You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
36<br />
kutoka kanisa la muungano wa Wamethodosti. Baada ya kumaliza chuo cha<br />
Havard mwaka 1971, nilijiandikisha shule ya Utakatifu ya Havard, na hapo<br />
nilipata stashahada ya uzamili juu ya theolojia mwaka 1974, baada ya<br />
kusimikwa kikamilifu katika ushemasi wa muungano wa makanisa ya<br />
Methodisti mwaka 1972, na kwa kuwa, hapo kabla nilipata udhamini wa<br />
masomo wa Stewart Scholarship kutoka muungano wa makanisa ya<br />
Methodisti ikiwa ni kama nyongeza ya udhamini wangu wa Havard Divinity<br />
School. Nikiwa katika elimu ya seminari, pia nilimaliza masomo ya nje ya<br />
vipindi vya miaka miwili ya ukasisi wa mahospitalini katika hospitali ya Peter<br />
Bent Brigham mjini Boston. Baada ya kumaliza masomo katika shule ya<br />
utakatifu ya Havard, niliutumia wakati wa kiangazi nikiwa ni mchungaji wa<br />
makanisa mawili ya Methodisti katika viunga vya Kansas, ambako<br />
mahudhurio yalipanda juu kwa kiwango ambacho hakijawahi kuonekana<br />
katika makanisa yote hayo kwa miaka kadhaa.<br />
Kwa nje ilionyesha kuwa, nilikuwa mchungaji kijana mwenye kutunza ahadi<br />
sana ambaye amepokea elimu bora zaidi, kuvutia kundi kubwa la watu katika<br />
ibada ya Jumapili asubuhi, na kulikuwa na mafanikio katika kila kituo<br />
kwenye njia ya utumishi. Hata hivyo, kwa ndani ilionyesha, nilikuwa<br />
napambana vita vya daima kudumisha msimamo wangu binafsi katika uso wa<br />
majukumu ya utumishi. Vita hivi vilikuwa mbali sana na vile<br />
vinavyotazamiwa vya kupambana na baadhi ya wainjilisti wa hivi karibuni<br />
katika majaribio yasiofanikiwa ya kuendeleza utu wa kiroho na kingono.<br />
Hivyo, ilikuwa ni vita tofauti sana na vile nilivyopambana na mapadri<br />
Pedophilic waliotamba katika vichwa vya habari vya zama za sasa. Hata<br />
hivyo, mihangaiko yangu ya kudumisha uadilifu wa utu wangu huenda ikawa<br />
ni jambo la kawaida kukabiliwa na wanachama wa utumishi wenye elimu<br />
bora sana.<br />
Kuna aina fulani ya kejeli katika ukweli kwamba wale wanaodhaniwa kuwa<br />
ni watumishi bora kabisa wanaochaguliwa kwa elimu bora kabisa ya<br />
seminari, kwa mfano: wale wanaopewa ofa katika muda ule wa shule ya<br />
Theolojia ya Harvard. Kejeli ni kuwa, kwa kupewa elimu hiyo, wanaseminari<br />
wanawekewa wazi historia nyingi ya ukweli kama inavyojulikana: 1)-<br />
maelezo ya kanisa la mwanzo, na vipi lilijengwa kwa siasa ya nchi kama<br />
inavyoathiriwa na mambo ya kijografia. 2)- masomo “asilia” ya maandiko<br />
mbali mbali ya Kibiblia, mengi yao yakiwa katika makindano makali na yale<br />
yanayosomwa na Wakristo wengi wanapobeba Biblia zao, ingawa kidogo,<br />
baadhi ya maelezo hayo hayajaharibiwa na kutiwa katika tafsiri mpya na bora