08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

47<br />

ya dini. Nilichojua ni kuwa amepata elimu madhubuti ya seminari, na alikuwa<br />

anaimba katika kwaya ya kanisa la mtaani kila Jumapili.<br />

Mwitikio wangu wa awali ulikuwa ni “Oh, oh, hilo linakuja”. Hata hivyo, ni<br />

wajibu wa Mwislamu awe jirani mwema, na ni wajibu wa Mwislamu kutaka<br />

kujadili <strong>Uislamu</strong> na watu wengine. Kwa hiyo, nilikubali ule mwaliko wa jioni<br />

ifuatayo na nilitumia muda mwingi niliokuwa ni macho wa saa 24 zilizofuatia<br />

katika kutafakari nanma nzuri ya kumwendea muungwana huyu katika mada<br />

ya maombi yake. Muda tuliokubaliana ukafika, na tukaendesha gari yetu hadi<br />

tukafika kwa jirani yetu. Baada ya muda mchache wa maongezi madogo,<br />

yeye, mwishowe, aliuliza kwa nini nimeamua kuwa Mwislamu. Nilikuwa<br />

ninalingojea swali hilo, na nilikuwa nimeshaandaa vizuri jibu langu. “Kama<br />

ujuavyo ukiwa na elimu ya seminari, kuna mambo mengi yasio ya kidini<br />

ambayo yametayarishwa na kuunda maamuzi ya Baraza la Nicaea.” Naye<br />

kwa haraka haraka akanikatiza kwa sentensi nyepesi: “Wewe hatimaye<br />

hukupendezwa na imani ya kuabudu miungu mingi, au siyo?” alijibu<br />

kikamilifu kwa nini nilikuwa Mwislamu, naye hakupinga maamuzi yangu!<br />

Yeye mwenyewe, kwa umri wake na nafasi yake maishani, alichagua awe<br />

“Mkristo wa aina yake”. Allah anamtaka, na hadi kufikia sasa ameshamaliza<br />

safari yake kutoka msalabani hadi mwezini.<br />

Kuna muhanga unaotakiwa kutolewa kwa kuwa Mwislamu nchini Marekani.<br />

Katika jambo hilo, kuna muhanga unaotakiwa kutolewa kwa kuwa<br />

Mwislamu sehemu yeyote ile. Hata hivyo, inawezekana kuwa ni mikali sana<br />

Marekani na hasa hasa miongoni mwa waliobadili dini katika Wamarekani.<br />

Baadhi ya mihanga hiyo ni yenye kutabirika ikiwemo kubadili mavazi na<br />

kujizuia na pombe, nguruwe, na kuvutiwa na pesa za mtu mwingine. Baadhi<br />

ya mihanga hiyo haitabiriki kwa mfano, familia moja ya Kikristo, ambayo<br />

ilikuwa ni mrafiki zetu wa karibu, ilitufahamisha kuwa hawatoshirikiana nasi<br />

tena, kwa kuwa wao hawashirikiani na mtu yeyote “ambaye hamfanyi Yesu<br />

Kristo kuwa ndiye mwokozi wake.” Kwa kuongezea, baadhi ya wafanyakazi<br />

wenzangu wachache wamebadili tabia zao za kufungamana nami. Ima jambo<br />

hilo lilikuwa la upatanifu au la pato langu la kazi, nalo lilipungua na kulikuwa<br />

na takriban 30% inashuka katika pato langu kama matokeo ya hayo. Baadhi<br />

ya mihanga hiyo isiyotabirika ilikuwa ni mikali mno kuikubali, ingawa<br />

mihanga ilikuwa ni thamani ndogo sana kuilipa kwa kile kilichopatikana<br />

kama malipo mbadala.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!