Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
19<br />
akatangaza kuwa <strong>Uislamu</strong> ndiyo njia ya uwokovu kwake, mama yangu mzazi<br />
na watu wengine katika familia waliendelea kukasirishwa na kuingia kwetu<br />
katika <strong>Uislamu</strong> hapo mwanzoni. Mwishoni mambo yakawa ya kawaida na<br />
tuliishi kwa ukaribu, ingawa wao bado wanajihusisha na Ukristo.<br />
Allah anaahidi kuwatia majaribuni wale wote wanaotangaza imani yao juu<br />
yake, kwa kuwapa aina nyingi za mambo magumu magumu, na familia ni<br />
moja ya mambo hayo yaliyotajwa kuwa ni jaribio ndani ya Quran.<br />
Nanawaombea Allah awaongoze wafuate kitu kilicho bora kabisa duniani na<br />
Ahera. Lakini juu ya Allah, kama anawataka wawe katika utiifu kwake<br />
(<strong>Uislamu</strong> maana yake ni, utiifu kwa Allah) au kama hataki kuwa hivyo.<br />
4- “Vipi kuhusu usharika wako? Wamesema nini?<br />
Jibu: Kamwe sijawahi kuwa na kanisa langu mwenyewe. Nilikuwa ni<br />
mchungaji wa muziki kanisa la Mungu (Anderson, Indiana branch) mjini<br />
Texas na nilikuwa natoa mahubiri yangu kwa wafanyabiashara na kwa<br />
makutano yasiyo ya kawaida. Wote wanaonijua kwa sehemu kubwa hawana<br />
kizuizi na baadhi yao wameshaingia katika <strong>Uislamu</strong>, lakini kuna wachache<br />
ambao walihisi kuchanganyikiwa sana na wakanitukana, kwa “kumkana<br />
Yesu, amani iwe juu yake.” Bila kujali kile nilichojaribu kukisema au<br />
kukitenda, hawa watu maalumu walio wachache hawasikilizi wala hawataki<br />
chochote kinachohusu <strong>Uislamu</strong>.<br />
5- Je, umeshapata matatizo mengi kwa kubadili dini?<br />
Jibu: Bila ya shaka, kila mtu atakaye kuuzingatia <strong>Uislamu</strong> siku hizi, kama<br />
ilivyokuwa mida iliyopita, lazima atambue kuwa kutakuwa na matatizo ya<br />
majaribio maalumu katika njia yake hiyo. Wafuasi wa Yesu, amani iwe juu<br />
yake, walikosolewa na kuteswa sana hadi walifikia kuuliwa (soma kile<br />
alichokisema Paulo kwamba alikuwa anakifanya kwa wanafunzi wa Yesu<br />
ndani ya Biblia; kitabu cha Matendo ya Mitume). Wote waliomfuata<br />
Muhammad, amani iwe juu yake, waliteswa mikononi mwa watu wa<br />
makabila yao wenyewe, ndiyo kuwa, walikuwa wameshaazimia kumwabudu<br />
Mungu Muweza peke yake, bila ya mshirika na kutii matakwa yake.<br />
Tatizo kubwa kwa wasiokuwa Waislamu ni, ukosefu wao wa elimu na<br />
ufahamu juu ya nini ndiyo <strong>Uislamu</strong> wa kweli na akina nani wanaozingatiwa