You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
26<br />
fahari ya kanisa. Kila mtu alikuwa na matarajio makubwa juu yangu, na<br />
nilikuwa ninafuraha kwa mara nyingine tena kuwa hivyo, “katika njia ya<br />
kuelekea uwokovu.”<br />
Nilihudhuria kanisani kila mara ilipofunguliwa milango yake. Nilijifunza<br />
Biblia kwa masiku na mawiki, katika kipindi hicho. Nilihudhuria mihadhara<br />
iliyotolewa na wanazuoni wa Kikristo wa zama zangu, na nikajulikana na<br />
kualikwa katika uchungaji nikiwa na miaka ishirini. nilianza kuhubiri na<br />
kuwa mashuhuri sana, upesi upesi. Nilikuwa naamini na kung’ang’ania<br />
kikamilifu kuwa hakuna atakayepata uwokovu ila awe katika kundi la kanisa<br />
langu. Nami kwa waziwazi nilimlaumu kila mtu ambaye hakumjua Mungu<br />
kwa njia niliyomjua mimi. Nilifundishwa kuwa Yesu Kristo (amani iwe juu<br />
yake) na Mungu Muweza walikuwa ni kitu kimoja. Nilifundishwa kuwa<br />
kanisa letu haliamini utatu lakini Yesu (amani iwe juu yake) kwa hakika<br />
ndiye aliyekuwa Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Mimi mwenyewe<br />
nilijaribu kutaka kuelewa jambo hilo, hivyo, nililazimika kukiri kuwa jambo<br />
hilo haliingii akilini mwangu (halifahamiki). Niliheshimu nguo takatifu za<br />
wanawake na tabia njema ya wanaume. Nilifurahia kuitekeleza imani, pale<br />
ambako wanawake walitakiwa wavae maguo yanayowafunika gubi gubi,<br />
wasitie rangi nyuso zao kwa vipodozi, na wawe mabalozi wa kweli wa Kristo.<br />
Nilikinaishwa nyuma ya pazia ya mashaka kuwa hatimaye nimepata njia ya<br />
kweli ya kuingia katika furaha ya kweli. Nilikuwa nabishana na yeyote wa<br />
kutoka kanisa lolote na imani yeyote na nilikuwa nawanyamazisha kabisa<br />
kabisa kwa elimu yangu ya Biblia. Nimehifadhi mamia ya vifungu vya Biblia,<br />
na hilo lilikuwa ndilo nembo ya mahubiri yangu. Naam, hata hivyo, nilihisi<br />
kuwa kwa hakika nipo katika njia iliyosahihi, na sehemu yangu nyingine<br />
ilikuwa bado inatafuta. Nilihisi kuwa kulikuwa na ukweli wa hali ya juu<br />
ambao unatakiwa ufikiwe.<br />
Nilipokuwa peke yangu nilikuwa natafakari na kumuomba Mungu aniongoze<br />
katika dini sahihi na anisamehe ikiwa kile nilichokuwa nakitenda kilikuwa ni<br />
makosa. Kamwe nilikuwa sijawahi kuwa na mawasiliano na Waislamu. Watu<br />
pekee wanaodai kuwa <strong>Uislamu</strong> ndiyo dini yao walikuwa ni wafuasi wa Elijah<br />
Muhammad, ambao walikuwa wakizingatiwa na watu wengi kuwa ni<br />
“Waislamu Weusi” au “The Lost-Found Nation.” Na ilikuwa katika kipindi<br />
hiki mwishoni mwa miaka ya sabini pale mchungaji Louis Farrakhani kwa<br />
hakika, alikuwa vizuri katika kukijenga upya kile kilichojulikana kama ni<br />
“Taifa la Kiislamu” nilienda kumsikiliza mchungaji Farrakhani alipokuwa<br />
akizungumza katika mwaliko wa wafanyakazi wa ushirika na nikakata shauri