Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
46<br />
Na ilikuwa ni mwishoni mwa safari yetu ya Mashariki ya kati. Pale rafiki<br />
mmoja mzee aliyekuwa hajui Kingereza, na nikiwa natembea katika njia<br />
iliyopindapinda, njia ndogo, katika moja ya maeneo yaisioendelea kiuchumi<br />
katika mji mkongwe wa ‘Amani, Jordan.’ Tulipokuwa tunatembea, kikongwe<br />
kimoja kilitusogelea kutokea upande unaokabiliana nasi, na kusema, “Salam<br />
Alaykum”, yaani “Amani iwe juu yenu”, na akatupa mikono. Tulikuwa watu<br />
watatu tu sehemu hiyo. Sijui Kiarabu, pia rafiki yangu naye hajui, wala yule<br />
mgeni haongei Kingereza. Yule mgeni, akanitazama, na akaniniuliza,<br />
Mwislamu?<br />
Katika kipindi hiki barabara, nilikuwa nimenaswa kikamilifu. Kulikuwa<br />
hakuna mchezo wa maneno ya kiakili utakaochezwa, kwa kuwa nilikuwa<br />
ninaweza kuwasiliana kwa Kingereza tu, na wao walikuwa wanaweza<br />
kuwasiliana kwa Kiarabu tu. Kulikuwa hakuna mkalimani wa kunidhamini na<br />
kunitoa katika hali hiyo, na kuniruhusu nijifiche nyuma ya mazungumzo<br />
yangu ya Kingereza yaliyoandaliwa kwa uangalifu mkubwa. Sikuweza<br />
kujidai kuwa eti sijaelewa swali, kwa kuwa lilikuwa wazi kabisa. Uchaguzi<br />
wangu ulikuwa ni wa ghafla, usiotabirika, na usioelezeka na umepunguzwa na<br />
kubakia mambo mawili tu: nisema “Naam” yaani “Ndiyo” au niseme “La”<br />
yaani “Hapana”. Chaguo ni langu, na nilikuwa sina chaguo jengine. Kwa sasa<br />
nililoazimika kuchagua; ilikuwa ni lepesi kabisa. Allah atukuzwe, Nilijibu<br />
“Naam”.<br />
Kwa kusema neno hilo moja, michezo ya maneno ya kiakili yote ilikuwa<br />
nyuma yangu. Ikiwa michezo ya maneno ya kiakili ipo nyuma yangu, mchezo<br />
wa kisaikolojia wa kuzingatia utambulisho wangu wa kidini nao ulikuwa<br />
nyuma yangu. Sikuwa mmoja wa Wakristo wa ajabu nisiye wa kawaida.<br />
Nilikuwa Mwislamu. Allah atukuzwe, mke wangu mwenye miaka therathini<br />
na tatu akawa Mwislamu katika muda huo.<br />
Na si miezi mingi baada ya kurejea Marekani kutokea mashariki ya kati, jirani<br />
mmoja alitualika twende nyumbani kwake, na kusema kuwa anataka kuongea<br />
nasi juu ya kubadili kwetu dini na kuwa Waislamu. Alikuwa ni mchungaji<br />
mstaafu wa Kimethodisti, ambaye nilikuwa na mijadala naye mingi hapo<br />
kabla. Ingawa mara kwa mara tulikuwa tukizungumza kijuu juu kuhusiana na<br />
mambo kama uundwaji wa kibandia wa Biblia kutokana na vyanzo mbali<br />
mbali vya mwanzo vilivyotengana, kamwe hatukuwa na maongezi ya kina juu