<br />

iliyopindapinda, njia ndogo, katika moja ya maeneo yaisioendelea kiuchumi<br />

katika mji mkongwe wa ‘Amani, Jordan.’ Tulipokuwa tunatembea, kikongwe<br />

kimoja kilitusogelea kutokea upande unaokabiliana nasi, na kusema, “Salam<br />

Alaykum”, yaani “Amani iwe juu yenu”, na akatupa mikono. Tulikuwa watu<br />

watatu tu sehemu hiyo. Sijui Kiarabu, pia rafiki yangu naye hajui, wala yule<br />

mgeni haongei Kingereza. Yule mgeni, akanitazama, na akaniniuliza,<br />

Mwislamu?<br />

Katika kipindi hiki barabara, nilikuwa nimenaswa kikamilifu. Kulikuwa<br />

hakuna mchezo wa maneno ya kiakili utakaochezwa, kwa kuwa nilikuwa<br />

ninaweza kuwasiliana kwa Kingereza tu, na wao walikuwa wanaweza<br />

kuwasiliana kwa Kiarabu tu. Kulikuwa hakuna mkalimani wa kunidhamini na<br />

kunitoa katika hali hiyo, na kuniruhusu nijifiche nyuma ya mazungumzo<br />

yangu ya Kingereza yaliyoandaliwa kwa uangalifu mkubwa. Sikuweza<br />

kujidai kuwa eti sijaelewa swali, kwa kuwa lilikuwa wazi kabisa. Uchaguzi<br />

wangu ulikuwa ni wa ghafla, usiotabirika, na usioelezeka na umepunguzwa na<br />

kubakia mambo mawili tu: nisema “Naam” yaani “Ndiyo” au niseme “La”<br />

yaani “Hapana”. Chaguo ni langu, na nilikuwa sina chaguo jengine. Kwa sasa<br />

nililoazimika kuchagua; ilikuwa ni lepesi kabisa. Allah atukuzwe, Nilijibu<br />

“Naam”.<br />

Kwa kusema neno hilo moja, michezo ya maneno ya kiakili yote ilikuwa<br />

nyuma yangu. Ikiwa michezo ya maneno ya kiakili ipo nyuma yangu, mchezo<br />

wa kisaikolojia wa kuzingatia utambulisho wangu wa kidini nao ulikuwa<br />

nyuma yangu. Sikuwa mmoja wa Wakristo wa ajabu nisiye wa kawaida.<br />

Nilikuwa Mwislamu. Allah atukuzwe, mke wangu mwenye miaka therathini<br />

na tatu akawa Mwislamu katika muda huo.<br />

Na si miezi mingi baada ya kurejea Marekani kutokea mashariki ya kati, jirani<br />

mmoja alitualika twende nyumbani kwake, na kusema kuwa anataka kuongea<br />

nasi juu ya kubadili kwetu dini na kuwa Waislamu. Alikuwa ni mchungaji<br />

mstaafu wa Kimethodisti, ambaye nilikuwa na mijadala naye mingi hapo<br />

kabla. Ingawa mara kwa mara tulikuwa tukizungumza kijuu juu kuhusiana na<br />

mambo kama uundwaji wa kibandia wa Biblia kutokana na vyanzo mbali<br />

mbali vya mwanzo vilivyotengana, kamwe hatukuwa na maongezi ya kina juu

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!