08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

26<br />

fahari ya kanisa. Kila mtu alikuwa na matarajio makubwa juu yangu, na<br />

nilikuwa ninafuraha kwa mara nyingine tena kuwa hivyo, “katika njia ya<br />

kuelekea uwokovu.”<br />

Nilihudhuria kanisani kila mara ilipofunguliwa milango yake. Nilijifunza<br />

Biblia kwa masiku na mawiki, katika kipindi hicho. Nilihudhuria mihadhara<br />

iliyotolewa na wanazuoni wa Kikristo wa zama zangu, na nikajulikana na<br />

kualikwa katika uchungaji nikiwa na miaka ishirini. nilianza kuhubiri na<br />

kuwa mashuhuri sana, upesi upesi. Nilikuwa naamini na kung’ang’ania<br />

kikamilifu kuwa hakuna atakayepata uwokovu ila awe katika kundi la kanisa<br />

langu. Nami kwa waziwazi nilimlaumu kila mtu ambaye hakumjua Mungu<br />

kwa njia niliyomjua mimi. Nilifundishwa kuwa Yesu Kristo (amani iwe juu<br />

yake) na Mungu Muweza walikuwa ni kitu kimoja. Nilifundishwa kuwa<br />

kanisa letu haliamini utatu lakini Yesu (amani iwe juu yake) kwa hakika<br />

ndiye aliyekuwa Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Mimi mwenyewe<br />

nilijaribu kutaka kuelewa jambo hilo, hivyo, nililazimika kukiri kuwa jambo<br />

hilo haliingii akilini mwangu (halifahamiki). Niliheshimu nguo takatifu za<br />

wanawake na tabia njema ya wanaume. Nilifurahia kuitekeleza imani, pale<br />

ambako wanawake walitakiwa wavae maguo yanayowafunika gubi gubi,<br />

wasitie rangi nyuso zao kwa vipodozi, na wawe mabalozi wa kweli wa Kristo.<br />

Nilikinaishwa nyuma ya pazia ya mashaka kuwa hatimaye nimepata njia ya<br />

kweli ya kuingia katika furaha ya kweli. Nilikuwa nabishana na yeyote wa<br />

kutoka kanisa lolote na imani yeyote na nilikuwa nawanyamazisha kabisa<br />

kabisa kwa elimu yangu ya Biblia. Nimehifadhi mamia ya vifungu vya Biblia,<br />

na hilo lilikuwa ndilo nembo ya mahubiri yangu. Naam, hata hivyo, nilihisi<br />

kuwa kwa hakika nipo katika njia iliyosahihi, na sehemu yangu nyingine<br />

ilikuwa bado inatafuta. Nilihisi kuwa kulikuwa na ukweli wa hali ya juu<br />

ambao unatakiwa ufikiwe.<br />

Nilipokuwa peke yangu nilikuwa natafakari na kumuomba Mungu aniongoze<br />

katika dini sahihi na anisamehe ikiwa kile nilichokuwa nakitenda kilikuwa ni<br />

makosa. Kamwe nilikuwa sijawahi kuwa na mawasiliano na Waislamu. Watu<br />

pekee wanaodai kuwa <strong>Uislamu</strong> ndiyo dini yao walikuwa ni wafuasi wa Elijah<br />

Muhammad, ambao walikuwa wakizingatiwa na watu wengi kuwa ni<br />

“Waislamu Weusi” au “The Lost-Found Nation.” Na ilikuwa katika kipindi<br />

hiki mwishoni mwa miaka ya sabini pale mchungaji Louis Farrakhani kwa<br />

hakika, alikuwa vizuri katika kukijenga upya kile kilichojulikana kama ni<br />

“Taifa la Kiislamu” nilienda kumsikiliza mchungaji Farrakhani alipokuwa<br />

akizungumza katika mwaliko wa wafanyakazi wa ushirika na nikakata shauri

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!