08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

57<br />

humuamini Mwenyezi Mungu na maneno Yake. Na mfuateni yeye ili mpate<br />

kuongoka.” (Qurani 7:157-158).<br />

Kwa sasa yaani usiku ule ule, Bwana Khalil kama mchezo wa kuigiza<br />

alihitimisha: “Nilichukua uamuzi wangu wa mwisho. Wakati wa asubuhi<br />

nilizungumza na mke wangu ambaye nilizaa naye watoto wa kiume watatu na<br />

wa kike mmoja. Lakini haukupita muda mrefu hadi akadadisi kuwa mimi<br />

naelekea kuingia <strong>Uislamu</strong> naye akalia na kuomba msaada kwa mkuu wa<br />

misheni. Jina lake lilikuwa ni Monsieur Shavits kutoka Uswizi. Bwana huyo<br />

alikuwa ni mtu mjanja sana. Aliponiuliza kuhusu mtazamo wangu wa kweli,<br />

nilimwambia kinaganaga kile nilichokuwa nakitaka na kisha akasema: Hebu<br />

jifanye kuwa upo nje ya kazi hadi tutakapojua nini kimekutokea. Kisha<br />

nilisema: hii ndiyo barua yangu ya kuacha kazi. Alijaribu kunikinaisha<br />

niahirishe jambo hilo, lakini mimi niling`ang`ania. Kwa hiyo, yeye<br />

akatengeneza uvumi kwa watu kuwa nimekuwa chizi. Kwa hiyo, niliteseka<br />

vikali kwa mtihani huo mkali na ukandamizwaji hadi nilipoondoka na<br />

kuuacha mji wa Aswan kwa wema na kurudi Cairo.”<br />

Alipoulizwa juu ya hali ya kubadili kwake dini alijibu: “Mjini Cairo<br />

nilitambulishwa kwa profesa mmoja anaheshimika sana ambaye alinisaidia<br />

kuyashinda majaribu yangu yaliyokuwa makali mno na alifanya hivyo bila ya<br />

kujua chochote juu ya mkasa wangu. Alinitendea kama Mwislamu kwani<br />

nilijitambulisha kwake hivyo ingawa hadi wakati huo nilikuwa sijaingia<br />

<strong>Uislamu</strong> kirasmi. Huyo bwana alikuwa ni: Dr. Muhammad Abdul Moneim Al<br />

Jamal ambaye ni mtunza hazina mkuu. Naye alikuwa anajishughulisha na<br />

masomo ya Kiislamu na alitaka kutafsiri Quran Tukufu ikachapishwe<br />

Marekani. Aliniomba nimsaidie kwa sababu nilikuwa nafahamu vizuri<br />

Kingereza kwa kuwa nilipata stashahada yangu ya M.A katika chuo kikuu cha<br />

Marekani. Pia alijua kuwa nilikuwa najiandaa kufanya uchunguzi wa<br />

mlinganisho wa Quran, Taurati na Biblia. Tukashirikiana katika uchunguzi<br />

huo wa mlinganisho na katika kutafsiri Quran. Wakati: Dr. Jamal alipojuwa<br />

kuwa nimeacha kazi huko Aswan na kwa hiyo, sina kazi, alinisaidia kwa<br />

kunipatia kazi katika shirika la Standard Stationary mjini Cairo. Kwa hiyo,<br />

nilijiunda vizuri baada ya muda mfupi. Sikumwambia mke wangu nia yangu<br />

ya kuingia <strong>Uislamu</strong> kwa hiyo, alifikiria kuwa nimeshasahau mambo yote na<br />

sikuwa na lolote ila ni mgogoro wa mpito ambao haupo tena. Lakini, nilijua<br />

vizuri kabisa kuwa kusilimu kwangu kirasmi na kuingia <strong>Uislamu</strong> kunahitaji<br />

majaribio ya kutatanisha marefu na kwa hakika ilikuwa ni vita ambavyo

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!