08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

73<br />

Alidhani kuwa mimi tayari ni mwenziwao.<br />

Nikasema; “Ndiyo bwana” [kinyenyekevu].<br />

Sikujua kwa nini nilirejeshwa nyuma, lakini hata hivyo, nilirudi nyuma.<br />

Walikuwa na hema na mazuria yaliyokuwa nje. Nilisimama hapo, kwa aina<br />

fulani ya kuona haya, na walikuwa wamekaa chini na kusikiliza mahubiri. Na<br />

watu wengine wakasema, nenda mbele, ndugu, kaa chini. Nami ninaenda,<br />

hapana, shukrani, hapana, shukrani, ninawatembelea tu.<br />

Kwa hiyo, mwishowe mahubiri yakaisha. Wote walipamga mstari ili waswali<br />

na wakasujudu. Kwa hakika nilirejeshwa nyuma yaani nilikumbushwa kujua<br />

mambo ya nyuma.<br />

Nilianza kutia akilini, katika mishipa yangu, mifupa yangu, moyoni mwangu<br />

na roho yangu. Kwani sala imeisha. Nasema, oyaa, nani atakayenitambua?<br />

Kwa hiyo, nilianza kujichanganya kama vile mimi ni mmoja wao, na nilikuwa<br />

natembea msikitini na ndugu mmoja anasema, “Assalaamu alaykum.” Nami<br />

nafikiria, Je amesema: “Chumvi na nyama.”<br />

“Assalaamu alaykum.”<br />

Kuna mtu mwingine aliyeniambia “Chumvi na nyama.”<br />

Sikujua kitu gani katika dunia hii wanachokisema, lakini wote walitabasamu.<br />

Kabla ya mmoja wao kugundua kuwa mimi si mtu wa kuwa hapo na<br />

akanichukua hadi chumba cha mateso, au cha kunikata kichwa, nilitaka kuona<br />

mambo mengi niwezayo kuyaona. Kwa hiyo, hatimaye, nilienda maktaba na<br />

huko kulikuwa na ndugu wa Kimisri; jina lake lilikuwa ni Omar Mungu<br />

ameniletea mtu huyo.<br />

Omar alinijia, na akasema, “samahani. Je, hii ndiyo mara yako ya kwanza<br />

kuja hapa? Kwa hakika alikuwa na lahaja nzito.<br />

Nikasema; eenhe, ndiyo.<br />

“Oh, vizuri sana. Je, wewe ni Mwislamu?”<br />

“Hapana, nasoma kidogo tu.”<br />

“Oh, wewe unajifunza? Hii ndiyo mara yako ya kwanza kutembelea<br />

msikitini?”<br />

“Ndiyo.”<br />

“Njoo, acha nikuonyeshe sehemu hii.” Na akaninyanyua kwa mkono, nikawa<br />

natembea kwa nguvu ya mtu mwingine – tulikamatana mikono. Nilisema,<br />

Waislamu hawa ni marafiki. Kwa hiyo, akanionyesha maeneo hayo.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!