Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
68<br />
saba ya Biblia. Nilianza kuwahubiria makutano mengine. Nilikubaliwa katika<br />
shule ya Brooklyn, New York, ni shule ya tabaka bora sana waimilikayo<br />
Mashahidi wa Yehova “the Crème de la crème, ni ya kwanza kwa kuwa na<br />
asilimia kubwa. Lakini sikuenda.<br />
Vitu vichache ambavyo kwa sasa haviniingii akilini. Kwa mfano, mfumo wa<br />
sehemu ya haki. Jambo hilo linaonekana kama vile kila mara nilipotaka<br />
kupinda kona nakujikuta katika nafasi nyingine ya majukumu, nililazimika<br />
vitu hivyo vya kisekyula ili kuuthibitisha uungu wangu. Hiyo ni kwa kuwa<br />
kama utafikia malengo ya sehemu yako ya haki ya mwezi huu, Mungu<br />
anakupenda. Na kama hutafikia sehemu yako ya haki katika mwezi unaofuata<br />
Mungu hakupendi. Jambo hilo halikuniingia akilini kabisa kabisa. Mwezi<br />
mmoja ananipenda na mwezi mwengine hanipendi?<br />
Kitu kingine nilichoanza kukiona ni mtazamo wa njia ya chini. Mashahidi wa<br />
Yehova ni watu pekee watakaookolewa katika mpango mpya wa Mungu,<br />
hakuna mtu mwingine atakayeokoka, kwa sababu, watu hao wanatekeleza<br />
dini ya uongo. Sawa, nilifikiria: mama Tereza wa Kikatoliki. Huyo ni adui<br />
yetu wa kutisha. Kwa hiyo, nilisema ngoja kidogo mama Tereza ametoa<br />
maisha yake yote akifanya vitu alivyosema Yesu: kuwalea masikini,<br />
wagonjwa na mayatima. Lakini hatopata huruma za Mungu kwa sababu ni<br />
Mkatoliki?<br />
Tulikuwa tunalikosoa kanisa la Kikatoliki kwa sababu Wakatoliki wana mtu<br />
ambaye ni padri, wanamwendea na kuungama dhambi zao kwake. Na tuna<br />
msemo “Usiende kwa mtu kuungama dhambi zako! Dhambi zako ni dhidi ya<br />
Mungu!” Ndiyo sisi tulienda kwa baraza la wazee. Unaungama dhambi zako<br />
kwao, na wao wanakuwekea mkono, na walisema [mzee ni kama oporeta wa<br />
simu:] “Jizuie kwa dakika moja hivi … unafikiri nini, bwana? Hapana? …<br />
sawa, samahani tumejaribu vya kutosha lakini wewe bado hujatibika vya<br />
kutosha. Dhambi zako ni kubwa mno, kwa hiyo, ima upoteze ufuasi wako<br />
kanisani au upelekwe majaribuni.”<br />
Ikiwa dhambi ni dhidi ya Mungu, Je, sikupaswa nimwelekee Mungu moja<br />
kwa moja na kumuomba msamaha?<br />
Uhenda msumari uliogongelewa jeneza ulikuwa ni ule ule niliouna kuwa wao<br />
waliianza kuisoma Biblia kidogo tu. Mashahidi wa Yehova wana vitabu vya<br />
kila kitu ambavyo vimetayarishwa na mnara wa wachunguzi wa Biblia na<br />
jumuia ya vitabu vya dini watu pekee katika sayari nzima ya dunia