You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
63<br />
Mungu (tu) ndiye anayestahiki kukusudiwa (na viumbe Vyake vyote kwa<br />
kumwabudu na kumuomba na kumtegemea). Hakuzaa wala Hakuzaliwa.<br />
Wala hana anaefanana Naye hata mmoja.” Anakumbuka jambo hilo. Na hiyo<br />
ilikuwa pale mbegu za <strong>Uislamu</strong>, hazijulikani kwake na zilikuwa ni mara ya<br />
kwanza kuonekana. Na ilikuwa ni hapo alipogundua kuwa Qurani ndicho<br />
Kitabu cha pekee kisichovurugwa na wanadamu tangu kilipoteremshwa. “Na<br />
katika kuhitimisha uchunguzi wangu wa uzamili nilisema hivyo. Sikujua<br />
kama watanipa stashahada yangu ya uzamili au hawanipi – huo ndiyo<br />
uliokuwa ukweli, na nilikuwa nautaka ukweli.”<br />
Alipokuwa katika hali hiyo ya kiakili alimwita profesa wake ampendaye sana:<br />
bwana Van Burger. “Nilifunga mlango, na kumwangalia machoni na<br />
kumuuliza “katika dini zote duniani ni ipi ya ukweli?” Akajibu ni <strong>Uislamu</strong>.<br />
“Kwa nini wewe si Mwislamu? Niliuliza tena. Akaniambia: “Mosi,<br />
nawachukui Waarabu, pili, Je, unaviona vitu vya anasa vyote hivi<br />
niliovyonavyo? Je, unadhani itakuwaje kama nitavitupa vitu vyote hivi kwa<br />
ajili ya <strong>Uislamu</strong>?” Nilipofikiri kuhusu majibu yake, pia nilifikiria nafsi yangu<br />
mwenyewe.” Anakumbuka Mwaipopo. Kazi yake, gari zake, vyote hivyo<br />
katika taswira yake. Hapana, hatoingia <strong>Uislamu</strong>, na kwa mwaka mmoja<br />
madhubuti, aliliweka jambo hilo nje ya akili yake. Lakini baadaye ndoto<br />
zilikuwa zikimjia kwa kumsumbua, Aya za Quran ziliendelea kumtokea, watu<br />
waliovalia nguo nyeupe waliendelea kumjia. “Hasa hasa siku za Ijumaa; hadi<br />
alipofikiria kuwa hawezi kuvumilia tena jambo hilo.<br />
Kwa hiyo, mnamo tarehe 22 Desemba, aliingia <strong>Uislamu</strong> kirasmi. Ndoto hizo<br />
zilizomwongoza - Je, hazikuwa za “kishirikina” kama ilivyo kwa tabia za<br />
Kiafrika? “Hapana, siamini kuwa ndoto zote ni mbaya. Kwani kuna zile<br />
ambazo zinakuongoza katika mwelekeo sahihi, na kuna nyingine hazifanyi<br />
hivyo, na za kwangu, kwa upekee kabisa zimeniongoza katika mwelekeo<br />
sahihi, kuufikia <strong>Uislamu</strong>,” ametueleza.<br />
Kwa hiyo, kanisa lilimnyang`anya nyumba na gari. Mkewe hakuweza<br />
kuvumilia hayo, akafungasha virago vyake, akachukua watoto wake na<br />
kuondoka, licha ya Mwaipopo kumuhakikishia kuwa halazimishwi awe<br />
Mwislamu. Mwaipopo alipoenda kwa wazazi wake nao pia, walikuwa<br />
wameshasikia habari zake. “Baba yangu aliniambia niukane <strong>Uislamu</strong> na<br />
mama yangu, yeye alisema: “Hataki kusikia upuuzi wowote kutoka kwangu;”<br />
alikumbushia Mwaipopo. Naye alikuwa kivyake vyake! Aliulizwa vipi<br />
anajihisi hivi sasa kwa upande wa wazazi wake, anasema kuwa