08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

35<br />

Katika siku za shule za hatua ya kwanza ya sekondari. Lile kanisa la<br />

Methodisti la mtaani lilifungwa, na tulikuwa tunahudhuria kanisa la<br />

Methodisti lilokuwepo katika mji wa karibu, ambalo ni kubwa kidogo kuliko<br />

lile la kitongoji alimokuwa akiishi. Hapo kwanza fikra zangu zilianza<br />

kutazama uchungaji kama unavyoitwa. Nikiwa mchangamfu katika ufuasi wa<br />

umoja wa vijana wa Methodisti, na hatimaye nikahudumia pande mbili, jimbo<br />

na uofisa wa mazungumzo. Pia nikawa muhubiri wa kawaida katika kipindi<br />

cha huduma kwa vijana siku za Jumapili kila mwaka. Mahubiri yangu<br />

yalianza kuongeza idadi ya washirika, na kabla ya muda kurefuka mara kwa<br />

mara nilikuwa najaza nafasi za membari za padri katika makanisa mengine,<br />

katika nyumba za uuguzi, katika usharika wa vijana wa makanisa mbali mbali<br />

na makundi ya akina mama, sehemu ambazo kwa aina yake, niliweka rekodi<br />

za mahudhurio.<br />

Nilipotimiza miaka miaka kumi na saba nilianza masomo ya mwaka wa<br />

kwanza chuo kikuu cha Harvard, uamuzi wangu wa kuingia uchungaji<br />

ulikuwa wa nguvu. Katika kipindi cha mwaka wangu wa kwanza chuoni<br />

hapo, nilijiandikisha katika kozi ya mihula miwili ya mlinganisho wa dini<br />

ambayo ilikuwa inafundishwa na Wilfred Cantwell Smith, aliyekuwa<br />

mtaalamu bingwa wa dini ya Kiislamu. Katika kozi hiyo, nilitoa mazingatio<br />

madogo kiasi kwa <strong>Uislamu</strong> kuliko dini nyinginezo, kama vile Uhindu na<br />

Ubudha, kwani hizo mbili za mwishoni zilionekana ni za faragha sana na ni<br />

ngeni sana kwangu. Ikiwa ni kinyume na <strong>Uislamu</strong>, ulionekana kuwa, kwa<br />

kiasi kidogo ni sawa sawa na dini yangu ya Ukristo. Kwa hiyo, sikutoa<br />

umakini mkali juu ya <strong>Uislamu</strong> kama inavyotakiwa, ingawa ninaweza<br />

kukumbuka kuandika waraka wa istilahi za hiyo kozi juu ya maana ya ufunuo<br />

katika Quran. Hata hivyo, kwa kuwa kozi hiyo ilikuwa ni moja ya kozi<br />

ngumu kabisa, kwa viwango vya kitaalamu, nilihitaji maktaba ndogo ya nusu<br />

dazeni ya vitabu vya Kiislamu, hivyo vyote viliandikwa na wasiokuwa<br />

Waislamu, na vyote vilikuwa ni vya kunihudumia kwa umadhubuti, miaka<br />

ishirini na tano baadaye. Pia nilihitaji tafsiri tofauti tofauti za maana ya Quran<br />

kwa Kingereza, ambazo nilizisoma kwa muda huo.<br />

Katika majira ya michipuo chuo cha Harvad kilinitangaza kuwa ni<br />

mwanazuoni mkali, akimaanisha kuwa, nilikuwa ni mmoja wa wanafunzi wa<br />

hali ya juu katika maandalizi ya theolojia chuoni hapo. Katika majira ya<br />

kiangazi ya mwaka wangu wa kwanza chuoni Harvard na mwaka wa pili,<br />

nilifanya kazi ya uchungaji kwa vijana walio katika kanisa kubwa kabisa la<br />

umoja wa Wamethodosti. Kiangazi kilichofuata, nilipata leseni ya kuhubiri

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!