Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
53<br />
familia ya mume wangu, nilifahamika vibaya na watoto wangu wakubwa, na<br />
nilikuwa napelelezwa na serikali yangu mwenyewe. Bila ya kuwa na imani<br />
ambayo inamuwezesha mtu kusimama kidete dhidi ya nguvu za shetani<br />
nisingeweza kuhimili mambo yote hayo. Mimi ninamshukuru sana Allah kwa<br />
kuwa mimi ni Mwislamu na naomba niishi na kufa nikiwa ni Mwislamu.<br />
“Sema: “hakika Sala yangu, na ibada zangu (zote nyingine) na uzima wangu,<br />
na kufa kwangu; (zote) ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Muumba wa<br />
walimwengu wote. (Likinisibu jambo limenisibu kwa kutaka Mwenyezi Mungu<br />
si kwa kutaka viumbe vyake. Na yote ninayoyafanya nayafanya kwa ajili<br />
Yake). Hana mshirika. Na hayo ndiyo niliyoamrishwa, na mimi ni wa kwanza<br />
wa waliojisalimisha (kwa Mwenyezi Mungu).” Quran 8 6:162-163<br />
Sista Khadija Watson anafanyakazi ya ualimu wa wanawake katika moja ya<br />
vituo vya Da`wah (kuwaita watu waingie <strong>Uislamu</strong>) kilichopo Jeddah, Falme<br />
ya Kiarabu ya Saudia - Arabia.<br />
8 Tafsiri za aya za Quran kwa kiswahili zimenukuliwa kutoka QURANI TAKATIFU ya marehemu Sheikh<br />
Abdullah Saleh Al-Farsy