You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
35<br />
Katika siku za shule za hatua ya kwanza ya sekondari. Lile kanisa la<br />
Methodisti la mtaani lilifungwa, na tulikuwa tunahudhuria kanisa la<br />
Methodisti lilokuwepo katika mji wa karibu, ambalo ni kubwa kidogo kuliko<br />
lile la kitongoji alimokuwa akiishi. Hapo kwanza fikra zangu zilianza<br />
kutazama uchungaji kama unavyoitwa. Nikiwa mchangamfu katika ufuasi wa<br />
umoja wa vijana wa Methodisti, na hatimaye nikahudumia pande mbili, jimbo<br />
na uofisa wa mazungumzo. Pia nikawa muhubiri wa kawaida katika kipindi<br />
cha huduma kwa vijana siku za Jumapili kila mwaka. Mahubiri yangu<br />
yalianza kuongeza idadi ya washirika, na kabla ya muda kurefuka mara kwa<br />
mara nilikuwa najaza nafasi za membari za padri katika makanisa mengine,<br />
katika nyumba za uuguzi, katika usharika wa vijana wa makanisa mbali mbali<br />
na makundi ya akina mama, sehemu ambazo kwa aina yake, niliweka rekodi<br />
za mahudhurio.<br />
Nilipotimiza miaka miaka kumi na saba nilianza masomo ya mwaka wa<br />
kwanza chuo kikuu cha Harvard, uamuzi wangu wa kuingia uchungaji<br />
ulikuwa wa nguvu. Katika kipindi cha mwaka wangu wa kwanza chuoni<br />
hapo, nilijiandikisha katika kozi ya mihula miwili ya mlinganisho wa dini<br />
ambayo ilikuwa inafundishwa na Wilfred Cantwell Smith, aliyekuwa<br />
mtaalamu bingwa wa dini ya Kiislamu. Katika kozi hiyo, nilitoa mazingatio<br />
madogo kiasi kwa <strong>Uislamu</strong> kuliko dini nyinginezo, kama vile Uhindu na<br />
Ubudha, kwani hizo mbili za mwishoni zilionekana ni za faragha sana na ni<br />
ngeni sana kwangu. Ikiwa ni kinyume na <strong>Uislamu</strong>, ulionekana kuwa, kwa<br />
kiasi kidogo ni sawa sawa na dini yangu ya Ukristo. Kwa hiyo, sikutoa<br />
umakini mkali juu ya <strong>Uislamu</strong> kama inavyotakiwa, ingawa ninaweza<br />
kukumbuka kuandika waraka wa istilahi za hiyo kozi juu ya maana ya ufunuo<br />
katika Quran. Hata hivyo, kwa kuwa kozi hiyo ilikuwa ni moja ya kozi<br />
ngumu kabisa, kwa viwango vya kitaalamu, nilihitaji maktaba ndogo ya nusu<br />
dazeni ya vitabu vya Kiislamu, hivyo vyote viliandikwa na wasiokuwa<br />
Waislamu, na vyote vilikuwa ni vya kunihudumia kwa umadhubuti, miaka<br />
ishirini na tano baadaye. Pia nilihitaji tafsiri tofauti tofauti za maana ya Quran<br />
kwa Kingereza, ambazo nilizisoma kwa muda huo.<br />
Katika majira ya michipuo chuo cha Harvad kilinitangaza kuwa ni<br />
mwanazuoni mkali, akimaanisha kuwa, nilikuwa ni mmoja wa wanafunzi wa<br />
hali ya juu katika maandalizi ya theolojia chuoni hapo. Katika majira ya<br />
kiangazi ya mwaka wangu wa kwanza chuoni Harvard na mwaka wa pili,<br />
nilifanya kazi ya uchungaji kwa vijana walio katika kanisa kubwa kabisa la<br />
umoja wa Wamethodosti. Kiangazi kilichofuata, nilipata leseni ya kuhubiri