Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
73<br />
Alidhani kuwa mimi tayari ni mwenziwao.<br />
Nikasema; “Ndiyo bwana” [kinyenyekevu].<br />
Sikujua kwa nini nilirejeshwa nyuma, lakini hata hivyo, nilirudi nyuma.<br />
Walikuwa na hema na mazuria yaliyokuwa nje. Nilisimama hapo, kwa aina<br />
fulani ya kuona haya, na walikuwa wamekaa chini na kusikiliza mahubiri. Na<br />
watu wengine wakasema, nenda mbele, ndugu, kaa chini. Nami ninaenda,<br />
hapana, shukrani, hapana, shukrani, ninawatembelea tu.<br />
Kwa hiyo, mwishowe mahubiri yakaisha. Wote walipamga mstari ili waswali<br />
na wakasujudu. Kwa hakika nilirejeshwa nyuma yaani nilikumbushwa kujua<br />
mambo ya nyuma.<br />
Nilianza kutia akilini, katika mishipa yangu, mifupa yangu, moyoni mwangu<br />
na roho yangu. Kwani sala imeisha. Nasema, oyaa, nani atakayenitambua?<br />
Kwa hiyo, nilianza kujichanganya kama vile mimi ni mmoja wao, na nilikuwa<br />
natembea msikitini na ndugu mmoja anasema, “Assalaamu alaykum.” Nami<br />
nafikiria, Je amesema: “Chumvi na nyama.”<br />
“Assalaamu alaykum.”<br />
Kuna mtu mwingine aliyeniambia “Chumvi na nyama.”<br />
Sikujua kitu gani katika dunia hii wanachokisema, lakini wote walitabasamu.<br />
Kabla ya mmoja wao kugundua kuwa mimi si mtu wa kuwa hapo na<br />
akanichukua hadi chumba cha mateso, au cha kunikata kichwa, nilitaka kuona<br />
mambo mengi niwezayo kuyaona. Kwa hiyo, hatimaye, nilienda maktaba na<br />
huko kulikuwa na ndugu wa Kimisri; jina lake lilikuwa ni Omar Mungu<br />
ameniletea mtu huyo.<br />
Omar alinijia, na akasema, “samahani. Je, hii ndiyo mara yako ya kwanza<br />
kuja hapa? Kwa hakika alikuwa na lahaja nzito.<br />
Nikasema; eenhe, ndiyo.<br />
“Oh, vizuri sana. Je, wewe ni Mwislamu?”<br />
“Hapana, nasoma kidogo tu.”<br />
“Oh, wewe unajifunza? Hii ndiyo mara yako ya kwanza kutembelea<br />
msikitini?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Njoo, acha nikuonyeshe sehemu hii.” Na akaninyanyua kwa mkono, nikawa<br />
natembea kwa nguvu ya mtu mwingine – tulikamatana mikono. Nilisema,<br />
Waislamu hawa ni marafiki. Kwa hiyo, akanionyesha maeneo hayo.